tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergey Lavrov amesema kwamba Urusi haitakubali kurejesha ardhi iliyokwisha itwaa kutoka Ukraine katika mazungumzo ya kutafuta amani yanayotarajiwa kufanyika leo katika jimbo la Alaska nchini Marekani baina ya Rais Donald Trump na Rais Vladmir Putin.
Akizungumza katika mahojiano na Kituo cha CBS, Lavrov alikataa wazo la makubaliano yoyote ya kimaeneo katika usitishaji vita unaoweza kutekelezwa na Marekani, akidokeza badala yake Urusi inaweza kukubali kusitisha vita katika mstari wa mbele iwapo silaha za Magharibi zitasitishwa kupelekwa Ukraine.
Soma pia: Urusi yafanya mashambulizi makubwa ya anga nchini Ukraine
Tayari Rais wa Marekani, Donald Trump ameoneshwa katika vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa akijiandaa kukutana na Rais wa Urusi, Vladmir Putin katika juhudi za kusaka amani na kusitisha vita baina ya Urusi na Ukraine.
Akizungumza katika mahojiano na Kituo cha CBS, Lavrov alikataa wazo la makubaliano yoyote ya kimaeneo katika usitishaji vita unaoweza kutekelezwa na Marekani, akidokeza badala yake Urusi inaweza kukubali kusitisha vita katika mstari wa mbele iwapo silaha za Magharibi zitasitishwa kupelekwa Ukraine.
Soma pia: Urusi yafanya mashambulizi makubwa ya anga nchini Ukraine
Tayari Rais wa Marekani, Donald Trump ameoneshwa katika vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa akijiandaa kukutana na Rais wa Urusi, Vladmir Putin katika juhudi za kusaka amani na kusitisha vita baina ya Urusi na Ukraine.