Dickson Ng'hily
JF-Expert Member
- Oct 22, 2010
- 451
- 485
Chai ni nzuri zaidi,maji yakiwa ya uvuguvugu nayo pia ni mazuri .Soda si nzuri.Faida ya chai au maji ya moto ni kuyeyusha mafuta,ila soda au maji baridi hugandisha na hivyo kufanya umengenyaji wa chakula kuwa tatizo.
Wakubwa naomba mnifunze kitu hapa, nimekuwa nikisikia kuwa unywaji wa maji wakati unakula au mara baada ya kula sio mzuri. Inasemekana unahitajika kupumzika walau saa moja kisha ndo unywe maji...Sasa swali langu ni hili, je unywaji wa chai wakati unakula unamadhara gani! Coz binafsi napenda kimiminika cha moto nikiwa nakula au mara baada ya kula. Au unywaji wa kimiminika cha baridi iwe soda au juice! Kwani tatizo ni maji kwa maana ya maji au tatizo ni kimiminika! Mwenye ufahamu na hili tafadhari anisaidie....
Habari kaka Ng'hily, huwa nakufuatilia michango yako kule kwenye jukwaa la siasa, nafurahi kukuona na huku pia!
Kiukweli maji hayajawahi kuwa na tatizo lolote ukinywa wakati wa kula au soon baada ya kula (provided huna matatizo ya figo ambapo kiasi cha maji ya kunywa kinakuwa limited). Mwili wa binadamu unahitaji lita 2 - 2.5 za maji kila siku, kiasi ambacho wengi wetu ni vigumu kukifikia, chakula ni chanzo kimojawapo cha maji hivyo kunywa maji wakati wa kula hakuna madhara yeyote wala hakukatazwi kiafya. Maji ya moto au baridi haijalishi, inategemeana na hali ya hewa tu. lakini chakula huwa kinakaa tumboni kwa masaa 3 - 4 kikichanganywa na vimeng'enyi mbali mbali katika joto maalum ambalo vimeng'eny hivyo vinaweza fanya kazi vizuri, hivyo hata ukinywa maji baridi bado yatapashwa kufikia kiasi cha joto linalohitajika kunyonywa mwilini. Na maji baridi hayazuii mafuta kumeng'enywa au kunyonywa tumboni/mwilini.
Chai ningekushauri unywe masaa 2 hadi matatu baada ya mlo mkuu..Chai ina kitu kinaitwa 'tannins', hii kemikali huwa inazuia unyonywaji mzuri wa chakula hasa 'micronutrients' kama madini (iron) na vitamins. Kahawa ina tannins kidogo sana kulinganisha na chai, bora unywe kahawa kuliko chai kama ni lazima muda mfupi baada ya kula.
Juice pia kama ilivyo kwa maji haina tatizo lolote, iwe baridi au moto haizuii chakula chako kunyonywa vyema.
Riwa
Asante sana maana kuna mtu mmoja alikuwa anatangaza kuwa huruhusiwi kunywa maji baada ya kula.
Asante sana kwa shule hii kaka
kuna ukweli wowote juu ya kupata kitambi kwa kutokana na kunywa maji mengi!Nitashukuru kwa majibu kaka...
Kaka Ng'hily...hakuna ukweli wowote kuhusu kupata kitambi kutokana na kunywa maji mengi. Kama huna matatizo ya mafigo, kunywa maji mengi lita mbili au zaidi ni nzuri sana kwa afya yako.
Kitambi au kunenepa kwa ujumla kunasababishwa na mwili kupata (kupitia chakula) energy (calories) nyingi kuliko unavyozitumia na hivyo mwili kuweka ziada, Energy au calories hizo uhifadhiwa katika mfumo wa mafuta ambayo hudeposit kwenye kuta za tumbo, makalio na hips hasa kwa wanawake lakini hata wanaume, ndani ya tumbo na hata kuzunguka moyo...na mafuta mabaya zaidi ni yale yanayojilimbikiza katika damu hasa low density cholesterol.
Vaykula vyenye calories nyingi kiasi cha kurisk mwili kujilimbikiza mafuta kwa wingi ni vyakula vya wanga (starch) na vyakula vyenye mafuta...Maji hayana starch na wala hayana mafuta, hivyo kwa namna yeyote ile maji hayawezi kusababisha mwili ulimbikize mafuta (energy/calories). Kunywa maji kati ya lita 2 - 2.5 kila siku kwa afya yako.
Kaka Riwa....Nakushukuru sana kwa darasa, ukweli umenifungua sana tena kupita maelezo na Mungu akubariki kaka...Naamini darasa hili limesaidia wengine pia...Kaka me maji nakunywa sana ila nilishituliwa na huyo jamaa kwa radio kuwa haifai kunywa maji wakati wa chakula na baada ya chakula na jamaa alikuwa anatumia lugha mbaya mpaka unaogopa....Hili la kitambi ni hisia zangu coz nilidhani ukinywa maji mengi yanasababisha tumbo kutanuka..Kama nilivyosema me ni mnywaji wa maji na ninaweza kunywa hata lita nane kwa siku coz kwa seating moja huwa nakunywa maji kama lita 1.5 na home nina kikombe cha lita 1.5 ambacho huwa nakitumia kunywa maji...Nway, asante sana kaka..
wingi wa maji inategemea yanatumikaje mwilini! kama anaongea sana, anatembea sana, anawakiwa na jua sana ama anatoa jasho sana ni sawa. idadi ya lita alizotaja ni kwa watu wa kazi ngumu sana juani!
Kaka me maji nakunywa sana ila nilishituliwa na huyo jamaa kwa radio kuwa haifai kunywa maji wakati wa chakula na baada ya chakula na jamaa alikuwa anatumia lugha mbaya mpaka unaogopa
Kaka Ng'hily hapo kwenye radio na niongezee tv nadhani Tanzania tunakosa udhibiti, na partly lawama nizielekeze kwetu sisi wadau wa afya, taasisi za afya, chama cha madaktari Tanzania, chama cha wauguzi Tanzania, wizara ya afya kitengo cha elimu ya afya kwa jamii, na zaidi kwa vyombo vya habari. Sources za habari sahihi kuhusu mambo yahusuyo afya yapo ( kwa kuliona hilo sasa hizi mimi na wadau wengine tupo katika mchakato wa kusaidia wizara ya afya kitengo cha elimu ya afya kwa jamii kutengeneza 'digital library' ambapo information nyingi kuhusu afya na tafiti mbali mbali zitapatika kwa easy referrence). Baadhi vyombo vya habari havijishughulishi kupata taarifa sahihi wakati wa kuandaa vipindi, na wanapoalika watu ambao wanatoa tiba mbadala hawawahusishi watu wa kitengo cha wizara ya afya ya tiba za asili/mbadala Muhimbili.
Hii inapelekea watu kuwa huru kutoa taarifa zisizo na ukweli na zisizofanyiwa utafiti kuthibitisha ukweli wake kwa jamii. Kilikuwa na watu kama kina mama Terry kwenye mambo ya lishe (kuna vitu alikuwa anasema vya ukweli na manufaa lakini vingine si kweli na pengine hata madhara), walikuja akina Ngoka 11 na dawa moja inayotibu magonjwa zaidi ya 100 n.k, na sasa kuna akina Isaac Ndodi na wengine kama huyo uliyemsikia....lakini hakuna udhibiti wa nini wanasema hawa watu hata kama kina athari kwa afya za watu wanaowasikiliza na kufuata wasemayo.
Taasisi mbali mbali za kitaalam za afya ikiwemo chama cha madaktari Tanzania na wizara ya afya kitengo cha elimu kwa afya ya jamii hawarespond kwa taarifa zisizo za kweli zinazotolewa na watu hawa, na kutoa ukweli uliothibitishwa kisayansi..matokeo yake wanajamii wanafuata na pengine baadhi yao wanaathirika.
Zamani watu walikua wana changia maada kwa kuheshimiana kweli.
Sio siku hizi, unalikuta limtu kama Wangari Maathai linabwatuka tu.