Unawaamini waganga wa kienyeji au huwaamini na kwanini? Tupe uzoefu wako

thewajibu

JF-Expert Member
Jan 14, 2017
226
292
Miongo kadhaa iliyopita nilizaliwa huko wilayani chato, tarafa ya nyamirembe katika mojawapo ya kaya kubwa kabisa kijijini kwetu ambapo mgeni aliwaza mara mbili mbili kabla ya kuingia kwenye kaya hiyo kutokana na ukubwa wake na wingi wa watu waliokuwepo.

Ni mengi niliyashughudia yakifanyika na mengine kuyashiriki yaliyohusu waganga wa kienyeji yakilenga ulinzi wa familia, mali na mambo mengine.

Nilichokigundua waganga wanachofanya nikukuunganisha kwenye mnyororo wa thamani na kukuonesha mazingaombwe yenye ukaribu na ukweli ili uwaamini na waendelee kupiga pesa.

Pamoja ulinzi na dawa za wanganga wakutosha lakini familia hiyo kubwa ilisambalatika kabisa huwezi jua kama kulikuwa na kaya mahali pale mpaka mzaliwa wa pale kama mimi
Sitasahau 2002 Mama angu mkubwa alipougua ukimwi miaka hiyo tunaiita (silimu) waganga wengi walikuja na kudai kalogwa na kuondoka na ng'ombe baadae ikagundulika ni mwathilika lakini tayari familia imepata hasara.

Mama mzazi 2008 huenda angepona lakini waganga wa kienyeji walihusika pakubwa katika kifo chake huenda angepelekwa kwenye hospital kubwa angepona kifua pekee kilimsababishia kifo Mungu awaangalie ipasavyo.

Mwisho naandika kwa masikitiko sana ninavyoandika hapa Mama mkubwa mwingine pamoja na dada zangu watatu wameingia kwenye mtego wa maostadhi nimejaribu kuwambia sana lakini hawaelewi mwishoe mimi ndo nikataka kuwa adui wao nimeamua kuachana nao lakini kusema ukweli wanamaliza mali za mama mkubwa.


Sitawaamini waganga hata kama wataumba mbingu mpya na kama ntalazimika nitakufa lakini sitaki waganga wa kienyeji.
 
Shida kuna waganga wa kweli na matapeli waganga wa kweli huwa wanasema utakuja kunishukuru ukifanikiwa kweli ukitusua lazima uludi we mwenyewe unakua unajishtukia mfano wa waganga wa kweli ni mwandulame wa buza kanisani dar nasikia kiboko huyu kuna siku mtamfungia safari toka huku mwanza akanisafishe nyota kidogo
 
Waganga wa kienyeji asilimia kubwa ni matepeli tu, we jaribu kwenda hata Kama huumwi chochote, waambie unaumwa! utaambiwa Mara umelogwa na blaa blaa nyingi, naamini katika dawa za miti shamba lakini sio kupigiwa lamli za waganga
 
Shida kuna waganga wa kweli na matapeli waganga wa kweli huwa wanasema utakuja kunishukuru ukifanikiwa kweli ukitusua lazima uludi we mwenyewe unakua unajishtukia mfano wa waganga wa kweli ni mwandulame wa buza kanisani dar nasikia kiboko huyu kuna siku mtamfungia safari toka huku mwanza akanisafishe nyota kidogo

Mkuu samahani unaweza kujazia nyama kidogo, huyu Mwandulame ye ni nani!? Yuko Buza eneo gani!? Na huduma zake zikoje!?

Na vipi huko pande za Mwanza! ?
 
Shida kuna waganga wa kweli na matapeli waganga wa kweli huwa wanasema utakuja kunishukuru ukifanikiwa kweli ukitusua lazima uludi we mwenyewe unakua unajishtukia mfano wa waganga wa kweli ni mwandulame wa buza kanisani dar nasikia kiboko huyu kuna siku mtamfungia safari toka huku mwanza akanisafishe nyota kidogo
Mkuu kusema ukweli hakuna mganga wa kweli atakachofanya ni kukuonyesha mazingaombwe yaliyo kalibu na ukweli lakini hautaona mafanikio.
Mfano miaka ile alikuja mganga wa ngo'mbe nyumbani akafanya mambo yake na akaacha dawa tukawa tunakoka cha ajabu dawa ilionekana kufanya kazi maana duni la ng' ombe lilionekana kupanda kwa speed ya ajabu kila mtu aliamini dawa iko vizuri lakini hakuna mabadiliko ya uhakika
 
Waganga wa kienyeji asilimia kubwa ni matepeli tu, we jaribu kwenda hata Kama huumwi chochote, waambie unaumwa! utaambiwa Mara umelogwa na blaa blaa nyingi, naamini katika dawa za miti shamba lakini sio kupigiwa lamli za waganga
Mimi navyojua wote waongo ukiwafuatilia kwa makini ni wana fursa tu
 
Kwanza, pole kwa kupoteza ndugu wakiwa katika tiba asilia. Pili, niambie hospitali ambayo wagonjwa wake wote uwa wanapona wakilazwa kutibiwa. Tatu, kama wote wanapona kwanini mochwari zinajengwa mahospitalini, zisijengwe kwenye vituo vya polisi? Ndugu yangu hata waganga wa tunguli na waganga wa kikemikali wanakufa. Kifo kikija hakizuiliki. Yote yanayofanyika chini ya jua, ni ubatili mtupu, mbele ya kifo. Ondoa simanzi moyoni furahia pumzi yako uivutayo. Kumbuka, sote tumetoka katika umauti tunarudi huko huko, kifo kikituitaji twende bila kusita,mzunguko wa maisha uendelee kama kawaida, kufa kuzaliwa upya. Pole kwa simanzi uliyoipitia. Tabasamu tena.
 
Kwanza, pole kwa kupoteza ndugu wakiwa katika tiba asilia. Pili, niambie hospitali ambayo wagonjwa wake wote uwa wanapona wakilazwa kutibiwa. Tatu, kama wote wanapona kwanini mochwari zinajengwa mahospitalini, zisijengwe kwenye vituo vya polisi? Ndugu yangu hata waganga wa tunguli na waganga wa kikemikali wanakufa. Kifo kikija hakizuiliki. Yote yanayofanyika chini ya jua, ni ubatili mtupu, mbele ya kifo. Ondoa simanzi moyoni furahia pumzi yako uivutayo. Kumbuka, sote tumetoka katika umauti tunarudi huko huko, kifo kikituitaji twende bila kusita,mzunguko wa maisha uendelee kama kawaida, kufa kuzaliwa upya. Pole kwa simanzi uliyoipitia. Tabasamu tena.
Sijawahi kusikia mganga akikwambia nimeshindwa kazi au silioni tatizo tofauti na hospitali wanakueleza ukweli kama tatizo hawalioni au hawawezi kutibu tatizo lako, Kufa siyo tatizo kabisa mkuu lakini unaona ni halali mgonjwa wa ukimwi kumwambia kalogwa?
 
Sijawahi kusikia mganga akikwambia nimeshindwa kazi au silioni tatizo tofauti na hospitali wanakueleza ukweli kama tatizo hawalioni au hawawezi kutibu tatizo lako, Kufa siyo tatizo kabisa mkuu lakini unaona ni halali mgonjwa wa ukimwi kumwambia kalogwa?
Mgonjwa wa UKIMWI kuambiwa kalogwa kwa nyakati zile za( silimu) ilikuwa sahihi, kuliko nyakati hizi za (kusendeka). Kwa kuwa hapakuwapo hauweni ya aina yoyote kama ilivyo sasa. Linganisha unyanyapaa wa kipindi kile mahospitalini kwa wagonjwa wa UKIMWI. Naweza kusema wale waliyo kufa kwa ugonjwa huo, wakiamini wamelogwa, walikufa kwa amani zaidi kuliko wale waliofia mahospitalini kwa ugonjwa huo huo wakiwa wamevimba mishipa kwa kudungwa sindano, huku wakitambua hawatopona! Tafadhali, fikiria mchawi wa wakizungu aliyepandikiza uchawi(HIV) huo katika mwili wa wanadamu. RAMLI UWA HAIDANGANYI. Tafsiri ndiyo uwa inapotosha tu na walio wengi. USISAHAU NDOTO YA KIMWELI!
 
Mgonjwa wa UKIMWI kuambiwa kalogwa kwa nyakati zile za( silimu) ilikuwa sahihi, kuliko nyakati hizi za (kusendeka). Kwa kuwa hapakuwapo hauweni ya aina yoyote kama ilivyo sasa. Linganisha unyanyapaa wa kipindi kile mahospitalini kwa wagonjwa wa UKIMWI. Naweza kusema wale waliyo kufa kwa ugonjwa huo, wakiamini wamelogwa, walikufa kwa amani zaidi kuliko wale waliofia mahospitalini kwa ugonjwa huo huo wakiwa wamevimba mishipa kwa kudungwa sindano, huku wakitambua hawatopona! Tafadhali, fikiria mchawi wa wakizungu yaliyepandikiza uchawi(HIV) huo katika mwili wa wanadamu. RAMLI UWA HAIDANGANYI. Tafsiri ndiyo uwa inapotosha tu na walio wengi. USISAHAU NDOTO YA KIMWELI!
Hayo ni machache tu niliyoyaona kuhusu waganga kwa sababu nimekulia humo na nimeyaona mengi huhusu waganga nishaweka hitimisho mkuu.
 
Mimi katika pita pita zangu Siwez kuwadharau Waganga wa tiba za Asili wala kuwadhihaki kwa kuwa nimeshuhudia Mambo ya Ajabu sana ktk maisha yangu na ya Marafiki zangu ambao walifanikiwa Matatizo yao. Hawa jamaa wanasaidia sana jamii ktk kutatua shida zao mfano. Mtu ukifungua biashara haitokii, Kuuguliwa tuu Mfululizo, Umesoma na Cheti Unacho ila Ajira Hupati licha ya kufanya Usaili miaka kibao kila kukicha, Mwanamke kuvuja bleed zaid ya wiki nzima na ukienda hospitalin unachomwa sindano bado Dam haikati, Ukilima mazao yanakubali vizuri ila Mavuno yanakuwa Madogo.
Ila kwa hivisasa taaluma yao imeingiliwa na Matapel hivyo yatupasa tuwe makini sana pindi Mtu anapohitaji huduma.
Note: Kuna uzi nilipost unahusu Ushuhuda Kigoma.
Plz Msini Ban
 
Shida kuna waganga wa kweli na matapeli waganga wa kweli huwa wanasema utakuja kunishukuru ukifanikiwa kweli ukitusua lazima uludi we mwenyewe unakua unajishtukia mfano wa waganga wa kweli ni mwandulame wa buza kanisani dar nasikia kiboko huyu kuna siku mtamfungia safari toka huku mwanza akanisafishe nyota kidogo
acha imani hiyo mwamini mungu nasiku zote ukimukna mganga ambae mnamwita wa kweli ujue amemuhasi mungu yupo upande wa shetani na maeshafanya mahasi mengi mganga wa kweli ni nungu tu mtegemee mungu
 
acha imani hiyo mwamini mungu nasiku zote ukimukna mganga ambae mnamwita wa kweli ujue amemuhasi mungu yupo upande wa shetani na maeshafanya mahasi mengi mganga wa kweli ni nungu tu mtegemee mungu
Lini umeacha uzinzi mkuu nayo ni zambi
 
Mimi katika pita pita zangu Siwez kuwadharau Waganga wa tiba za Asili wala kuwadhihaki kwa kuwa nimeshuhudia Mambo ya Ajabu sana ktk maisha yangu na ya Marafiki zangu ambao walifanikiwa Matatizo yao. Hawa jamaa wanasaidia sana jamii ktk kutatua shida zao mfano. Mtu ukifungua biashara haitokii, Kuuguliwa tuu Mfululizo, Umesoma na Cheti Unacho ila Ajira Hupati licha ya kufanya Usaili miaka kibao kila kukicha, Mwanamke kuvuja bleed zaid ya wiki nzima na ukienda hospitalin unachomwa sindano bado Dam haikati, Ukilima mazao yanakubali vizuri ila Mavuno yanakuwa Madogo.
Ila kwa hivisasa taaluma yao imeingiliwa na Matapel hivyo yatupasa tuwe makini sana pindi Mtu anapohitaji huduma.
Note: Kuna uzi nilipost unahusu Ushuhuda Kigoma.
Plz Msini Ban
Ukweli wapo wanaotenda na kufanikisha na humo humo matapeli wamejaa..
 
Back
Top Bottom