Ulimwengu wa mapenzi na walemavu

nyaggad

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
1,160
Reaction score
694
Habari wana Jamii forums

Kuna jambo nimekuwa nikifikiria sana ni kuhusu mahusiano ya kimapenzi kati ya walemavu na watu wa kawaida,niliwahi kuwa na mwalimu wangu mmoja alikuwa ni kilema,alipata shida sana alipotaka kuoa kila msichana aliyemfuata kumtongoza alimkataa.

Eti kwa kigezo kuwa yye ni kilema,sasa mmi ninaswali hivi kuna tatizo gani kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mlemavu,mbona wao ni binadamu kama wengine,wakina dada muache ubaguzi wa style hiyo,wanaume ssi tunajali sana mwanamke ata awe kichaa hawezi kukosa mwanaume.
 
Bado sijaona sababu ya kumbagua kilema katika suala lolote lile kwani mfumo wa maisha unaonyesha dhahiri kuwa kila mmoja wetu ni mlemavu mtarajiwa,kwani kila siku maisha yetu yamezungukwa na hatari za aina mbali mbali,tunatembea mabarabarani ,tunatumia vyombo vya usafiri vya aina mbalil mbali vyote hivyo vinatuweka karibu na ulemavu.

Mtu mwenye busara hawezi akamkataa mtu kutokana na maumbile yake bali kwa kutokuwa chaguo la moyo wake nimeshaona ndugu zangu wa karibu waliokuwa wamezaliwa wazima wa afya lakini leo hii wamepata ulemavu wa kudumu kutoka ajali ,wengine maradhi kiukweli hakuna ajuae kesho yake itakuwaje ni MUNGU tu pekee ndiye anayejua.
 
Wanaobagua hawafanyi vizuri.....
 
Kama ukilema wake ni inheritable kunauwezekano mkubwa wa kupata watoto vilema lkn kama not inheritable hakuna tatizo haina haja ya kumbaguwa
 
Wanaume walio wengi ndo wanaobagua kuliko wanawake. Wanaume walemavu wengi wameoa kuliko wanawake walemavu walioolewa. Chunguza utaona.
 
Kwa mwanaume kuoa mpaka uwe na Mali kama Sio elimu nina ushuhuda wa vilema wengi wa kidume waliooa
 
Kwani kalemaa VIA vya uzazi?? Kama tendo la ndoa linaweza kufanyika bila shida na umependa taabu nini kutomuoa?? Jamani HAKI SAWA KWA WOTE ni muhimu......
 
Ukimpenda mtu hayo ya ulemavu hutoyaona kamwe.
 
Kama ni mlemavu wa akili inakuwa changamoto na hata sheria inaruhusu kutoa talaka kwa mwenzako incase amekuwa kichaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…