URUSI: Mahakama ya Moscow yafuta Uamuzi wa Kamisheni ya Uchaguzi

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
May 27, 2016
5,416
7,828
Mahakama ya Moscow yafuta Uamuzi wa Kamisheni ya Uchaguzi

1565778717367.png

Sergei Mitrokhin

Mahakama moja katika mji mkuu wa Urusi, Moscow imefuta uamuzi wa kamisheni ya uchaguzi wa kumzuia mgombea wa upinzani, Sergei Mitrokhin kugombea katika uchaguzi wa mabaraza ya mji huo.

Taarifa zilizochapishwa na mashirika ya habari ya serikali ya Urusi, yamesema mahakama hiyo imeiamuru kamisheni ya uchaguzi kumsajili mara moja mwanasiasa huyo kutoka chama cha Yabloko, kinachofuata sera za mrengo wa kati.

Mamia kwa maelfu ya watu waliandamana mjini Moscow Jumamosi iliyopita, wakipinga kuenguliwa kwa wagombea wa upinzani na wa kujitegemea kwenye uchaguzi huo wa jiji.

Maandamano hayo yalifuata mengine kadhaa yaliyoanza mwezi Julai kuunga mkono wagombea binafsi katika baraza la jiji la Moscow.


Reuters Reports:
Moscow court allows opposition candidate to run after protest

MOSCOW (Reuters)
- The Moscow city court cancelled a decision by an election commission to bar a Russian opposition candidate, Sergei Mitrokhin, from running in a municipal election in September, TASS news agency reported.

The court ruled in favour of Mitrokhin three days after tens of thousands of protesters turned out at a rally in Moscow, in which Mitrokhin also took part.

A month of demonstrations over elections for the Moscow city legislature have turned into the biggest sustained protest movement in Russia since 2011-2013, when protesters took to the streets against perceived electoral fraud.



DW | Reuters | The Moscow Times
 
Maandamano ya watu wanaojielewa na kujua wanataka nini siku zote hufanikiwa
Hong Kong wamepata walichotaka.
Urusi wamepata pia. Sisi ndo hatujui twataka nini
 
Back
Top Bottom