Unanunua hisa, umewahi kusoma popote kuhusu hisa?

Makirita Amani

JF-Expert Member
Jun 6, 2012
1,915
3,420
Kuna watu wamenishangaza sana, wanakimbilia kuchukua mikopo benki ili wakanunue hisa. Najiuliza haya mawazo watu huwa wanayatoa wapi?

Wanayo tabia ya kujielimisha binafsi kabla ya kuchukua hatua?

Wanayo tabia ya kuomba ushauri kwa wenye uelewa kabla ya kufanya kitu?

Iko hivi rafiki, unapotaka kufanya kitu chochote ambacho hujawahi kufanya kwenye maisha yako, unahitaji ujielimishe na ukielewe kwanza kitu hicho kabla ya kuchukua hatua.

Na njia za kujielimisha zipo mbili kwa kuanzia;

1. Soma vitabu vitano bora kwenye kitu hicho.

2. Kaa chini na mtu mwenye uelewa wa jambo hilo na akushauri vizuri.

Sasa kama huna muda wa kujielimisha kabla ya kuchukua hatua, usilie pale unapofanya maamuzi ya hovyo.

Na hii ni kwa kila jambo, siyo hisa tu, iwe ni kufuga kuku, bata au hata nyuki. Iwe ni kuanza biashara au hata kuanza familia.

Jenga tabia ya kujielimisha kabla ya kufanya maamuzi.

Kocha Makirita,

www.amkamtanzania.com

www.kisimachamaarifa.co.tz
 
Kocha, nimekuja mbio nikidhani umetuwekea darasa kuhusu hisa kumbe ni maneno yale yale tu ya siku zote. Weka darasa hapa tufaidike. Tupo bize na kasi ya magufuri kiasi kwamba hata huo mda wa kusoma vitabu vitano hatuna
 
Heshima Mkuu!

Ulichokiandika ni Soundfull ila hatutokuelewa ulichokimaanisha.Tatizo lipo kwetu kwa kupenda kuendeleza falsafa zisizokuwa na mantiki.Hatupendi kusoma, Kudadisi, Kusaili masuala ya msingi nk.Tunachokitaka sisi ni Shortcut.Na mwisho wa shortcut huwa tunafahamu.

Tunajenga nyumba nzuri sna ila hazina Maktaba.Je tutaondokana na Utumwa wa kifikra?.Mbona kina Prof Mansa Musa wa Timbuktu,JKN,Mandela na wengineo waliotutangulia walianza vizuri?.Tatizo letu ni nini?.

Tupende kusoma vitabu.Books help us grow and we wont ever grow without reading.

Asalaam.
 
Kocha, nimekuja mbio nikidhani umetuwekea darasa kuhusu hisa kumbe ni maneno yale yale tu ya siku zote. Weka darasa hapa tufaidike. Tupo bize na kasi ya magufuri kiasi kwamba hata huo mda wa kusoma vitabu vitano hatuna
Heshima Mkuu!

Naomba nikushauri kitu.Katika maisha yako amua ukisema MIMI na siyo SISI.Unaposema tupo bize unamaanisha nini?.Mpo bize na nani?.

Pia unaposema huo muda wa kusoma vitabu vitano huna una maanisha nini?.Vitabu vitano ni vingi?.Huo muda huna na nani?.

Naomba nimalizie kwa kukushauri tena kuwa,Tatizo si muda.Tatizo ni nia.Ukiwa na nia ni lazima njia itapatikana tu.

Kumradhi kwa hili.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Kocha, nimekuja mbio nikidhani umetuwekea darasa kuhusu hisa kumbe ni maneno yale yale tu ya siku zote. Weka darasa hapa tufaidike. Tupo bize na kasi ya magufuri kiasi kwamba hata huo mda wa kusoma vitabu vitano hatuna
Darasa la hisa nimeshatoa sana mkuu,
Labda tu utakuwa hufuatilii kwa makini.
Pamoja na yote, ni muhimu sana ujielimishe, ni muhimu usome vitabu.
Angalia darasa la hisa hapa;
 
Sasa utapata wapi uzoefu bila ya kuthubutu kujaribu? Changamoto nayo ni elimu
Sijaandika hapa usithubutu, nimesema ujielimishe kabla ya kufanya maamuzi.
Utaepuka kufanya makosa ya wazi,
Lakini usikimbilie kuchukua hatua bila ya uelewa wowote ukijiaminisha utajifunza kwa kukosea.
 
Heshima Mkuu!

Ulichokiandika ni Soundfull ila hatutokuelewa ulichokimaanisha.Tatizo lipo kwetu kwa kupenda kuendeleza falsafa zisizokuwa na mantiki.Hatupendi kusoma, Kudadisi, Kusaili masuala ya msingi nk.Tunachokitaka sisi ni Shortcut.Na mwisho wa shortcut huwa tunafahamu.

Tunajenga nyumba nzuri sna ila hazina Maktaba.Je tutaondokana na Utumwa wa kifikra?.Mbona kina Prof Mansa Musa wa Timbuktu,JKN,Mandela na wengineo waliotutangulia walianza vizuri?.Tatizo letu ni nini?.

Tupende kusoma vitabu.Books help us grow and we wont ever grow without reading.

Asalaam.

Bro acha kulaumu watanzania, vitabu vyenyewe ni vichache, ni kazi kubwa kuvipata vitabu kwa walio nje ya DSM, booksshop zetu zimejaa vitabu vya shule za msingi na secondary..
Mimi binafsi napenda sana kusoma, nilishajiwekea kila mwezi nimalize kitabu, na kweli nimevisoma sana vitabu. Nakiri kusoma kwingi ni kuongeza maarifa. Changamoto ni kuvipata vitabu, hasa namaanisha Hard copies, kusoma online kunaumiza sana macho.
 
Back
Top Bottom