Wazo la kabwela
JF-Expert Member
- Feb 13, 2013
- 1,884
- 1,466
Ulitegemea kipenga na kadi alivyopoteza refa vitoke wapi?
Mpambano unaendelea. Katikati ya mchezo,refa
anagundua kuwa amepoteza kadi-ya njano na
nyekundu pamoja na filimbi. Kutokana na kasi ya
mchezo, anauchuna. Haisikiki filimbi wala
haionekani kadi hata pale inapohitajika.
Wachezaji wanakatana mitama ya kiama lakini
kimya. Wachezaji wanatukana na vikumbo kupigana
lakini kimya. Mpira unatoka na kurushwa tena bila
filimbi kupigwa.
Wachafu wanacheza rafu na wasafi wanachafuliwa.
Wachezaji wanatamba kila namba na kujigamba.
Refarii yuko kimya huku akionekana dhahiri shahiri
kuwa kasi ya mchezo inamshida.
Anajikaza kisabuni tu. Anaendelea kukimbia hapa na
pale akiomba tu mchezo uishe salama. Itasikika
filimbi gani goli likifungwa? Atasemaje kuwa ni goli
halali au haramu? Mpambano hauna mfano.
Refarii anafanya siri. Hasemi ukweli kama
amepoteza filimbi na kadi. Anakufa na tai yake
shingoni. Hata mchezaji kibaka naye kajichanganya
mpirani na anakaribia kutangazwa 'man of the
match'.
Mpambano unaendelea. Katikati ya mchezo,refa
anagundua kuwa amepoteza kadi-ya njano na
nyekundu pamoja na filimbi. Kutokana na kasi ya
mchezo, anauchuna. Haisikiki filimbi wala
haionekani kadi hata pale inapohitajika.
Wachezaji wanakatana mitama ya kiama lakini
kimya. Wachezaji wanatukana na vikumbo kupigana
lakini kimya. Mpira unatoka na kurushwa tena bila
filimbi kupigwa.
Wachafu wanacheza rafu na wasafi wanachafuliwa.
Wachezaji wanatamba kila namba na kujigamba.
Refarii yuko kimya huku akionekana dhahiri shahiri
kuwa kasi ya mchezo inamshida.
Anajikaza kisabuni tu. Anaendelea kukimbia hapa na
pale akiomba tu mchezo uishe salama. Itasikika
filimbi gani goli likifungwa? Atasemaje kuwa ni goli
halali au haramu? Mpambano hauna mfano.
Refarii anafanya siri. Hasemi ukweli kama
amepoteza filimbi na kadi. Anakufa na tai yake
shingoni. Hata mchezaji kibaka naye kajichanganya
mpirani na anakaribia kutangazwa 'man of the
match'.