sinafungu
JF-Expert Member
- Feb 13, 2010
- 1,524
- 863
Yalikuwa maneno ya kipenzi changu kuanzia 1990 hadi 2004, vitoto vinakua , tukaona tutafute mbadala wa kipato badala ya kutegemea kamshahara kangu tu.tukaanzisha biashara, na msimamizi akawa ni yeye, mwenzangu huko akapata walimu wakampa somo likamkolea. nyumbani kukawa hakuna amani, hisani na maisha ya watoto hakuvijali akili yake ikawa kuvunja nyumba na kukimbilia utajiri ....., wazee wakatusuluhisha lkn sikio la kufa halisikii dawa. nyumba ikavunjika . tangu wakati huo hadi leo ni ndg zake tu ndo wanaokuja kuangalia watoto ,yeye ni aibu kwenda mbele. amejaribu namna turudiane uwezekano huo umekosekana kwani mimi tayari nimeoa , maisha yamempiga kisawasawa namuonea huruma lkn mchuma janga hula na wa kwao. nimejifunza jambo ktk maisha ya ndoa , usitupe penzi alilokupa MUNGU kwa kutaraji kupata kwa akili yako utachemka.