Upasuaji wa vidonda vya tumbo

Upasuaji wa vidonda vya tumbo

Zombi Mweusi

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2017
Posts
1,076
Reaction score
2,161
Habari wakuu kuna huu ugonjwa unatesa wa vidonda vya tumbo nimetumia dawa za kila aina nahisi kuchoka,

Naombeni msaada wa kujua kwa hapa Tanzania kuna huduma za upasuaji wa vidonda vya tumbo,hospital hata za mkoa naweza pata huduma hio na gharama zake zikoje

Natanguliza shukrani

Note: Nahitaji gharama za upasuaji na sio dawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Imejirudia
Mkuu pole sana je umefanya operesheni ya vidonda vya tumbo vimejirudia tena?tangu lini kuna operesheni ya vidonda vya tumbo? Nitafute kwa wakati wako ili nipate kukutibu maradhi yako ya vidonda vya tumbo ili uweze kupona maradhi yako uguwa pole.
 
Vidonda vya tumbo havitibiwi kwa operation unless mtu amepata complications kama perforation
Je unajua hivyo vidonda vimesababishwa na nini, hii itasaidia kutibu tatizo
 
Mkuu pole sana je umefanya operesheni ya vidonda vya tumbo vimejirudia tena?tangu lini kuna operesheni ya vidonda vya tumbo? Nitafute kwa wakati wako ili nipate kukutibu maradhi yako ya vidonda vya tumbo ili uweze kupona maradhi yako uguwa pole.
Sijawahi kufanyiwa upasuaji ila dokta kuna dawa nilishanunua kwako hapa jamatini dodoma nimetumia sana lakini wapi asa una dawa gani tena mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee, Ina mana dawa zote zimeshindikana?.. pole Sana.
 
Pole sana..Mungu akusaidie kupata tiba sahihi
 
Sorry!
Unataka kupona vidonda vya tumbo au unataka upasuaji?
 
Pole, pia waweza mtembelea Mwamposa, Suguye au Kuhani Musa na wengineo wa hapo Dar.

Hao watakupatia upasuaji rahisi wa bei nafuu, hata kama hauna chochote bado watakufanyia upasuaji wa vidonda hivyo.
 
Mkuu hebu jaribu hii kitu mm imenipa nafuu
Chukua
1. Habat soda
2. Black seed ya unga
3. Tende kilo moja
3. Maziwa fresh
Cha kufanya ondoa mbegu kwenye tende , chemsha maziwa hadi yachemke
Chukua kijiko cha wali pima viwili unga wa habat na black seed halafu tende punje 20 ublend huu mchanganyiko
Utakuwa unakunywa glas moja kila kabla nusu saa ya mlo wako
Pia uzingatie masaa ya kula
 
Mkuu hebu jaribu hii kitu mm imenipa nafuu
Chukua
1. habat soda
2. Black seed ya unga
3. Tende kilo moja
3. Maziwa fresh
Cha kufanya ondoa mbegu kwenye tende , chemsha maziwa hadi yachemke
Chukua kijiko cha wali pima viwili unga wa habat na black seed halafu tende punje 20 ublend huu mchanganyiko
Utakuwa unakunywa glas moja kila kabla nusu saa ya mlo wako
Pia uzingatie masaa ya kula
Mkuu asante sana kwa msaada wako ila nilishatumia vimenianza 2008 mpaka sasa navokwambia hakuna rangi ya dawa sijaona hasa hizi za asili ndomana nimefikia hitimisho kama kuna upasuaji wa hii kitu mnijuze tu na gharama zake pia maana gharama za hiyo miaka kama ningefanya upasuaji nahisi zisingefika
Nawaza tu baada ya mateso hadi kufikilia huduma ambazo labda hazipo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu asante sana kwa msaada wako ila nilishatumia vimenianza 2008 mpaka sasa navokwambia hakuna rangi ya dawa sijaona hasa hizi za asili ndomana nimefikia hitimisho kama kuna upasuaji wa hii kitu mnijuze tu na gharama zake pia maana gharama za hiyo miaka kama ningefanya upasuaji nahisi zisingefika
Nawaza tu baada ya mateso hadi kufikilia huduma ambazo labda hazipo

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu samahani lakini kama ntakukwaza maana umesema umeshatumia sana dawa za asili ila naomba nikuulize kipindi chote hicho umejaribu kutumia mbegu ya parachichi!!!? maana mimi pia nilikuwa muhanga wa huo ugonjwa
 
Mkuu samahani lakini kama ntakukwaza maana umesema umeshatumia sana dawa za asili ila naomba nikuulize kipindi chote hicho umejaribu kutumia mbegu ya parachichi!!!? maana mimi pia nilikuwa muhanga wa huo ugonjwa
mbegu ya parachichi inatumikaje mkuu mimi pia ni muhanga wa vidonda vya tumbo sina amani.
 
mbegu ya parachichi inatumikaje mkuu mimi pia ni muhanga wa vidonda vya tumbo sina amani.

unanunua parachichi kisha ile ibegu yake unaisaga vizuri alafu unaianika juani kisha unakuwa unakunywa kwenye chai au maji ya moto ambapo utakuwa unachota ule unga wake vijiko viwili au vitatu mimi imenisaidia sana pamoja na ndugu zangu
 
unanunua parachichi kisha ile ibegu yake unaisaga vizuri alafu unaianika juani kisha unakuwa unakunywa kwenye chai au maji ya moto ambapo utakuwa unachota ule unga wake vijiko viwili au vitatu mimi imenisaidia sana pamoja na ndugu zangu
Asante sanaa mkuu dozi ni kwa muda gani na kutwa au kwa siku mara ngapi kwa muda gani?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom