Upinzani umeongeza idadi ya majimbo?

Upinzani umeongeza idadi ya majimbo?

Mssassou

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2015
Posts
1,537
Reaction score
597
Vyama vinavyounda UKAWA vimefanikiwa kuongeza majimbo ya ushindi ktk uchaguzi wa mwaka huu au vimepoteza?
 
Matokeo ya 2010

Chadema wabunge wa kuchaguliwa 23 viti maalum 25. Jumla 48.
Cuf wabunge wa kuchaguliwa 24 viti maalum 10. Jumla 34.

Nccr kuchaguliwa viti 4 viti maalum 0
2015
Chadema wanategemewa kupata viti kati ta 33 na 35 vya kuchaguliwa. Viti maalum vitakuwa at least 30.

Cuf around 32 kuchaguliwa na around 15 viti maalum.

Nccr 1

Piga mahesabu ujue wamepanda au kushuka.
 
wamepanda lakini tulitegemea wabunge wa kuchaguliwa wasiwe chini ya 120 kwa kwa wana UKAWA
 
wamepanda lakini tulitegemea wabunge wa kuchaguliwa wasiwe chini ya 120 kwa kwa wana UKAWA

Dr,slaa aliongeza wabunge zaidi ya 20, lowasa ameongeza wabunge 11 ,hii ni pamoja na kuwepo kwa ukawa ,big politician mwenye ushawishi mkubwa kama ED ,kwangu mim naona ni kama msuli tembo ,majibu sisimizi
 
Vyama vinavyounda UKAWA vimefanikiwa kuongeza majimbo ya ushindi ktk uchaguzi wa mwaka huu au vimepoteza?

Mimi ni ccm na nafurahi chama changu kimeshinda ila kwenye ubunge nimefurahi sana wapinzani wamepata viti vingi na kwa mwaka huu upinzani umeongeza viti na siwezi kuingia kwenye mjadala wa kiongozi yupi wa upunzani kaleta viti vingi kwani nadhani hiyo sio hoja kubwa hapa.
Jambo la kujivunia sana ni wapinzani wawe wengi ili bunge liwe zuri na lenye manyfaa kwa watanzania
 
Slaa aliongeza viti 18 mwaka 2010.

Lowasa kaongeza viti 11 mwaka 2015.

Slaa alipata 27% ya kura za uraisi 2010.

Lipumba alipata 12% ya kura za uraisi 2010.

Ukichukua % za 2010 ukazijumlisha za slaa na Lipumba unapata 39%.

Lowasa ndani ya ushirikiano wa upinzani kapata 39%. ambayo ingekuwa sawa na jumla ya Lipumba na Slaa 2010.

Lowasa kasaidia kuingezea Cuf wabunge bara pia kasaidia kuiua Nccr bara.

Lowasa kasaidia kuongeza ruzuku ya chama ndani ya chadema,Lakini pia kasaidia kupunguza ruzuku katika vyama shiriki.

Kama ukichukua jumla ya ruzuku ya vyama vinavyounda ukawa kabla ya ushirikiano unaweza kukuta ipo sawa baada ya ushirikiano.

Lowasa kasaidia kukuza demokrasi pia na ushindani katika uchaguzi huu.

Pia Lowasa kafuta ajenda ya ufisadi katika baadhi ya vyama ndani ya uchaguzi huu.

Pia Lowasa katusaidia kuona rangi halisi za viongozi wetu.

Pongezi nyingi zimuendee ndugu Edward Lowasa kwa kuufikisha upinzani hapa ulipofikia.
 
Matokeo ya 2010

Chadema wabunge wa kuchaguliwa 23 viti maalum 25. Jumla 48.
Cuf wabunge wa kuchaguliwa 24 viti maalum 10. Jumla 34.

Nccr kuchaguliwa viti 4 viti maalum 0
2015
Chadema wanategemewa kupata viti kati ta 33 na 35 vya kuchaguliwa. Viti maalum vitakuwa at least 30.

Cuf around 32 kuchaguliwa na around 15 viti maalum.

Nccr 1

Piga mahesabu ujue wamepanda au kushuka.

CCM wanapenda namba hila hawajui hesabu,yote haya anayajua nashangaa dhumuni lake la kuuliza Hilo swali.
 
Dr,slaa aliongeza wabunge zaidi ya 20, lowasa ameongeza wabunge 11 ,hii ni pamoja na kuwepo kwa ukawa ,big politician mwenye ushawishi mkubwa kama ED ,kwangu mim naona ni kama msuli tembo ,majibu sisimizi
Ili uwe objective toa takwimu za Magufuli na Kikwete
 
Wapinzani Mwaka huh watakuwa na wabunge karibu mia moja,wakuchaguliwa na kuteuliwa
 
Kama DK slaa 2010 alipata kura Milioni mbili kapata viti maalum 25, lowasa kapata kura milioni sita...ni ongezeko maradufu
 
Kama DK slaa 2010 alipata kura Milioni mbili kapata viti maalum 25, lowasa kapata kura milioni sita...ni ongezeko maradufu
Maradufu wapi wewe,Wakati huo huo unasahau CCM wana ongezeko la Kura takribani milion 3.

Idadi ya wapiga kura imeongezeka tofautiu na 2010.

Hawatapata maradufu lakini wataongeza viti maalumu vingi.
 
Swali limeuliza idadi ya majimbo,hapa comments nyingi zinaeleza tathmini.(Mjadala mpana sana kutoka 85 to 61 to 58).
 
Slaa angegombea mwaka huu mbali ya kupoteza majimbo ya kanda ya ziwa UKAWA pia wasingepata majimbo ya Monduli,Longido, Simanjiro,Arumeru Magharibi na Siha.Haya majimbo yana wamasai wengi na walikuwa watiifu kwa CCM lakini waliamua kumfuata Lowassa. Kanda ya ziwa walipiga kura kwa ukanda kwa kuwa Magufuli anatoka huko hivyo ilikuwa vigumu sana UKAWA kutetea majimbo ya kanda ya ziwa.
 
Wakati slaa kafanya Kazi hiyo miaka zaidi 15
Lowassa kapaisha chama kwa miezi miwili tu.
 
Slaa angegombea mwaka huu mbali ya kupoteza majimbo ya kanda ya ziwa UKAWA pia wasingepata majimbo ya Monduli,Longido, Simanjiro,Arumeru Magharibi na Siha.Haya majimbo yana wamasai wengi na walikuwa watiifu kwa CCM lakini waliamua kumfuata Lowassa. Kanda ya ziwa walipiga kura kwa ukanda kwa kuwa Magufuli anatoka huko hivyo ilikuwa vigumu sana UKAWA kutetea majimbo ya kanda ya ziwa.
Kabisa, umesema la maana!
 
Back
Top Bottom