Unanyoa ama unasuka mtindo gani wa nywele

ukitaka hii style ikae poa zaidi mtu awe na kichwa cha box kama huyo jamaa na nywele zenye afya....kuna mwanangu flani nikimyoa inamkaa kinoma tena namwambiaga aje ule muda nnaokaribia kufunga ili awe mteja wa mwisho,kwangu mimi hii ndo stle nnayoipenda kuliko zote na ndo ninayonyoa kichwani kwangu na nina vinyozi wawili wanaoninyoa vizuri nikiwakosa hao basi ni bora nijinyoe mwenyewe au nighailishe maana kujinyoa napo kunanigharimu lisaa lizima na sikuhizi nimekuwa mvivu kinoma.
Mimi nina kichwa kama yai....! Sijui ni style gani itanifaa
 
Mimi nina kichwa kama yai....! Sijui ni style gani itanifaa
😂😂😂 mkuu umenichekesha sana ila watu hawajui tu kupendeza kwenye kunyolewa napo kunasababishwa na vitu vingi achilia mbali kichwa na nywele...rangi ya mtu mpk muonekano wa sura yake .
 
Yapo majukwaa mahsusi ya masuala haya. Usinchanganye mambo, hapa tuongelee ulimbwende na mitindo.
Najua kwamba kuna hayo majukwaa lakini kwanini tusiongeee mambo ya msingi kila mahali ili watu wahamasike zaidi kubadili mtazamo wa nchi badala ya kutaka kujua nanyoa upara au kiduku alafu nini sasa

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom