Umeme na maji imekuwa kero

Umeme na maji imekuwa kero

KILIVITE

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2013
Posts
1,302
Reaction score
556
Tatizo la umeme na maji Tanzania limekuwa kero kubwa sana.Serikali ya CCM imekuwa ikitoa ahadi nyingi zisizotekelezeka kutatua ukosefu wa umeme na maji.

Magufuli ana ahidi kujenga viwanda vingi kila Wilaya sasa najiuliza viwanda hivyo vitatumia nishati gani?.Viwanda vingi vinahitaji maji pia.Kila maeneo mjini na Vijijini hakuna maji na hakuna umeme.

Nina amini hakuna maendeleo yatakayopatikana kama hakutakuwa na umeme na maji.Naomba bila kinyongo kila mchangiaji aseme ukubwa wa tatizo la maji na umeme eneo alipo.

Naanza mimi mwenyewe,hapa nilipo Kata ya Mlowa,Makambako Njombe,Kukatika kwa umeme mara kwa mara kumeathiri maendeleo kwa kiasi kikubwa.

Upatikanaji wa maji ni mgumu.Tunalazimika kuamka saa kumi alfajiri kufuata maji kilometa 8.Umeme na maji imeshakuwa kero ambayo CCM imeshindwa kutatua.

Mimi nimeamua kuipiga chini CCM Oktoba 25,2015.Nitampa kura yangu LOWASSA.Wewe je?
 
Wagosi waliimba wimbo miaka 10 hadi sasa ukipigwa uko relevant hali haijabadilika kabisa "umeme na maji Tanzania ishakua kero..watu keroooo... Keroooo"
 
Tatizo la umeme lineathiri sana shughuli zangu kwa mwezi wa pili sasa.
CCM wasinilaumu Octoba 25.
 
Pamoja na haya kuna watanzania wanaishabikia ccm.
 
Nipo Mwenge upo afu Achen kuchanganya Mambo ya kitaalam na Siasa
Wewe acha kujifanya kimbelembele umeme sehemu kubwa umekatwa!umeme wanakata sehemu zingine kunakuwepo na umeme...ukweli ni huu tanesco hawana hela ya kuendesha mitambo shirika lina hali mbaya kifedha...
 
Kusema mahali nilipo Kuwa Upo nimekuwa kimbelembele kwan we culiuliza kwaiyo ulitegemea kuwa kote haupo?
 
Kusema mahali nilipo Kuwa Upo nimekuwa kimbelembele kwan we culiuliza kwaiyo ulitegemea kuwa kote haupo?
Naona bado unafurahia hali ya mgao wa umeme tanzania....wenzetu duniani wanapiga hatua mbele sisi tunarudi nyuma....
Unajua sahv ni watu wangapi hawaingizi hela kwa kutofanya kazi kwa kukosekana umeme.
Yote kwa sababu ya serikali hii ya kimaku ya ccm
 
Back
Top Bottom