wakati kuna watu wanauwawa kwa kuiba simu za mchina zenye samani ya 50000....hivi hizo bilioni zaidi ya 2 zinge pelekwa hospitalini au mashuleni zinge saidia kiasi gani? tuache unafiki
Tatizo lako unashindwa kuelewa kuwa mabunge yetu ndio yanayoweka hizi sheria na si mimi wala wewe. Labda mwenzangu ni mbunge.
Sheria zetu na nyingine nyingi duniani, zinazotungwa na watu (wabunge) zimejaa kulindana, hapo bungeni wale unaowaona usifikiri kuwa wako pale kwa maslahi yako wewe zaidi, wako pale kwa maslahi yao na kujilinda wao kwa wao, si wa upinzani wala wa chama tawala.
Hivi, umeshajiuliza ni kwanini wanaowaua waiba simu hawachukuliwi hatua? nini kinachowalinda? utakuta ni wewe mmoja wapo unaowalinda hao wauaji wa mitaani, akitokea mwizi akauliwa na wewe upo kwenye eneo, unajuwa kabisa ni fulani na fulani ndio waliomuuwa, lakini unakaa kimya huendi kuwashitaki wala kupeleka ushahidi. Halafu leo uozo huohuo unautolea mfano?
Wizi upo, haukuanza leo Tanzania hii, cha kutia moyo ni kuwa angalau kwa sasa tunaona hao wizi wa "EPA" wakifikishwa mahakamani. Kumbuka kuwa hii EPA ni madudu ya awamu iliyopita na walikuwepo watunga sheria pia, walikuwa wapi? mpaka aje Kikwete ndiyo ayaibuwe na kuisuka PCCB upya?, hivi kabla ya PCCB kulikuwa hakuna hivi vyombo vya kuzuwia rushwa? vilikuwa wapi? vilifanya nini? vilimfikisha nani mahakamani? majibu ni rahisi kabisa. Hakuna.
Leo hii yule anaechapa kazi na kuyaibuwa yote haya na kuchukuwa hatua stahiki za kubadilisha sheria za kulindana na kufumuwa mitandao ya huu wizi na mwingine ndiye anaonekana hafai. Ajabu sana.
Kumbuka kuwa sheria zimebadilishwa sana kipindi cha Kikwete zimeziba mianya mingi iliyopo awali na pia ukumbuke kuwa hivyo ni vita endelevu, ni uozo ulioota mizizi na kuuvunja na kuuondoa huo uozo kwa siku moja ni ndoto. Lakini matumaini yapo na ni mema sana na tumeona nia safi ya Kikwete katika awamu yake ya uongozi.