Upasuaji bila ridhaa inaruhusiwa??

Chinengu

Member
Joined
Jan 20, 2019
Posts
92
Reaction score
85
Amani iwe juu yenu waungwana.
Husika kichwa cha habari hapo juu,ningependa yupeane ufafanuzi kidogo juu ya swala hili.
Nijuavyo Mimi,mgonjwa anazo haki zake za msingi,mfano kupendekeza,kuchagua au kukataa kutibiwa na dr Fulani kwasababu zake mwenyewe,nk.
Sasa kwakuwa elimu ni pana sana yapo ambayo wengine munayafahamu wengine hatuyajui.
Kumezuka utaratibu katika hospital ya wilaya Newala ambao ni mpya na waajabu sana,mfano ukiwa na mjamzito ambae wao madaktari wataamini anahitaji upasuaji basi atafanyiwa upasuaji pasipo kushitikishwa/kuhusishwa au kupata ridhaa ya mgonjwa/mume au nfugu yeyote.
Na ikitokea kafanyiwa huo upasuaji hamruhusiwi kwenda wodini kumuona mgonjwa wenu hadi yeye mwenyewe apate nafuu ndio atoke aje kuwaona nyie nje.
Pia iwapo mna mjamzito na akafanikiwa kujifungua hamruhusiwi kwenda kumuona yeye wala mototo hadi aruhusiwe.
Sababu yao kubwa wanadai wanaogopa wagojwa kurogwa vifonda ya operation visipone au kurogwa ili vichanga vife,binafsi siioni sababu ya msingi Ila naona kuna fursa kwao ama kuiba watoto,viungo vingine vya mwili,kupiga dili za kuuza watoto wa jinsia Fulani na kuwawekea akina mama watoto ambao si wao.
Yu

Tusaidiane kupeana maarifa jaman swala hili lipo kiharali au ndio tunaanza biashara mpya mahospitalini?
 
Jib ni ndiyo kama ni emmergency kuokoa maisha ya mama na mtoto.
Tofauti na hapo jib ni HAPANA.

[emoji375][emoji375]
 
Jib ni ndiyo kama ni emmergency kuokoa maisha ya mama na mtoto.
Tofauti na hapo jib ni HAPANA.

[emoji375][emoji375]
Dharura gani ya kutotaarifiwa mgonjwa anaejitambua?
 
Daktari ana uwezo wa kuamua kufanya au kuchagua matibabu ya mgonjwa wake bila consent au ridhaa ya mgonjwa mwenyewe au ndugu zake kama anaona hali ya mgonjwa ni mbaya sana na hakuna njia nyingine ya kumsaidia isipokua anayotaka kufanya ila katika hali ya kawaida mgonjwa na shahidi (ndugu) hujaza consent form kabla ya upasuaji.
Kuhusu kuzia kumuona mgonjwa hiyo inawezekana ukawa ni utaratibu wa hospitali husika na ni kweli kwamba watu kumtembelea ovyo mgonjwa ni risky kupata infections kwenye kidonda, ni kweli pia kuna jamii zingine watu hutumia tiba asili kuponesha haraka kidonda hivyo kupelekea infections na ni hatari kweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hicho kitakua kilikua kifafa cha mimba mkuu.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…