mudy92
JF-Expert Member
- Feb 19, 2014
- 671
- 535
Mizimu ni roho za wazee wetu (wa ukoo) toka katika pande zote mbili Baba na Mama ambao ni babu na bibi toka kwa baba na babu na bibi toka kwa Mama,roho hizi huja na kuwa na sisi pale tunapozihitaji au zinapotuhitaji....!
kwanini Mizimu huja kwetu au kwaini tunaiita?
-UDUGU, kumbuka roho hizi ni zile za waze wetu (ancestors) ambao walizaa baba na mama zetu hivyoo kuja au kuwaita hutokana na Udugu
-ULINZI, roho zote zisizo na mwili huona yasiyoonekana kama Uchawi na magonjwa hivyoo Wazee wetu huja na tunawaita watuambie haya tusiyoyaona.
-MILA, utamaduni na desturi zetu hututaka tufanye mambo yaliyo katika mpangilio ulio sahihi kama kuwapa wazee heshima na kusikiliza yale wanayotuambia.
Njia ya Kuwaita Wazee wako (MIZIMU) ili waje kwako na wakuambie utakalo Uliza...
Hatua ya 1.
-Pika POMBE ya ulezi au Pombe yeyote ya Kienyeji itokanayo na nafaka ( Uliza kufahamu babu na bibi yako walikuwa wanakunywa Pombe ipi enzi za uhai wako au wanakunywa ipi kama wako hai.)
Hatua ya 2.
-Tafuta KUKU mweupe kabisa asiye na Doa wakienyeji chinja na Muache afe kwa Kurukaruka mpaka atakapo kata Roho, kisha Mpike kama Mboga
Hatua ya 3.
-pika CHAKULA asili cha wazee wako kama Ugali, Ndizi na Mihogo au pika vyoote kwa Pamoja (usichanganye) katika kiasi kidogo kila chakula ila wali pika Mwingi.
Hatua ya 4.
-karibisha watu kwako waje kula Haswa Watoto na Wazee pia wape Wazee wanywe pombe uliyopika kwako na wakirimu kwa kila kitu, Kama wazee wako walikuwa wafugaji Nunua maziwa ya Pakti na Uwape watoto na wazee wanywee.
KUMBUKA:
1-kuwanawisha watu wote wanaokuja kula kabla na Baada ya Kula.
2-ukikosa Pombe kanunue vilabuni
3-usipikie Vyombo vilivyopikiwa Kitimoto
UTAPATAJE MAJIBU KUWA WAZEE (MIZIMU) WAMEFURAHI NA WAPO TAYARI KUKUSKILIZA?
- wakati wa Kulala Omba Mungu kisha Ita wazee wako woote wa Ukoo kwa baba na Mama kisha waambie shida yako kisha Wao watakuja Ndotoni na Jibu lako....
Jibu linaweza kuwa La mafumbo au Dhahiri Kazi kwako!
kwanini Mizimu huja kwetu au kwaini tunaiita?
-UDUGU, kumbuka roho hizi ni zile za waze wetu (ancestors) ambao walizaa baba na mama zetu hivyoo kuja au kuwaita hutokana na Udugu
-ULINZI, roho zote zisizo na mwili huona yasiyoonekana kama Uchawi na magonjwa hivyoo Wazee wetu huja na tunawaita watuambie haya tusiyoyaona.
-MILA, utamaduni na desturi zetu hututaka tufanye mambo yaliyo katika mpangilio ulio sahihi kama kuwapa wazee heshima na kusikiliza yale wanayotuambia.
Njia ya Kuwaita Wazee wako (MIZIMU) ili waje kwako na wakuambie utakalo Uliza...
Hatua ya 1.
-Pika POMBE ya ulezi au Pombe yeyote ya Kienyeji itokanayo na nafaka ( Uliza kufahamu babu na bibi yako walikuwa wanakunywa Pombe ipi enzi za uhai wako au wanakunywa ipi kama wako hai.)
Hatua ya 2.
-Tafuta KUKU mweupe kabisa asiye na Doa wakienyeji chinja na Muache afe kwa Kurukaruka mpaka atakapo kata Roho, kisha Mpike kama Mboga
Hatua ya 3.
-pika CHAKULA asili cha wazee wako kama Ugali, Ndizi na Mihogo au pika vyoote kwa Pamoja (usichanganye) katika kiasi kidogo kila chakula ila wali pika Mwingi.
Hatua ya 4.
-karibisha watu kwako waje kula Haswa Watoto na Wazee pia wape Wazee wanywe pombe uliyopika kwako na wakirimu kwa kila kitu, Kama wazee wako walikuwa wafugaji Nunua maziwa ya Pakti na Uwape watoto na wazee wanywee.
KUMBUKA:
1-kuwanawisha watu wote wanaokuja kula kabla na Baada ya Kula.
2-ukikosa Pombe kanunue vilabuni
3-usipikie Vyombo vilivyopikiwa Kitimoto
UTAPATAJE MAJIBU KUWA WAZEE (MIZIMU) WAMEFURAHI NA WAPO TAYARI KUKUSKILIZA?
- wakati wa Kulala Omba Mungu kisha Ita wazee wako woote wa Ukoo kwa baba na Mama kisha waambie shida yako kisha Wao watakuja Ndotoni na Jibu lako....
Jibu linaweza kuwa La mafumbo au Dhahiri Kazi kwako!

