Unapotaka ufanikiwe kwenye biashara inahitajika

ItsMi

Member
Sep 13, 2021
66
31
Ufanye vifuatavyo ambavyo ni baadhi ya njia, au mbinu na vitu vya kuzingatia unapotaka ufanye biashara.

1. Kwanza unahitajika kufanya tafiti katika upande wa masoko kwa bidhaa yako husika.

2. Mtaji wa biashara unayoenda kuanzisha kwa sababu kama tunavyojua huwezi kufanya biashara itakayokuletea mafanikio pasipo mtaji.

3. Pia ni lazime utafute nyaraka kwa ajili ya ulipaji kodi ikiwa ni pamoja na hatimiliki ya biashara, ambapo vyote hivyo vinapatikana katika mamlaka za mapato ya nchi yaani (TRA).

4. Unatakiwa kuzingatia pia ni mahali gani au eneo gani biashara hiyo utaiweka na kwa kuzingatia uhitaji wa bidhaa husika.

5. Miundombinu bora kwa usafirishaji wa bidhaa zako zinapokuwa zinatoka na kuingia mahali unapofanyia biashara

6. Pia ni lazima uwe na bidhaa au huduma itakayokuwa bora ili kuchochea Ushindani kwa biashara yako na watu wengine kwa sababu ushindani unasaidia kutofautisha kilicho bora na kisicho bora hii itasaidia kumvuta mteja anunue dukani kwako.

7. Ni lazima bidhaa zako ziwe na Ubora kwa sababu mteja hupenda bidhaa bora na uaminifu ili siku nyingine aweze kuja dukani kwako na kukuungisha tena.

8. Inakubidi kuwa na lugha nzuri kwa Wateja muda wote bila kuchagua wala kubagua.

9. Inatakiwa ujue hasara na Faida ya biashara unayofanya ili uweze kujua jinsi gani ya kujinusuru na kufirisika.

Asante.
 
Hayo yote uliyosema ni muhimu Ila tatizo wakubwa hawataki kuelewa wapunguze kodi ya vitu bro. Ushawahi sikia kitu Hiki 'There is everything in the shop but the people don't have the money to purchase'. Hii kwa biashara yangu ya electronic accessories naiona Mali zipo Ila wateja hawataki bei. Naomba niishie hapa.
 
Hayo yote uliyosema ni muhimu Ila tatizo wakubwa hawataki kuelewa wapunguze kodi ya vitu bro. Ushawahi sikia kitu Hiki 'There is everything in the shop but the people don't have the money to purchase'. Hii kwa biashara yangu ya electronic accessories naiona Mali zipo Ila wateja hawataki bei. Naomba niishie hapa.
Dah pole sana mkuu, ila kama ulivyosema watu wengi wanafungua maduka na hatimaye baada ya muda huyafunga maduka hayo kutokana na sababu mbalimbali ikichangiwa na mambo ambayo ni pamoja na :

1.ongezeko la kodi /ushuru kwa bidhaa au huduma

2.kufirisika kwa mfanyabiashara hali inayoweza kutokana na kutokujua mbinu na mikakati ili aweze kuendeleza biashara hiyo......

Hivyo yote hayo yanapaswa kuzingatiwa kwa kuiomba serikali ipunguze kodi zenye kumuumiza mteja. Halafu pia sisi wafanyabiashara tunapaswa kuboresha huduma zetu na kujua ni vitu gani wateja wetu wanavihitaji kwa kuzingatia mazingira ili kuchochea uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom