Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Tunajenga kesho yetu kwa tunachokipanda leo.
Tokea uhuru hivi ni chama gani kilikua kinaongoza?mkuu...umasikini wa Tanzania kwa kiasi kikubwa umesababishwa na wanasiasa mikataba mibovu, mipango mibovu ya maendeleo, wizi, ufisadi wote umefanywa na wanasiasa , wabunge wanalipwa hela ya bure tu wakat hakuna msaada wowote wanaotoa kwa Taifa...mi natamani hata siasa ipigwe marufuku kabisa tuangalie mambo mengine ya maana bora nchi iwe ya kidikteta kama north korea kuliko kuhangaika na siasa zenye kujali maslahi ya wachache..
Wewe unalipwa na nani ku comment? Na kusomaHivi wewe unalipwa kiasi gani kupost humu JF thread kila baada ya dakika 5?
watanzania hatuhitaji wanasiasa tena tunahitaji maendeleo lowasa ametumia pesa nyingi sana za ufisadi kuutafuta urais hizo pesa angezitumia kwenye mambo ya maendeleo taifa lingekuwa mbali sanaTokea uhuru hivi ni chama gani kilikua kinaongoza?
Soma thread yoteEti Gaddafi aliwakandamiza raia wake ndivyo ulivyokaririshwa???
Ushaidi ni upi ametumia pesa mingi ndio mlivyo ambiwa hapo lumumba?watanzania hatuhitaji wanasiasa tena tunahitaji maendeleo lowasa ametumia pesa nyingi sana za ufisadi kuutafuta urais hizo pesa angezitumia kwenye mambo ya maendeleo taifa lingekuwa mbali sana
lowasa amempa mbowe bilioni 10 ili apewe ridhaa ya kugombea urais mbowe kwa tamaa yake ya pesa akamfukuza dr.slaa na kumchomeka lowasa kampeni zote za Ukawa kwenye uchaguzi mkuu ziligharamiwa na lowasaUshaidi ni upi ametumia pesa mingi ndio mlivyo ambiwa hapo lumumba?
Ndio ukweli alikuwa mkandamizaji, kupendelea watu wa kabila lake. Sehemu kubwa ya utajiri wa Libya kufadhili ugaidi (Carlos, Mohamed Boudia, Red Army, etc) madikteta wa Africa(Idd Amin Dada, Jean Bedel Bokassa, Hissen Habre). Ingawaje kwa kiwango kidogo alisaidia ukombozi wa Africa. Soma vyanzo mbalimbali.Eti Gaddafi aliwakandamiza raia wake ndivyo ulivyokaririshwa???
Walibya hawakuwa wakifanya uchaguzi ambao ungewawezesha wananchi kubadili uongozi wautakao. Hapa kwetu tumetoka kufanya uchaguzi miezi saba iliyopita na mgombea wa chama cha mapinduzi Jon Magufuli alishinda. Waliompa kura walitaka aongoze kwa mtindo huu.Katika mfumo huru na rafiki wa maisha kuheshimu, kuruhusu, kukubali na kusikiliza maoni ya mtu ni nguzo ya ueledi, ustahimilivu, uungwana na ukomavu.
Hakuna mahali palipostaarabika duniani ambapo watu wamefungiwa milango na madirisha ya kutoa maoni na mawazo yao halafu jamii ikapiga hatua. Libya ilikuwa nchi tajiri kupindukia. Raia walipewa kila walichohitaji kwasababu serikali ilidhibiti kila kitu na ilikuwa na fedha za kufanya chochote lakini kilichomtokea Ghadafi ni matokeo ya raia kuchoshwa na ukandamizwaji wa hali ya juu. Hata kama ubeberu wa wamarekani ndio uliomng'oa Ghadafi, ukweli ni kwamba raia waliokuwa wamekandamizwa kwa miaka lukuki walipata ahueni na wengi wao waliunga mkono ubeberu ule japo kwa maslahi tofauti.
Katika siasa za Tanzania leo tunashangilia kuingia katika enzi ya tofauti ambapo wala nchi wanaadhibiwa na angalau ishara za kurejesha nidhamu ya uwajibikaji zinaonekana. Hali hii inatoa matumaini japo yanafifishwa na kinachoendelea nyuma ya pazia na ambacho kadri siku zinavyokwenda kinajidhihirisha peupe.
Ni hali ya kuzuia kwa nguvu zote watu na taasisi kuchambua, kujadili na kutoa mawazo mbadala dhidi ya utendaji wa serikali ya awamu ya tano. Katika mazingira tuliyonayo haiingii akilini kwamba serikali makini kama ya Dr. Magufuli itaogopa mijadala, kukosolewa na kushauriwa. Kuzuiwa kwa matangazo ya moja kwa moja ya vipindi vya mijadala bungeni na kupigwa marufuku mikutano ya vyama vya upinzani nchini ni kielelezo cha serikali kudhihirisha udhaifu wake katika kupokea na kuhimili mawazo mbadala.
Kuhusu bunge sihitaji kulisema tena kwasababu limesemwa sana. Najiuliza i wapi nia njema ya kuviacha vyama vya siasa viendelee na wajibu wao wa kisiasa? Vyama hivi vimesajiliwa kufanya kazi za kisiasa.
Unapovizuia vyama kukutana na wanachama wake mikutanoni unatuma ujumbe kwa taifa kwamba hakuhitajiki mawazo mbadala. Hii ni kansa ya kuliua taifa. Watawala jifunzeni kwenye historia. Tunajenga kesho yetu kwa tunachokipanda leo.
Vielelezo pleaselowasa amempa mbowe bilioni 10 ili apewe ridhaa ya kugombea urais mbowe kwa tamaa yake ya pesa akamfukuza dr.slaa na kumchomeka lowasa kampeni zote za Ukawa kwenye uchaguzi mkuu ziligharamiwa na lowasa
Kwa ushaidi upi au ndio kama uli wakumuita Lowassa fisadi bila ushaidi kumbe kisa ni Uwaziri mkuulowasa amempa mbowe bilioni 10 ili apewe ridhaa ya kugombea urais mbowe kwa tamaa yake ya pesa akamfukuza dr.slaa na kumchomeka lowasa kampeni zote za Ukawa kwenye uchaguzi mkuu ziligharamiwa na lowasa
Sheria yakuanzisha chama cha siasa nipamoja na mikutano ya HadharaWalibya hawakuwa wakifanya uchaguzi ambao ungewawezesha wananchi kubadili uongozi wautakao. Hapa kwetu tumetoka kufanya uchaguzi miezi saba iliyopita na mgombea wa chama cha mapinduzi Jon Magufuli alishinda. Waliompa kura walitaka aongoze kwa mtindo huu.
Upumbavu wenu wananchi waliukataa. Andaeni ajenda za kuwaambia wananchi mwaka 2020 kwa kukusanya takwimu za makosa na kufanya mikutano ya ndani. Siasa za kipumbavu na kufanya kampeni zisizoisha hazivumiliki. Wabunge wafanye mikutano na wananchi ajenda kuu ni kuwahimiza wananchi kujiletea maendeleo yao kulingana na mipango iliyopo ya serikali iliyoshinda. Mikutano yenye lengo la kuwafanya wananchi waichukie serikali yao na kushindwa kutekeleza mipango ya maendeleo ni kinyume cha uendeshaji mzuri wa demokrasia.
Hebu nenda sasa hivi Libya kayaseme hayo maneno yako kama ukukatwa kichwa.Ndio ukweli alikuwa mkandamizaji, kupendelea watu wa kabila lake. Sehemu kubwa ya utajiri wa Libya kufadhili ugaidi (Carlos, Mohamed Boudia, Red Army, etc) madikteta wa Africa(Idd Amin Dada, Jean Bedel Bokassa, Hissen Habre). Ingawaje kwa kiwango kidogo alisaidia ukombozi wa Africa. Soma vyanzo mbalimbali.
nitafurahi sana kama mwenye mawazo hayo uko peke yako maana ukiona mtu anapendelea udikteta ujuwe yeye ni hatari kuliko ukimwi.Leo nimeelewa kwanini watu wengine wakifa wengine wana shangilia badala ya kulia.mkuu...umasikini wa Tanzania kwa kiasi kikubwa umesababishwa na wanasiasa mikataba mibovu, mipango mibovu ya maendeleo, wizi, ufisadi wote umefanywa na wanasiasa , wabunge wanalipwa hela ya bure tu wakat hakuna msaada wowote wanaotoa kwa Taifa...mi natamani hata siasa ipigwe marufuku kabisa tuangalie mambo mengine ya maana bora nchi iwe ya kidikteta kama north korea kuliko kuhangaika na siasa zenye kujali maslahi ya wachache..