Sugar wa Ukweli
JF-Expert Member
- Jun 25, 2009
- 373
- 37
Da umenikumbusha mbali mkuu,enzi zile nilikuwa na demu korogwe girls,karatasi lazima iwe ya rangi rangi,mwandiko wa kuremba,michoro ya kufa mtu alafu lazima apulizie perfume.vitu kama hivi ndo huwa vinanifurahisha kwenye mapenzi mpaka leo ninazo hizo barua
Nakumbuka Kuna binti fulani kidato cha 5 alijinyoonga baada ya kutumiwa barua ndan yake wameandika kwa toilet paper then mchizi akajichambia. Binti alikua amegombana na mpenz wake wakaachana. Tarime sec hyo!
Hahaaaaa, umenifanya nichangie fasta hii thread maana juzi nilikua nawafundisha wanafunzi wangu mahali fulani nikawaambia kuwa hawajui kuandika essay kwasababu wao siku hizi wanategemea sms ambazo zimefupishwa kiasi kwamba huwezi jua hata maana yake. Enzi hizo nipo pale Magamba Boys now ( SeKUCo- Sebastian Kolowa University College-Lushoto) ndio nilikua nafanya dili za kuwaandikia washkaji barua halafu wananilipa....serious nilikua bingwa wa kuandika hizo barua hasa kwa lugha ya kigeni maana zilikua zinaenda Mazinde Juu ( St.Mary's) au Kifungilo Girls' ambako ndio by then kulikua na watoto wakali kinoma na ngeli inapanda sana, sasa ukiaka uwapate lazima uandike barua kwa kiingereza.
Nilikua naenda kununua karatasi maalum za kuandikia barua za mapenzi halafu nawauzia jamaa, kisha kama nitaandika Mimi hio barua inabidi uongeze dau! Ndio maisha yangu yalivyokuwa, huwezi kwenda kununua kadi bila kupata ushauri wangu.....next time nitawaeleza kisa nilichokifanya kwa mshkaji aliekua anataka nikamnunulie Card amtumie Demu wake pale Mazinde Juu.
Barua zilisaidia sana kuweza kuandika essay zenye maana na kanuni za uandishi zilizingatiwa......Umenikumbusha mbali saaaaana
Sikubaliani na wewe kwa jinsi ulivyoanisha kwamba kwa text huwezi kubuni/jaza hisia kama ilivyo kwa barua.Binafsi hua naandika text/email ndefu mpaka nashangaa na sio copy n paste mind you.We sema siku hizi watu ubunifu haupo kiwango...hata ingekua lwa barua bado tu wangeandika mistari kadhaa au mingi isiyotoka moyoni(yakuambiwa).Kwahiyo tatizo hapa sio njia ya mawasiliano bali ni watu wanavyowasiliana!!!
hapa naona mnasema tu, ebu mmoja atuandikie barua anayoikumbuka, iwe ameituma au ametumiwa ili angalau tukumbukie, mm kama nimesahau! ebu tumwagieni jamani
Dah! lizzy umeniacha hoooi! nkupe box yangu uniandikie barua kama hii, umeniacha nataabika kwa utamu wa barua. mama cjui ulimwandikia nani! yaani kama ungeniandikia mm ningetangaza ndoa mama. ebu jaribu kuniandikia tuone itakuwaje. nimeipenda na umetumia akili za ukweli mama.
Hehehheheeh....pesa ya stamp na bahasha ntapata wapi?!box 116 chato kagera