Ultrasound ni nini?

Ultrasound ni nini?

Ndio, si lazima ajibu mleta uzi yoyote mwenye ufahamu anaweza kunisaidia.
Oky asante sana ..
Jibu ni ndio.

Mimba iliyo nje ya mfuko ni ngumu kuonekana kwa sababu mara nyingi huwa ni ndogo sana.. hi hufanya iwe ngumu sana kuonekana kwa kipimo lakini pia kwa kuwa sehemu iliyopo sio sahihi hvo kutafuta ni changamoto...

Swali lingine mkuu
 
Oky asante sana ..
Jibu ni ndio.

Mimba iliyo nje ya mfuko ni ngumu kuonekana kwa sababu mara nyingi huwa ni ndogo sana.. hi hufanya iwe ngumu sana kuonekana kwa kipimo lakini pia kwa kuwa sehemu iliyopo sio sahihi hvo kutafuta ni changamoto...

Swali lingine mkuu
Sawa, shukrani sana.

Swali lingine, hiyo ectopic pregnancy hakuna namna nyingine ya kuiondoa hadi upasuaji?
 
HAbari mtaalam ikikupendeza tupatie na elimu ya MRI.
Wacha nikujibu mm.
MRI( magnetic resonance imaging) hutumia nguvu ya usumaku kutengeza picha.

1. Mwili wa mwanadamu una organ( ubongo, ini, Figo n.k) ndani ya organi kuna tissue na ndani ya tissue kuna cells na ndani ya cells kuna maji n.k

Kama umesoma physics vizuri kuna hii kitu..
Palipo na umeme kuna usumaku pia..
( jiulize kwa nn mtu anapigwa shots ya umeme? Maana ake na yy ana umeme ndani yake.)

Sasa kwenye maji yaliyo ndani ya cell kuna hydrogen proton ambazo zinazunguka (spin) na hivyo zinakua na usumaku ndani yake..
Na kila organ au sehemu ya mwili ina idadi tofauti ya cell hivyo itakua na kiwango tofauti cha maji na vile vile kiwango tofauti cha hydrogen.
Hizi hydrogen proton huwa zina rotate kwenye position fulani naturally tu...

Sasa
1. Mwilini kuna usumaku
2. Machine ina sumaku

Nn kinafanya picha itokee?

Machine ya MRI hutuma taarifa za usumaku kuja kwenye mwili wa mwanadamu. Usumaku huu hupelekea ule usumaku wa mwili kulalia upande fulani(flip)

Halafu baadae kila sehemu ya mwili kutokana na kiwango chake cha hydrogen itakua inarudi kwenye position yake ya ku spin ya mwanzo kabla haijapata ile sumaku kutoka kwa machine..
Wakati zinarudi kuna kifaa kinaitwa coil hiki ndo huwa kinatuma taarifa na huwa kinapokea taarifa kutoka kwa hydrogen proton zinazorudi kwenye position zao za mwanzo...

Sasa Machine ina uwezo wa kubadili taarifa za usumaku zinazorudi kutoka kwenye mwili na kuwa picha...

Kukiwa na shida labda uvimbe kwenye organ fulani labda ini. idadi ya cell huongozeka, maji yanaongezeka..

Sasa sehemu hii ha uvimbe itakua na sifa tofauti ya cell za ini zilizo nzima..
Hivyo pich itakayokuja sehemu ya uvimbe itaonekana tofauti...


Mwisho kabsa..
MRI ni nzuri kwenye vipimo vinavyohusisha sehemu laini ya nyama( soft tissue)
Kama vile uvimbe, kuangalia ubongo, ini , uti wa mgongo, sehemu za joints..

Huku x ray na CT scan ni nzuri kwenye mifupa

Kuna vitu vingi saana nimejibu japo kwa uchache
Asanteni.
 
Tofauti ya ultrasound na x ray ni nn
X ray( ionising radiation)
Ni mionzi inayoweza kuvunja DNA ya cell..
Kipimo cha X ray ni kizuri kuona mifupa

Ultrasound ( Non-ionizing radiation)
Ni mionzi isiyoweza kuvunja DNA ya cell
Ni mawimbi ya sauti yenye nguvu ya juu ambayo masikio ya mwanadamu hayawezi kusikia..

Kipimo cha ultrasound ni kizuri kuona vitu vya nyama nyama
Kama vile ini, figo, moyo, mishipa y damu, mtoto tumboni n.k


MADHARA
1. X ray inaweza kupelelea kansa ikiwa mtu anakuwa amepokea kiwango kikubwa cha mionzi...
Ultrasound haiwezi kusababisha kansa na kwa kiasi kikubwa mno haina madhara
 
X ray( ionising radiation)
Ni mionzi inayoweza kuvunja DNA ya cell..
Kipimo cha X ray ni kizuri kuona mifupa

Ultrasound ( Non-ionizing radiation)
Ni mionzi isiyoweza kuvunja DNA ya cell
Ni mawimbi ya sauti yenye nguvu ya juu ambayo masikio ya mwanadamu hayawezi kusikia..

Kipimo cha ultrasound ni kizuri kuona vitu vya nyama nyama
Kama vile ini, figo, moyo, mishipa y damu, mtoto tumboni n.k


MADHARA
1. X ray inaweza kupelelea kansa ikiwa mtu anakuwa amepokea kiwango kikubwa cha mionzi...
Ultrasound haiwezi kusababisha kansa na kwa kiasi kikubwa mno haina madhara
Xray haioni nyama nyama..?
 
Vipimo vya hospitali huwa havifanyiki mara zote huwa vinafanyika tu pale ambapo Daktari ameona kuna Umuhimu wa kufanya hivyo, Ila ultrasound haina madhara yeyote kwa mama mjamzito au kwa mwili wa binadamu
 
Back
Top Bottom