Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,183
- 2,100
Maafisa wa uokoaji walisimama kwa dakika moja ya kimya karibu na jengo la Sky Villa condominium, moja ya maeneo yaliyoathirika zaidi na tetemeko la ardhi la Machi 28, katika jiji la Mandalay mnamo Aprili 1, 2025.
Mamlaka nchini Myanmar zimefanya dakika moja ya kimya kuwakumbuka waathirika wa tetemeko kubwa la ardhi lililosababisha vifo vya zaidi ya watu 2,700, wakiwemo watoto 50 katika shule moja ya awali karibu na jiji la Mandalay.
Tukio hilo la kumbukumbu lililofanyika Jumanne linakuja wakati mashirika ya misaada yakiripoti kuwa jamii zilizoathirika zaidi zinakabiliwa na upungufu wa chakula, maji na makazi.
Tetemeko hilo la ardhi lenye ukubwa wa 7.7, lililotokea karibu na muda wa chakula cha mchana Ijumaa, ndilo kubwa zaidi kuwahi kutokea nchini humo katika zaidi ya karne moja, likiangusha pagoda za kale na majengo ya kisasa.
Kiongozi wa kijeshi wa Myanmar, Jenerali Mkuu Min Aung Hlaing, katika hotuba yake ya televisheni Jumanne, alisema idadi ya vifo imefikia 2,719 na huenda ikapita 3,000.
Alisema watu 4,521 wamejeruhiwa, na 441 bado hawajulikani walipo.
Watu wasiopungua 20 pia wamefariki katika nchi jirani ya Thailand.
-
Myanmar holds minute of silence as death toll from earthquake tops 2,700
Rescue officials observe a minute of silence near the Sky Villa condominium building, one of the sites most affected by the March 28 earthquake, in Mandalay on April 1, 2025
Authorities in Myanmar have held a minute of silence to honour the victims of a catastrophic earthquake that killed more than 2,700 people, including 50 children at one preschool near the city of Mandalay.
The moment of remembrance on Tuesday came as aid groups said communities in the hardest-hit areas were struggling to find food, water and shelter.
The magnitude 7.7 earthquake, which hit around lunchtime on Friday, was the strongest to hit the Southeast Asian country in more than a century, toppling ancient pagodas and modern buildings alike.
Myanmar’s military leader Senior General Min Aung Hlaing, in a televised address on Tuesday, said the death toll had reached 2,719 and could even exceed 3,000.
He said 4,521 people were injured, and 441 were missing.
At least 20 people were also killed in neighbouring Thailand.
Source: Al Jazeera
Mamlaka nchini Myanmar zimefanya dakika moja ya kimya kuwakumbuka waathirika wa tetemeko kubwa la ardhi lililosababisha vifo vya zaidi ya watu 2,700, wakiwemo watoto 50 katika shule moja ya awali karibu na jiji la Mandalay.
Tukio hilo la kumbukumbu lililofanyika Jumanne linakuja wakati mashirika ya misaada yakiripoti kuwa jamii zilizoathirika zaidi zinakabiliwa na upungufu wa chakula, maji na makazi.
Tetemeko hilo la ardhi lenye ukubwa wa 7.7, lililotokea karibu na muda wa chakula cha mchana Ijumaa, ndilo kubwa zaidi kuwahi kutokea nchini humo katika zaidi ya karne moja, likiangusha pagoda za kale na majengo ya kisasa.
Kiongozi wa kijeshi wa Myanmar, Jenerali Mkuu Min Aung Hlaing, katika hotuba yake ya televisheni Jumanne, alisema idadi ya vifo imefikia 2,719 na huenda ikapita 3,000.
Alisema watu 4,521 wamejeruhiwa, na 441 bado hawajulikani walipo.
Watu wasiopungua 20 pia wamefariki katika nchi jirani ya Thailand.
-
Myanmar holds minute of silence as death toll from earthquake tops 2,700
Rescue officials observe a minute of silence near the Sky Villa condominium building, one of the sites most affected by the March 28 earthquake, in Mandalay on April 1, 2025
Authorities in Myanmar have held a minute of silence to honour the victims of a catastrophic earthquake that killed more than 2,700 people, including 50 children at one preschool near the city of Mandalay.
The moment of remembrance on Tuesday came as aid groups said communities in the hardest-hit areas were struggling to find food, water and shelter.
The magnitude 7.7 earthquake, which hit around lunchtime on Friday, was the strongest to hit the Southeast Asian country in more than a century, toppling ancient pagodas and modern buildings alike.
Myanmar’s military leader Senior General Min Aung Hlaing, in a televised address on Tuesday, said the death toll had reached 2,719 and could even exceed 3,000.
He said 4,521 people were injured, and 441 were missing.
At least 20 people were also killed in neighbouring Thailand.
Source: Al Jazeera