Uminywaji wa Demokrasia na mauaji ya wamanchi: Viongozi wote wa dini Tanzania mko wapi? Raia tunaangamia!

Molembe

JF-Expert Member
Dec 25, 2012
9,821
11,527
Alianza na watumishi wa umma akawatengua bila makosa, watu wengi walishangilia kitendo hicho na kumsifia, bila kujali kuwa Watanzania wenzetu wengi walikuwa wakionewa bila kosa aidha kwa chuki binafsi.

Akaja kwa vyama vya siasa, akazuia shughuli zao ambazo zipo kwenye katiba ikiwemo mikutano ya hadhara, wananchi wakakaa kimya, vyombo vya habari vikakaa kimya wala hakukemewa hata viongozi wa dini kuhusu mwenendo wake huo wa siasa.

Amezuia ajira serikalini, vijana wamebaki wakilia vilio vya samaki hawajui kushoto yao lakini jamii umewaacha wakilia bila msaada si viongozi wa dini wala wananchi wanahoji kuhusu hilo ni kwa vile haliwagusi moja moja.

Ameteka bunge, bajeti anapanga yeye, sheria anatunga yeye wabunge wetu wamebaki kimya wanatumika hawajitambui na wala hawahoji mamlaka hiyo alipoitoa kwa vile hawajaguswa.

Kipindi anatumbua wananchi huko vijijini walimshangilia bila kujua kwamba wengi walitumbuliwa sababu ya visasi na chuki leo hii wanalia njaa kaziba pamba masikioni na kasema hatoi chakula cha msaada ng'o, wameguswa.

Magazeti nayo yameguswa, watumishi wa umma wameguswa, wahitimu vyuo vikuu wameguswa, wananchi wenye njaa wameguswa, wafanyabiashara wameguswa.

Wamebaki viongozi wa dini, mmeyafumbia macho haya yote hammkemei mtu huyu kwa kujiona mpo salama ipo siku mtaguswa.
 
Kulianza na sintofahamu kule Zanzibar wakati wa uchaguzi lakini viongozi wa madhehebu yetu wakawa kimya.

Kwa sasa bunge la Jamhuri ya Muungano liko katika hali ya mpasuko mkubwa lakini viongozi wa dini wako kimya!

Kuna kauli tata kwa sasa zinazotofautiana kutoka serikalini lakini hawa viongozi wetu wako kimya.

Hivi wanaelewa kuwa siku ya kiama wataulizwa mambo kama haya? Hivi hawa viongozi wetu wa dini wanaelewa kuwa kama kuna raia wanaishi kwa kulalamika katika jamii ibada zao hazina tija mbele ya MwenyeziMungu? Nini kimewakuta viongozi wetu hawa?

Mbona kilipokaribia kipindi cha kampeni walikuwa wanashindana kuwashawishi watu kwenda kugombea urais? Kwani hawa raia wanaolalamika hawana dini?
 
Mkuu viongozi wa dini hapa kwetu ni wanafiki wakubwa. Wao wanachojua ni kukusanya sadaka na zaka kutoka kwa masikini. Mstakabali mtajijua wenyewe.

Hata siku moja usitegemee kiongozi wa dini anasimama kukemea maovu. Hizi organized religions ni agents wa serikali kama ulikuwa hujui.
 
Mkuu viongozi wa dini hapa kwetu niwanafiki wakubwa. Wao wanachojua ni kukusanya sadaka na zaka kutoka kwa masikini. Mstakabali mtajijua wenyewe. Hata siku moja usitegemee kiongozi wa dini anasimama kukemea maovu. Hizi organized religions ni agents wa serikali kama ulikuwa hujui.

Mimi nilisha achana nao. Inabidi wawe sauti ya wanyonge, to the contrary wanakuwa sauti ya wababe
 
Viongozi wa dini wakitoa ushauri au kukosoa basi wanaingia kwenye matatizo mfano askofu kakobe, mchungaji gwajima na shehe ponda
 
Mimi nilisha achana nao. Inabidi wawe sauti ya wanyonge, to the contrary wanakuwa sauti ya wababe
Walituaminisha uongo mtu.. Stories za dini ni Conspiracy theories tu. Wajanja walikuja na gear hiyo ili kujipatia utajiri. They made and still making a lot of wealth from the poor.
 
Viongozi wa dini wa Tanzania hawa akina Augustino Ramadhan na akina Musa ?

Chukulia kwamba nchi hii ni taifa la kipagani lisilo na hofu yoyote ya Mungu , ndio maana paroko bila aibu anawalisha sakramenti watu waovu wanaokandamiza haki za raia .

Nitamke wazi kwamba mimi kwa sasa nimebaki na Mungu na Mitume wake tu lakini hawa wanafiki wa madhehebu sitaki kabisa kushirikiana nao .
 
Walituaminisha uongo mtu.. Stories za dini ni Conspiracy theories tu. Wajanja walikuja na gear hiyo ili kujipatia utajiri. They made and still making a lot of wealth from the poor.
Kwenye dini kuna majipu pia. Wengine wanangoja kuomba badaa ya kukemea na wengine wanasifia hata kama wanajua kuna tatizo.
Hivi ukiona mtu anpigwa utaomba au utazuia?
 
Mkuu wako busy kukusanya sadaka za wajinga na ahadi kedekede kwamba ukitoa hela zako kwake mafanikio ni dakika moja.Hayo mambo mengine hawana muda nao,wao wako busy wanavuna tu mkuu
 
Kwenye dini kuna majipu pia. Wengine wanangoja kuomba badaa ya kukemea na wengine wanasifia hata kama wanajua kuna tatizo.
Hivi ukiona mtu anpigwa utaomba au utazuia?

Viongozi wa dini inabidi wawe sauti ya wanyonge, lkn eti wanaomba watu wanakufa eti unaomba.
 
Kinachoendelea bungeni ni janga la kujitakia. Watu hawajafukuzwa wanatoka wenyewe kwa mapenzi yao. Wangekuwa kwa kutoka kwao wanalipwa posho wananchi wangelelamika na viongozi wa dini pia. Wao wakae nje mpaka 2020 hakuna hasara.

Nyie mnao mchango mkubwa wa kurudisha hao watu bungeni kwani mnayo namba ya Mbowe mwambieni mmeuvaa mkenge abadili mbinu ya kurudi bungeni hata ya yeye kujipeleka kwa askofu yoyote adai ameitwa na akitoka huko abadili msimamo kwa ushauri wa askofu. Vingenevyo tuonaneni mkutano wa nne mkiwa njen au mkubali yaishe.
 
walionekana hawana hekima, hawakusoma na wachochezi waliposema serikali ya ccm ina udini (ukristo).

Awamu ya 1; vyovyote ilivyokuwa hawakuwa na neno

Awamu ya 2; kupitia julias walimzogoa sana ali, ali kwa hasira akavunja azimio lao na kuleta la zanz.

Awamu ya 3; ben pamoja na ubabe, uuzwaji wa mashirika kifisadi, epa. hawakuwa na matamko wala nyaraka.

Awamu ya 4; mrisho walimtamkia mengi mabaya na nyaraka nyingi sana kutoka kurasini hasa pale alipomfanya edo kuwa pm wake, imetumika mbinu kubwa na hila ili samwel asiweze kuingia ikulu, kwani heri za msuni kuliko mprotestant, baada kuona mkakati wa edo ni thabiti na kukosa msaada wa ikulu kuzuia mpango wa edo waliamua kumuandaa wilbroad upande wa pili na kumsakama sana mrisho na edo, waliogundua mfumo kristo huo waliungana na edo na kutoka ccm.

Inawezekana kabisa sakata la vilaza wa udom lina mlengo wa mfumo huo.
 
Kwanini lawama zisielekezwe kwa mihimili mitatu kwa mujibu wa katiba yetu:Serikali,Mahakama na Bunge?

Wanalaumiwa kama nani? Mhimili wa nne au wa tano?

Kwa maoni yangu, nadhani hizi lawama kwa viongozi wa dini haziwastahili. Wao hawako katika sehemu yoyote kati ya

vyombo vya kufanya maamuzi.
 
Wao wameguswa si ulisikia pale bukoba walivoambiwa wavumilie sana sadaka itakuwa hakuna na isitoshe subiri sheria kamili kuua misamaha ya kodi ndio watazinduka
 
Alianza na watumishi wa umma akawatengua bila makosa, watu wengi walishangilia kitendo hicho na kumsifia, bila kujali kuwa Watanzania wenzetu wengi walikuwa wakionewa bila kosa aidha kwa chuki binafsi.
Akaja kwa vyama vya siasa, akazuia shughuli zao ambazo zipo kwenye katiba ikiwemo mikutano ya hadhara, wananchi wakakaa kimya, vyombo vya habari vikakaa kimya wala hakukemewa hata viongozi wa dini kuhusu mwenendo wake huo wa siasa.
Amezuia ajira serikalini, vijana wamebaki wakilia vilio vya samaki hawajui kushoto yao lakini jamii umewaacha wakilia bila msaada si viongozi wa dini wala wananchi wanahoji kuhusu hilo ni kwa vile haliwagusi moja moja.

Ameteka bunge, bajeti anapanga yeye, sheria anatunga yeye wabunge wetu wamebaki kimya wanatumika hawajitambui na wala hawahoji mamlaka hiyo alipoitoa kwa vile hawajaguswa.

Kipindi anatumbua wananchi huko vijijini walimshangilia bila kujua kwamba wengi walitumbuliwa sababu ya visasi na chuki leo hii wanalia njaa kaziba pamba masikioni na kasema hatoi chakula cha msaada ng'o, wameguswa.

Magazeti nayo yameguswa, watumishi wa umma wameguswa, wahitimu vyuo vikuu wameguswa, wananchi wenye njaa wameguswa, wafanyabiashara wameguswa.

Wamebaki viongozi wa dini, mmeyafumbia macho haya yote hammkemei mtu huyu kwa kujiona mpo salama ipo siku mtaguswa.
Nchi hii mheshimiwa imejaa unafiki.
Kuna watu pamoja na maovu ya Rais wanamsifu bado.
Kuna wasomi na wanamsifu wakati iko wazi kuwa amepotoka na hapaswi kusifiwa kabisa.
 
Naandika hapa nikiwa kwenye hali ya wasiwasi mkubwa sana maana hali si nzuri hakika.
Mengi yamefanywa na watawala awamu hii hapa sitoyaorodhesha maana yanafahamika vizuri tu lakini mengi ya hayo yameumiza sana raia sababu yanaminya haki za msingi za raia.
Wapo walojaribu kuzungumza kwa kushauri watawala lakini waliishia kulala ndani ya kuta za mahabusu huko, wengine kutishiwa kuuawa nk, wanaamua heri wabaki kimya kwa uoga wa kuuawa.

Mauaji yanayoendelea huko pwani Kibiti, Mkuranga na Rufiji yatatumaliza maana takwimu zinaonesha hadi sasa raia wasio na hatia zaidi ya 30 wameshauawa kwa kupigwa risasi na kile kinachoitwa 'watu wasiojulikana' wakiwemo askari polisi 13 na nilimskia ndugu rais John Magufuli akiwa ziarani huko pwani akiwaomba hao watu wauaji 'wasiojulikana waokoke', na hatujui kwa hakika inaezekana kwao kuokoka si lazima na sio kipaumbele chao sasa si tutakwisha!

Tegemeo la raia limebaki kwa viongozi wa dini hawa ni Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania [Tanzania Episcopal Conference - TEC], Mashehe na maaskofu wa madhehebu tofauti Tanzania na wachungaji wote kupaza sauti zao katika kuwataka watawala wachukue hatua kudhibiti na kuzuia mauaji haya kuendelea tu kutokea hali ndugu na jamaa zetu wapenda wanaendelea kupoteza maisha huko Pwani.
Lakini chakuskitiza zaidi hawa viongozi wa dini wako kimya tu hata tamko na waraka hakuna kutoka kwao hivi hadi afe nani ndiyo mtatoka na kutoa waraka na matamko?

Mchungaji mwema anawachunga na kuwalinda kondoo wake na kuhakikisha wanabaki salama siku zote.
Mauaji haya yanayoendelea hao kondoo wanaezaje kuskia na kuuata mafundisho yenu ya dini hali wanasakwa na kuwindwa ili wauawe kwa kumiminiwa risasi na walengaji shabaa bila huruma na hakuna mtetezi?

Tunamkumbuka mchungaji Rev. Martin Luther King Jr. kwa kupigania amani duniani na upendo wa watu wote pasi na ubaguzi hadi alitunukiwa tuzo ya amani ya Nobel [Nobel piece prize] na kwa hakika dunia haitoeza kumsahau kwa mchango wake na alivyojitoa kwa watu nawaomba muige mfano wake.
Mwingine ni askofu Desmund Tutu wa Afrika ya kusini na huyu pia aliwahi kushinda tuzo ya Nobel na aliwahi kusema nanukuu '
If you are neutral in situations of injustice, you have chosen the side of the oppressor' tafsiri kama unakuwa kimya tu na hauna upande kwenye uminywaji wa haki basi wewe umeamua kuchagua upande wa yule mvunja haki.

Ni nani wa kuwatetea ndugu Watanzania hawa wanaoteseka na kuuawa kila uchao? ni nani huyo na yuko wapi?

Mungu ibariki Tanzania na wote waliouawa kwa kupigwa risasi nao wametutangulia mbele ya haki.

Mwanaharakati mie herikipaji.
 
Back
Top Bottom