Unafiki wa baadhi yetu baada ya majangili kumuua kapteni wa chopa mzungu

PhD

JF-Expert Member
Jul 15, 2009
4,599
3,673
Ndugu zangu,

Hivi juzi kumetokea tukio baya la kuhuzunisha baada ya majangili wa tembo kumuua rubani wa kiingereza katika pori la akiba huko Simiyu mpakani mwa hifadhi ya Serengeti.

Ni wazi tukio hilo ni baya kwani limepoteza maisha ya binadamu mwenzetu lakini pia majangili hao walikuwa wamekwisha ua tembo mmoja katika eneo la tukio. Tunamuombea marehemu pumziko jema na ahueni kwa familia yake.

Ukiachana na tukio hilo, kilicho nikera ni unafiki wa baadhi ya watanzania kwenye mitandao ya kijamii (Twitter na FB) kujidai wanaumizwa sana na tukio hilo moja na kujisaulisha kuwa watanzania wenzetu askari wa wanyamapori wanauwa kila siku na majangili kwenye mapori na hifadhi za Taifa.

Sijawahi kuwasikia wakipost habari hizo za uzuni na kuguswa kwa wingi kama walivyofanya kwa kapteni wa chopa. Au kwa kuwa ndugu zetu hawa wanauwawa wakiwa kwenye malandlover na sio chopa? huu ni unafiki mkubwa.

Pili hao wanafiki wa mitandaoni wanatulazamisha kuamini kuwa kusimamishwa kwa operesheni tokomeza na bunge ndio kumesababisha majangili kuongezeka na sasa wanailamu bunge. Huu ni unafki mwingine mkubwa, nani asiyejua jinsi operesheni hiyo ilivyofanyika kwa unyama kwa mama zetu na picha za ushahidi zikiwawazi.

Nashauri tuepuke double standard kwenye masuala ya msingi, kiherehere cha kudai umeguswa na kifo cha kapteni mzungu kuliko askari wetu wa wanyama pori wanaokufa Selous, Katavi na Serengeti kila siku katika mazingira magumu kikome.

Inajulikana wazi mitandao ya majangili inahusisha watu wakubwa wenye nyadhifa kwenye chama na serikali, nguvu ielekezwe huko na tuthamini sana mchango wa watazanzania askari wazawa wanaovuja jasho kulinda rasilimali zetu.
 
Siyo hudhuni ni huzuni. Na pia siyo uzuni ni huzuni. Rudi shule ndugu. Au kabla hujapost nitafute niku haririe habari yako ili watu wasikudharau. Pia hukuwa na ulazima sana wa kuanzisha thread.
 
Hayamkini habari zao hazitangazwi,
Lakini iko tofauti kubwa kati ya mauaji ya kawaida ya asikari wa wanyama pori.
Na mauaji yaliyoandamana na kutunguliwa kwa helikopita
Hili sio tukio la kawaida.
 
Labda alivyouwawa Mzungu ,serikali itakuja na mikakati halisi ya kupambana na ujangili.
 
Siyo hudhuni ni huzuni. Na pia siyo uzuni ni huzuni. Rudi shule ndugu. Au kabla hujapost nitafute niku haririe habari yako ili watu wasikudharau. Pia hukuwa na ulazima sana wa kuanzisha thread.
GREAT THINKER!
 
Labda alivyouwawa Mzungu ,serikali itakuja na mikakati halisi ya kupambana na ujangili.
Tatizo la serikali kushindwa kukabiliana na ujangili ni moja tuu, kukosa ushirikiano wa askari wa wanyama pori kutoka kwa wananchi.
Madhila wanayopata wananchi wanaoishi pembezoni mwa hifadhi yanajenga uadui mkubwa kati ya askari na wananchi na mbaya tuu ni kuwa hayafiki kwenye vyombo vya habari.
Watu wanateswa hata kuuwawa kwa makosa madogo sana. Mfano wanawake kuingia hatua chache tuu kuokota kuni wakishikwa ni kudhalilishwa na hata kubakwa na walinzi hao. Hapo kweli utategemea msaada wa taarifa kutoka kwao?
Bila ushirikiano na wenyeji hatutafanikiwa lengo la kupambana na ujangili
 
Siyo hudhuni ni huzuni. Na pia siyo uzuni ni huzuni. Rudi shule ndugu. Au kabla hujapost nitafute niku haririe habari yako ili watu wasikudharau. Pia hukuwa na ulazima sana wa kuanzisha thread.
Na wewe kwanini unachanganya kiingereza na kiswahili? Ni lugha ipi hasa kati ya hizi mbili inayokushinda?
 
Siyo hudhuni ni huzuni. Na pia siyo uzuni ni huzuni. Rudi shule ndugu. Au kabla hujapost nitafute niku haririe habari yako ili watu wasikudharau. Pia hukuwa na ulazima sana wa kuanzisha thread.
Kaka mtoa hoja ana pointi za msingi sana, pima mambo kabla hujamkosoa mtu, kwa sababu wewe na familia yako mnalala na kuamka salama unafikiri na wengine wako salama kama wewe. Jitahidi uwe na chembe ya huzuni kwa watu, achana na utoto wa kukosoa maandishi wakati ujumbe ni muhimu kuliko makosa ya herufi. Be sensitive don't be silly.
 
Kaka mtoa hoja ana pointi za msingi sana, pima mambo kabla hujamkosoa mtu, kwa sababu wewe na familia yako mnalala na kuamka salama unafikiri na wengine wako salama kama wewe. Jitahidi uwe na chembe ya huzuni kwa watu, achana na utoto wa kukosoa maandishi wakati ujumbe ni muhimu kuliko makosa ya herufi. Be sensitive don't be silly.
Msamehe bure. Ndo matatizo ya walimu wa UPE.
 
KIVUKO KIMEZAMA KILOMBERO HUKO WATU WAPO KIMYAAAA,MPAKA WATU WALIOKUFA IDADI KAMILI HAIJULIKANI LAKINI KIMYAAAA LAKINI NAKUMBUKA SIKU MAGAIDI WALILIPUA FRANCE WEEEE KILA MTU KWENYE PAGE YA FACEBOOK KAWEKA BENDERA YA FRANCE,hii ni hatari sana
Ndugu zangu,

Hivi juzi kumetokea tukio baya la kuhuzunisha baada ya majangili wa tembo kumuua rubani wa kiingereza katika pori la akiba huko Simiyu mpakani mwa hifadhi ya Serengeti.

Ni wazi tukio hilo ni baya kwani limepoteza maisha ya binadamu mwenzetu lakini pia majangili hao walikuwa wamekwisha ua tembo mmoja katika eneo la tukio. Tunamuombea marehemu pumziko jema na ahueni kwa familia yake.

Ukiachana na tukio hilo, kilicho nikera ni unafiki wa baadhi ya watanzania kwenye mitandao ya kijamii (Twitter na FB) kujidai wanaumizwa sana na tukio hilo moja na kujisaulisha kuwa watanzania wenzetu askari wa wanyamapori wanauwa kila siku na majangili kwenye mapori na hifadhi za Taifa.

Sijawahi kuwasikia wakipost habari hizo za uzuni na kuguswa kwa wingi kama walivyofanya kwa kapteni wa chopa. Au kwa kuwa ndugu zetu hawa wanauwawa wakiwa kwenye malandlover na sio chopa? huu ni unafiki mkubwa.

Pili hao wanafiki wa mitandaoni wanatulazamisha kuamini kuwa kusimamishwa kwa operesheni tokomeza na bunge ndio kumesababisha majangili kuongezeka na sasa wanailamu bunge. Huu ni unafki mwingine mkubwa, nani asiyejua jinsi operesheni hiyo ilivyofanyika kwa unyama kwa mama zetu na picha za ushahidi zikiwawazi.

Nashauri tuepuke double standard kwenye masuala ya msingi, kiherehere cha kudai umeguswa na kifo cha kapteni mzungu kuliko askari wetu wa wanyama pori wanaokufa Selous, Katavi na Serengeti kila siku katika mazingira magumu kikome.

Inajulikana wazi mitandao ya majangili inahusisha watu wakubwa wenye nyadhifa kwenye chama na serikali, nguvu ielekezwe huko na tuthamini sana mchango wa watazanzania askari wazawa wanaovuja jasho kulinda rasilimali zetu.
 
Ndugu zangu,

Hivi juzi kumetokea tukio baya la kuhuzunisha baada ya majangili wa tembo kumuua rubani wa kiingereza katika pori la akiba huko Simiyu mpakani mwa hifadhi ya Serengeti.

Ni wazi tukio hilo ni baya kwani limepoteza maisha ya binadamu mwenzetu lakini pia majangili hao walikuwa wamekwisha ua tembo mmoja katika eneo la tukio. Tunamuombea marehemu pumziko jema na ahueni kwa familia yake.

Ukiachana na tukio hilo, kilicho nikera ni unafiki wa baadhi ya watanzania kwenye mitandao ya kijamii (Twitter na FB) kujidai wanaumizwa sana na tukio hilo moja na kujisaulisha kuwa watanzania wenzetu askari wa wanyamapori wanauwa kila siku na majangili kwenye mapori na hifadhi za Taifa.

Sijawahi kuwasikia wakipost habari hizo za uzuni na kuguswa kwa wingi kama walivyofanya kwa kapteni wa chopa. Au kwa kuwa ndugu zetu hawa wanauwawa wakiwa kwenye malandlover na sio chopa? huu ni unafiki mkubwa.

Pili hao wanafiki wa mitandaoni wanatulazamisha kuamini kuwa kusimamishwa kwa operesheni tokomeza na bunge ndio kumesababisha majangili kuongezeka na sasa wanailamu bunge. Huu ni unafki mwingine mkubwa, nani asiyejua jinsi operesheni hiyo ilivyofanyika kwa unyama kwa mama zetu na picha za ushahidi zikiwawazi.

Nashauri tuepuke double standard kwenye masuala ya msingi, kiherehere cha kudai umeguswa na kifo cha kapteni mzungu kuliko askari wetu wa wanyama pori wanaokufa Selous, Katavi na Serengeti kila siku katika mazingira magumu kikome.

Inajulikana wazi mitandao ya majangili inahusisha watu wakubwa wenye nyadhifa kwenye chama na serikali, nguvu ielekezwe huko na tuthamini sana mchango wa watazanzania askari wazawa wanaovuja jasho kulinda rasilimali zetu.
Mtumwa humcha bwana wake na ukizingatia ni mwingereza ndo balaaa.
Watanzania hatuthaminiani lakini twataka kuthaminiwa
 
Huyu rubani ni mzungu amekufa akipambana na ujangili unaofanywa na watanzania wenzetu dhidi ya maliasili yetu. Kwa mtanzania kufa akilinda vyetu, ni wajibu wake. Kwa mgeni kufa akilinda vyako ni zaidi ya wajibu.

Sisi waafrika tuko kwenye mkanganyiko. Hatutaki wazungu watuingilie kwenye upuuzi tunaofanya ati tu kwasababu na sisi ni sovereign countries. Lakini tukichinjana kama Rwanda tunaanza kulaumu wazungu kwa kutoingilia kati. Ni mkanganyiko. Watanzania wanafanya uharamia, wazungu ndo wanaogharamia miradi yote ya kupambana na ujangili na kutunza wanyama walio hatarini kutoweka. Kwa mtanzania, sitashangaa kama mlinzi wa wanyama pori ndiye jangili au anashilikiana na majangili. Huo ndio ukweli mchungu.
 
Back
Top Bottom