Mkuu ni suala la muda tu, maana kama tokea mwaka 1972 sera ya Marekani imekuwa ni One China Policy na hata Trump na jehuri yake ameshindwa kubadilisha anajua kabisa kwamba ipo siku Taiwani itarudi Uchina.
Uingereza miaka yote alikuwa anatambua Tibet kama eneo huru nje ya Uchina lakini mwaka 2008 alijiunga na wenzake wa Umoja wa Ulaya kutambua kama Tibet ni sehemu ya Uchina. Hii ilitokea baada ya Uingereza kutambua kwamba anahitaji sana masoko na pesa za Uchina.
Taiwani ni suala la muda tu mkuu, hasa kipindi hiki ambacho Uchina imekuwa na nguvu kubwa ya kiuchumi duniani na ya kijeshi kule Pasifiki kuliko kipindi chochote cha historia yake.