UONGOZI MKUU WA UDOM ACHENI UONEVU HUU

UONGOZI MKUU WA UDOM ACHENI UONEVU HUU

hizi barua wanaandka wale walolipa ada na michango mingne....lakn kama umelipa michango mingne bila ada hupatiwi matokeo
Utapatiwaje matokeo bila kulipa ada wewe? NECTA usipolipia hela ya mtihani hata kama umelipa michango ya shule watashikilia matokeo hadi ulipe!
Na utaratibu umeshatolewa kama nilivyokueleza awali kuwa loan officer yupo bodi anashughulikia majina ya wale ambao hawakusaini ada zao.
Hata ingekuwaje matokeo huwezi kuyaona hata kama unalipiwa na bodi kama hujasaini kwenye ile sheet board!
Unataka uoneshwe matokeo kabla hujasaini, unaujua utaratibu wa bodi unavyolipa hela za wanufaika wake kwa vyuo? Hata kama mimi ndiye ningekuwa VC, au VC academic nisingekuruhusu uone matokeo bila kusaini. Wewe saini tu uwaachie chuo wadai hela yao bodi nawe upate halali yako.

Kubwa kuliko umeshaambiwa uongozi wenu umekutana na management wakakubaliana kama walivyowapa taarifa halafu wewe huwaamini pengine labda una uongozi wako unaohisi ndio una mamlaka zaidi katika kushughulikia suala lako. Kama unaona UDOSO hawafanyi kazi au hawaaminiki basi utakuwa na godfather wako unayemwamini zaidi.

Muhimu kuwa mpole fuata yale wanayokuelekeza viongozi wako suala lako ni la kawaida litashughulikiwa na kama unahisi kuna kozi fulani una sup kutwa unajifua taratibu maana hata sup hizi zikikupita bado huwa kuna special sup pia unaweza kufanya.
 
umeelewa nilichokiandika?? au umejibu kutokana na mihemko yako kwa sabab ww ni staff wa udom???

nmekwambia chuo hakikumuombea ada bodi ,afu ww unakuja kusema et hakusain ada sasa atasain nn na jna halijaja?

pili unasema bodi haikatai kulipa unaujua utaratbu wa malipo kutoka bodi???? hebu acha mihemko kama hujui unachokizungumza

?
Mkuu mosi tambua kuwa mimi ni raia huru ninayesema uhalisia wa mambo wala sina mafungamano yoyote na UDOM ila kesi zenu wanafunzi wa vyuo nyingi nimewahi kukutana nazo, kama ingekuwa uonevu ulio wazi ningeungana nawe kuukemea ila hapa sijaona uonevu zaidi ya kukuona mpiga majungu tu kwa taasisi hiyo. Sijawahi na sitegemei kama nitakuja kuwa mwanajumuia wa UDOM either kwa kusoma hapo au kuajiriwa.

Pili hata kama jina halikuja umeshaambiwa na uongozi wako wa wanafunzi chuo kinavyoshughulikia suala hilo. Ina maana hukuamini taarifa hiyo hadi ukaja huku kuzushia hata yasiyohusika huku ukijua hoja yako kuu ni kushikiliwa matokeo yako? Acha fitina lenga kwenye pointi muhimu ya matokeo yako ova!

Tatu unaniuliza kama najua utaratibu wa namna bodi inavyolipa hiyo hela na unajiaminisha kuwa mimi sijui na wewe unajua. Kama ulikuwa unajua utaratibu huo kwa nini hukushughulikia mapema? Kwanza UDOM niwalaumu kwa uzembe mkubwa waliofanya kwa kutoshikilia matokeo yako ukiwa mwaka wa kwanza pale tu uliposhindwa kusaini kutokana na sababu unazozijua wewe, na pengine ungeshughulikia mapema usingefika hadi mwaka wa tatu hujasolve tatizo hili. Ungedisco mwaka wa pili hela hii ingelipwaje, katika hili wanatakiwa wajifunze na warekebishe vinginevyo watendaji kama hawa watakuwa wanazisababishia hasara taasisi za serikali!

Wito wangu kuwa mpole suala lako linawezekana kushughulikiwa na lipo ndani ya uwezo wa UDOSO na UDOM pia, fuata maelekezo!
 
Back
Top Bottom