Uongo una mwisho

Uongo una mwisho

Hassan Longoi

New Member
Joined
Apr 28, 2015
Posts
3
Reaction score
7
UONGO UNA MWISHO

Katika historia ya Tanzania kisiasa hakuna chama cha upinzani ambacho kimeshambuliwa kwa muda mrefu kwa hoja za UONGO kama CDM nitazitaja kwa uchache:-

UKANDA,
CDM ilihusishwa na kanda ya kaskazini kisa tu waanzilishi wake wametoka huko lkn hoja hii haina mashiko!

Tena imejibiwa na CDM kwa kutaja kanda zake zisizopungua nane km kanda ya Kati, ziwa,juu kusini,kaskazini,pwani n.k

Chadema ina matawi na wafuasi mpaka ulaya Mf USA,Uingereza achilia nchi jirani. Je hawa na matawi yao nao wako kanda ipi?

CCM Oct 2015 UKAWA(CDM, CUF, NCCR,NL)' itawafuta povu mdomoni...

DINI,

Vyama vilivyo jeruhiwa na uongo huu ni CDM na CUF. Chadema ikibambikizwa na ukristo na Cuf ikihusishwa na uislamu, sasa ukawa umeunganisha makundi haya ya kijamii na Nccr & Nld pengine wanawakilisha wasio na wanaotarajia kuwa na dini sasa CCM oct 2015 itapigiwa kura na nani?

FUNZO
vyama Viwe na falsafa, itikadi za kueleweka kwa watawaliwa sio kujiendesha kiujanjajanja na ulaghai igeni hata USA km unatetea maskini (Democratic ) au matajiri (Republican) kieleweke hivyo muda wote

Sio kama ccm imejinadi kutetea wakulima na wafanyakazi matokeo yake imekumbatia wafanyabiashara imeacha wateja wake barabarani nakuja na siasa za msimu za udini ambazo si lazima uwe na dini

UKABILA
Chadema imebamizwa sana na huu uongo! Kwamba Chadema ni ya wachaga bila kujua au ni kwa makusudi kwamba Tundu Lisu,Dr slaa,Halima Mdee, Sugu nk si wachaga na sasa nchi nzima CDM imejaa viongozi wa makabila Karibu yote Tanzania!!

Ndiyo angalia wenyeviti,katibu ktk mikoa na wilaya na ngazi zingine mpaka vitongoji na mitaa. Looo wanalo mwaka huu!

Kweli!! hebu angalia baadhi ya watia nia 2015 wasio wachaga Mbasa(ulanga magh), Djumbe (sgd kask),Hassani Longoi (Iramba magh), Vicent, Hemedi, Khangaa, Christowaja (Sgd Magh ), Omari Longoi, Mwita na Aisha (Sgd mjini) kwa uchache tu wanatosha. Hoja ya ukabila nani atakuelewa?

Funga kazi umoja wa UKAWA Sijui hata kabila lililoachwa

CCM mtapona kweli Oct 2015? Naona Giza mbele upande wenu!!

CHADEMA NI SACCOS

Hivi ni SACCOS gani husajiliwa na msajili wa
vyama vya siasa? hivi unaposimama mbele ya watu hata kama ni wawili kwa hoja hii watakuelewa kweli? chama kina miaka zaidi ya 22 bado unatumia uongo na ulaghai ukitegemea utavuna kura? Wapinzani wa ukawa endeleni kuoga upepo

UNDUGU (Nepotism)

Bado ni mapema sana kulaumu chama chochote cha upinzani kuwa kinajiendesha kwa kufahamiana kwani waanzilishi lazima mfahamiane kwanza ndiyo muanzishe wazo na baadaye litawanyike sehemu mbalimbali na usalama Wenu pia!! Huwezi kuanzisha Jambo ukiwa Mtwara bila kuwashirikisha wanamtwara kwanza ukamuota Mwita wa Musoma ambaye haujui hata kama yupo mtu wa aina hiyo umpe uongozi!! Muda wao ukifika tutawaambia ingawa kuna wengine umri umeanza kukaribia. CCM ni halali kuambiwa ukweli huu

Don't complain about the snow on your neighbor's roof, when your own doorstep is unclean!!

Hassani Longoi
 
Chadema wamebariki wizi wa kuwaibia watanzania bilioni 18 kupitia posho za wabunge. Chadema ni wezi,mafisadi hawana huruma kwa watanzania.
 
Chadema wamebariki wizi wa kuwaibia watanzania bilioni 18 kupitia posho za wabunge. Chadema ni wezi,mafisadi hawana huruma kwa watanzania.

umesahau escrow bilion 350? Hebu kuwa na akili,unajua unapoitetea ccm kwa kitu cha kijinga hata watu wanakudharau,we unafkr nani hajui issue ya escrow? Ufisadi kibao ccm
 
Chadema wamebariki wizi wa kuwaibia watanzania bilioni 18 kupitia posho za wabunge. Chadema ni wezi,mafisadi hawana huruma kwa watanzania.

Kweli.kabisa... Ndo hao Chadema wamefanya yafuatayo
1. Epa chadema walihusika
2. Yule aliyejiizia mgodi wa makaa ya mawe ni mwanachadzma
3. Epa Wote wanachama wa chadema
4. Escrow wahusika Wote ni chadema
5. Meremeta ni chadema
6. Loriondo imeuzwa na chadema
7. Ishu ya sukari iliyo chinichini ni ya chadema
8. Walioahidi grid ya taifa Songea... Meli... Hospitali za rufaa ni chadema
9. Waliowaleta net solution kwa tanesco ni chadem
10. Waliouza NBC ni chadema
11. Waliokuwa wavuliwe magamba ni chadema
12. Etc
 
Chadema wamebariki wizi wa kuwaibia watanzania bilioni 18 kupitia posho za wabunge. Chadema ni wezi,mafisadi hawana huruma kwa watanzania.

waanzilishi wa hilo wazo la kuwaibia watanzania ni akina nani?wachovu nyie.
 
umewapa za uso mkuu. Acha wateketee na kama mwaka huu watapata hata wabubge watano ni sawa na tembo kupenya tundu la sindano
 
Chadema wamebariki wizi wa kuwaibia watanzania bilioni 18 kupitia posho za wabunge. Chadema ni wezi,mafisadi hawana huruma kwa watanzania.

Zile kura za kipumbafu za NDIYOOOOO kuunga hoja za kijinga mjengoni hufanywa na CHADEMA? Ficha usengerema wako acha kujiaibisha.
 
Zile kura za kipumbafu za NDIYOOOOO kuunga hoja za kijinga mjengoni hufanywa na CHADEMA? Ficha usengerema wako acha kujiaibisha.

Ndugu kuna wasengelema waneolewa na chama cha majizi humu...hata usemeje hayaelewi
 
Chadema wamebariki wizi wa kuwaibia watanzania bilioni 18 kupitia posho za wabunge. Chadema ni wezi,mafisadi hawana huruma kwa watanzania.

mkuu imenisikitisha sana,yani hakuna mbunge hata mmoja wa chadema anayepinga hizi posho ,ndio maana vijana wengi hatupigi kura kwa upuuzi huu
 
Back
Top Bottom