Sheikh23
JF-Expert Member
- Jul 11, 2016
- 1,202
- 2,001
Wakuu habari ya muda huu, niende moja kwa moja kwenye tafakuri yangu, hizi bank za kibiashara zimekuwa zikitoza viwango tofauti vya gharama za kuchakata mkopo kwa wateja wake, gharama hizi hutofautiana kulingana na kiasi mteja anachokopa na muda wa mkopo huo (niko tayari kusahihishwa).
Sina uzoefu na mikopo ya kibiashara,au mikopo ya wajasiliamali, mathalani kwa mkopo wa watumishi wa umma ambao mtumishi huchakata yeye mkopo kupitia mfumo wa Ess, Afisa utumishi/Rasilimali watu huchakata tena taarifa na kuridhia mtumishi huyo akopeshwe, Bank humalizia jukumu la kumpatia mkopo mteja wao (mtumishi) baada ya utatu huo kukamilisha protocol zote, kama mchakato ni huo,processing fee ni sharti la kisheria toka BOT? Au ni sharti la kimkataba wa mkopo?
Nini mantiki haswa ya uwepo wa takwa hili/gharama hizi ilhali hakuna mizunguko ya upitishaji wa mkopo kama ilivyokuwa kabla ya mfumo wa Ess?
Kuna namna mikopo au kukopa kunakuwa kugumu na pengine jamii kuona kukopa ni jambo la hatari kwa sababu ya milolongo mingi, riba kubwa na kukosekana kwa elimu sahihi kwa jamii.
Nawasilisha,mwenye ufahamu anijuze.
Mbarikiwe.....wabillah tawfiq
Sina uzoefu na mikopo ya kibiashara,au mikopo ya wajasiliamali, mathalani kwa mkopo wa watumishi wa umma ambao mtumishi huchakata yeye mkopo kupitia mfumo wa Ess, Afisa utumishi/Rasilimali watu huchakata tena taarifa na kuridhia mtumishi huyo akopeshwe, Bank humalizia jukumu la kumpatia mkopo mteja wao (mtumishi) baada ya utatu huo kukamilisha protocol zote, kama mchakato ni huo,processing fee ni sharti la kisheria toka BOT? Au ni sharti la kimkataba wa mkopo?
Nini mantiki haswa ya uwepo wa takwa hili/gharama hizi ilhali hakuna mizunguko ya upitishaji wa mkopo kama ilivyokuwa kabla ya mfumo wa Ess?
Kuna namna mikopo au kukopa kunakuwa kugumu na pengine jamii kuona kukopa ni jambo la hatari kwa sababu ya milolongo mingi, riba kubwa na kukosekana kwa elimu sahihi kwa jamii.
Nawasilisha,mwenye ufahamu anijuze.
Mbarikiwe.....wabillah tawfiq