Kisima chetu
Member
- Nov 28, 2012
- 32
- 10
Habari zenu wanajamii,ningependa kuzungumzia kuhusu maneno hayo hapo juu, upendo ni uvumilivu,jamii yetu ya sasa imejaa mambo mengi yanayoikabili jamii kwa ujumla mambo mengi yanaongelewa kuhusu mahusiano,wake kutoka nje wanaume kuwa na nyumba ndogo na kutoridhishana kimapenzi,suala hilo kwa kweli limekua gumzo na dawa nyingi utasikia zinatangazwa za kuongeza nguvu za kiume,ndoa bila upendo wa kweli na kuvumiliana si ndoa hazitadumu ukiona ndoa imedumu miaka mingi ujue kuna uvumilivu wa hali ya juu sana,ikiwa ni pamoja na hayo ya ndani ya kutoridhishana,nawaomba sana wanawake wavumilie sana hizi hali za wenzetu kwani dunia ya sasa inamambo mengi sana yanawafanya washindwe kumudu tendo hilo hasa vyakula vyetu,utafutaji wa maisha watoto kusomesha majukumu kwa ujumla yanadhoofisha kwa kiasi kikubwa sana ufumbuzi wa tatizo hili ni uvumilivu tu hakuna kingine,kuweni wapole!