Ulipenda/kuchukia nini kwa Baba/mama yako?

Ulipenda/kuchukia nini kwa Baba/mama yako?

Mpauko

R.I.P
Joined
Jan 19, 2019
Posts
2,323
Reaction score
3,460
Niaje?

Ni miaka mingi imepita tangu tukiwa wadogo hadi sasa.. Wapo wenzetu ambao wazazi walikwishatangulia.. Poleni sana wana..waleambao wazazi bado wapo hatuna budi kumshukuru muumba.

Wakuu hivi ni nini ulipenda au ulikichukia kwa baba/mama yako?

Binafsi nilipenda vile baba alijihimu asubuhi na kunichemshia chai kabla sijaenda shule huku mama kalala tu[emoji16]

Nilipenda ule ushujaa wa kushika mguu mmoja anakuning'iniza huku akikushushia bakora..[emoji16]

Kwa maza nilichukia makofi ya mgongo na kufinyana kwenye mapaja.. Yanauma balaa[emoji16]

Yote kwa yote nilipenda vile maza ananipakulia ugali mkubwa[emoji16]

Nikiharibu home mama anakausha hamwambii baba.. Atamwambia siku za mbelee huko mzee anakosa cha kuniadhibu[emoji16]

Nakumbuka vile napewahela ya shule (bweni) na wazazi halafu nkifika shule nakuta mama kaniwekea hela nyingine kwenye bahasha aliyoweka wakati ananipangia nguo[emoji16]

Maisha marefu wazazi wangu...

Kipi ulikipenda/ulichukia kutoka kwa mama/baba?
 
Mshua alisema "wanangu mtasoma hatakama itatulazimu kulala chini na kula majani" na kweli alisimamia kauli yake na kutekeleza katika kipindi kigumu zaidi.

R. I. P mshua, muumba alikupenda zaidi na kukuchukua hata kabla yakuona matunda ya wanao.
 
Mshua alisema "wanangu mtasoma hatakama itatulazimu kulala chini na kula majani" na kweli alisimamia kauli yake na kutekeleza katika kipindi kigumu zaidi.

R. I. P mshua, muumba alikupenda zaidi na kukuchukua hata kabla yakuona matunda ya wanao.
Pole sana mkuu
 
Sina cha kunifanya nimchukie mzazi wangu yeyote.

Alikuwa baba bora kwangu
 
Ila huyu baba sio aliekuzaa ni dady ako sasa... Usituambie bado upo kwa baba[emoji16]
Siagizi...ananiletea tu [emoji4][emoji4]
Nasubiri leo sijui ataniletea nini[emoji23][emoji23]
 
Nilichukia sana ambavyo wageni wakija walikuwa wanahamishiwa chumbani kwangu halafu Mimi nahamishiwa kwa hausigeli
Ila nipojiongeza, nilifurahi sanaaaaaaa, nikawa natoroka shule nikakae chumbani kwa hausigeli.
 
nampongeza dingi kunileta duniani.

kutojihusisha kwake kunilea itabak kuwa mambo ya kidunia.

Rip dingi.
 
Baba despite your weakness Bata Sana sijui wake wengi.Wanao umetupa kipaumbele kuliko kitu chochote kwenye maisha yako.
Best education umetupatia ya darasani na maishani......
Na mihela yote ile lakini shamba tulienda na kambi tukaeka.naeza ishi popote pale na yeyote yule.
Wazazi wangu ni elimu tosha,makungwi na washauri wakubwa sana through reference pasina wao kujua.
Nahakika ndoa yangu itakuja dumu milele,nmejifunza vingi toka kwao.
Baba na mama mmemlea mtoto si wenu mpk amekua successful anajitegemea na mji wake(baba alioa mke mdogo teyari akiwa na mtoto japo alitangulia mbele za haki lakn walitulea nae mpk kesho bila ubaguz wowote)Ni somo kubwa sana kwng.

NB.nikipata mume akawapenda watoto wake kuliko kitu chochote,ruksa kuoa hadi wanne.wanawake tu wengi sana kuliko wanaume,vyema kusitiriana.
Nimejikuta baba kaninspire,na nimejiandaa vizuri saikologikali ikitokea.

Asante Sana baba na mama
 
Dah hongera mkuu kwa malezi bora
Baba despite your weakness Bata Sana sijui wake wengi.Wanao umetupa kipaumbele kuliko kitu chochote kwenye maisha yako.
Best education umetupatia ya darasani na maishani......
Na mihela yote ile lakini shamba tulienda na kambi tukaeka.naeza ishi popote pale na yeyote yule.
Wazazi wangu ni elimu tosha,makungwi na washauri wakubwa sana through reference pasina wao kujua.
Nahakika ndoa yangu itakuja dumu milele,nmejifunza vingi toka kwao.
Baba na mama mmemlea mtoto si wenu mpk amekua successful anajitegemea na mji wake(baba alioa mke mdogo teyari akiwa na mtoto japo alitangulia mbele za haki lakn walitulea nae mpk kesho bila ubaguz wowote)Ni somo kubwa sana kwng.

NB.nikipata mume akawapenda watoto wake kuliko kitu chochote,ruksa kuoa hadi wanne.wanawake tu wengi sana kuliko wanaume,vyema kusitiriana.
Nimejikuta baba kaninspire,na nimejiandaa vizuri saikologikali ikitokea.
 
Back
Top Bottom