Updates: Special Thread Kagasheki Cup Bukoba!

Updates: Special Thread Kagasheki Cup Bukoba!

DJ Baraka

Senior Member
Joined
May 15, 2013
Posts
177
Reaction score
82
attachment.php



Yale mashindano ya Ligi ya jimbo cup maarufu kama Kagasheki Cup yanayodhaminiwa na Mbunge wa Bukoba mjini Balozi Khamis Kagasheki yameanza kutimua vumbi leo katika uwanja wa kaitaba mjini Bukoba.


Ligi hii ina shamra shamra kubwa katika mji huo kuliko hata ligi kuu ya Vodacom.


Uzinduzi wa ligi hiyo umefanywa na Kagasheki mwenyewe. Ambapo amesema msindi wa kwanza atapata sh milioni 5,mshindi wa pili milioni 3 na wa tatu milioni 1.5 aidha kila timu itapata sh 500,000 za usafiri kwa timu zote 14 zinazounda jimbo hilo.


Picha za uzinduzi na taarifa nyingine fuatilia thread hii itakayokuwa na update juu ya ligi hii hadi itakapomalizika.


....................Keep watching...............



DSC02451.JPG


DSC02474.JPG


DSC02494.JPG
 

Attachments

  • Kagasheki.PNG
    Kagasheki.PNG
    71.8 KB · Views: 66
Ligi hii iko chini ya Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi Marick Tibabimale na kuwa timu zote zitapata jezi na mipira tena vifaa vya kisasa ili vijana waweze kucheza soka kwa uzuri, Pia amewapatia jezi waamuzi wote watakoshiriki kuchezesha mechi.



Lakini pia atalipia posho zote za marefa watakaochezesha, Pia timu zote zitapata maji kwa ajili ya wachezaji
 
Timu zinazoshiriki ni 14 na leo ufunguzi ilikuwa Kata ya Bakoba na Kata ya Hamugembe

Matokeo
Bakoba 1 Hamugembe 0

Kesho
Rwamishenye Vs Buhembe
saa 10:00 jioni Kaitaba kama kawaida michezo yote iko LIVE kupitia 88.5 Kasibante FM radio
 
Niliposema Kagasheki ni zaidi ya Mbuge kuna watu walinuiponda! sasa wajitokeze hapa
umeniwahi kuweka hii,mkuu uko pande zip bk?
 
Kama nilivyosema kwenye ufunguzi,mashindano haya yawe ni sehemu ya kuziandaa timu za Bukoba mjini ili ligi ya wilaya itakapoanza apatikane bingwa mwenye kiwango cha kuweza kugombea ubingwa wa mkoa mwezi February mwakani.
Ninawatakia mashindano mema tukijaliwa nitakuwepo siku ya fainali mwezi August kama nilivyokuwepo kwenye ufunguzi.
 
Kama nilivyosema kwenye ufunguzi,mashindano haya yawe ni sehemu ya kuziandaa timu za Bukoba mjini ili ligi ya wilaya itakapoanza apatikane bingwa mwenye kiwango cha kuweza kugombea ubingwa wa mkoa mwezi February mwakani.
Ninawatakia mashindano mema tukijaliwa nitakuwepo siku ya fainali mwezi August kama nilivyokuwepo kwenye ufunguzi.

Karibu,hivi leo ni Kashai vs Bakoba mchezo wa leo ni issue nyingine,hakuna hata pa kutema mate kaitba .
dk ya 80 kipindi cha pili bao ni 1-1

big up Kagasheki
 
mpira kati ya Kashai na Bakoba umemalizika matokeo ni 1-1
jioni njema
 
Back
Top Bottom