KWA NINI WANANCHI WA KUSINI WANAPINGA GESI ISITOKE
1. Mkataba mzima wa mradi huu, mpaka sasa si viongozi wa kusini tu inavyoonekana hata mawaziri husika hawajui na kama wanajua basi wasibitishe hilo , ndiyo maana hata cha kuwaeleza wananchi mpaka sasa hawana.
Mkataba wenyewe kuanzia majadiliano mpaka mradi kukamilika unaonakana umefanywa ndani ya miezi 20 tu na unafanywa na viongozi ambao wamebakisha miaka 2 kumaliza muda wao, wanataka kila kitu kikamilike kabla wao hawajatoka madarakani hii inaonyesha wazi kunakitu ambacho wanalazimisha cha maslai yao binafsi na si Taifa.
2. Wananchi wa kusini walipata mateso makubwa, zaidi ya miaka 40 wameishi bila umeme,maji ya tabu, miaka 51 ya uhuru mpaka leo barabara haijakamilika ianakuwaje mradi huu mkubwa zaidi inabidi ukamilike ndani yamiezi 18 tu, Tanzania wote ni ndugu na ni wamoja, ilikuwa kusini ni mikoa ya adhabu kwa wafanyakazi wa serikali ambao walikuwa wanafanya makosa katika mikoa mingine ya Tanzania,mikoa 25 ya zamani ya Tanzania yote ilikuwa imeungwa kwenye gridi ya taifa na walikuwa wanapata umeme kwa masaa 24 kasoro mikoa ya kusini mpaka leo bado ilchosababisha viwanda vingi kufa na maisha kuwa magumu sana mpaka ikawa adhabu ya dunia ndiyo maana waliokuwa wanakosea makazini wanapelekwa huko kwa adhabu.
Gas ndiyo ikawa tumaini lao pekee, lakini leo gesi inahamishwa hata jiwe la msingi la kiwanda hata kimoja au mradi wowote bado ndiyo maana wanagoma.
3. Tanzania sisi bado hakuna ulazima wa kukopa zaidi ya tilioni 2 kupeleka gesi Dar, July 2004 gesi ilianza kuingia Dar 51.2 Mmscf/d toka Songosongo , August 2008 vilikamilika visima viwili vya gesi pale Songosongo na kuongezeka kwa gesi Dar mpaka kufikia 90 Mm scf/d lakini tangu 2004 mpaka leo gesi hiyo kwa viwandani na matumizi mengine inayotumika 10 Mmscf/d ya 90 Mmscf/d ya gas inayozalishwa na songosongo kwa hiyo ukiondoa la umeme Dar na Tanzania kwa ujumla bado hakuna ulazima wa kukopa kiasi hiki cha pesa ambacho serikali kupitia TPDC katika mikutano yao ya kuchangia sera ya gesi imekili pindi mradi huu utakapoanza gharama za umeme zitaongezeka maradufu ina maana kupandishwa bili za umeme kwa viwanda vingine vyote vinavyotumia nishati ya umeme Tanzania na wananchi wengine ili tulilipe deni hilo.
4. Tanzania ilifanikiwa kupata wawekezaji wengi wakubwa kwa kuwa waliambiwa njooni muwekeze Tanzania, njooni mwekeze kusini kwa kuwa kuna bandari ya asili yenye kina kirefu , kiwanja kikubwa cha ndege, gesi nyingi, uranium, makaa ya mawe,chuma n.k, Wawekezaji waliokuwa wanakuja kuwekeza si kama walikuwa wanaangalia masoko ya Tanzania, na miradi iliyokuwa inawekezwa mingi ni mikubwa sana kama kiwanda cha mbolea cha wamarekani, Dangote n.k, Wao walikuwa na masoko yao tayari South Afrika, Angola n.k hata BG gesi yao tayari wana soko india ,wawekezaji walikuja kufuata huku malighafi na bandari na eneo yani mazingira mazima ya kusini.
Hawa wawekezaji hawakufuata Dar wala Bagamoyo na wangeweza kuekeza nchi yoyote ila walifuata kusini kwa ajili ya fursa zilizopo kule.
Nachokuambia kitendo cha kuondoa gesi mpaka sasa wawekezaji wengi wameondoa imani na Tanzania na miradi mingi ambayo tayari menejimenti zilikuwa zimeshaanza tayari wameshaondoka.
Hii gesi kutotoka Mtwara kwa sasa ni faida kwa Tanzania mzima siyo kusini mambo bado kabisa haijafika muda wa kukopa pesa nyingi na kwenda huko kwa hili la mkataba wa miezi 18 kukamilika kwani kabla ya miaka miwili ya kumaliza muda wao inatupasa tufikiri kuwa huu mkataba una lengo la kuwanufaisha wachache kabla ya kuondoka madarakani.
NOTE:
Baaydhi ya vyombo vya habari kama gazeti la uhuru linapotosha watanzania na kusema wanaogoma ni wachache , si Mtwara tu kusini yote wanagoma na kwa hilo halina itikadi ya vyama, huyu Ghasia waliomtaja wanamuunga mkono si kweli na kwa hili hata wanakijiji wa kijiji chake hawamtaki kabisa hata kumuona. Vyombo vya habari njooni kusini mutasibitisha hilo.
28/12/2012 waziri mwenye dhamana alikuwa anojiwa na Channel 5 anawadanganya watanzania gharama za umeme zitapungua wakati TPDC katika mikutano yao yote wanasema zitaongezeka maradufu, kuna vyombo vya habari kama clous wanaropoka , hawajafika,hawajaona mikataba na hakika wao walienda siku ya uzinduzi tu pale kinyerezi, hawajui lolote kuhusu hii gesi, jaribuni kufanya uchunguzi mnaondoa imani kwa wasikilizaji.
Kwa hili vyovyote mtakavyofanya mwisho wa siku ukweli utajulikana tu.
Watanzania wote tuungane tuwe wamoja tusikubali keki ya Taifa wale wajanja wachache.
Kwa kuthibitisha keki ya taifa inataka kuliwa na wajanja wachache katika gazeti la daily news la 05 july 2012 waliripoti kuwa wawekezaji wawili wanakwenda kwenda kuwekeza kiwanda cha mbolea ya Urea wakimnukuu kutoka Dodoma muheshimiwa Adam Malima,na kiwanda hiki kingekuwa kikubwa kusini mwa bara la Afrika na wangeuza mbolea katika nchi za Malawi,Zambia,msumbiji,Rwanda,Burundi,kenta,Uganda<Drc,visiwa vya comorona sudani lakini ikatokea taarifa katika mtandao wa jamii wa forum kuwa Rostam Azizi akishirikiana na Mawaziri anatuhumiwa kukwamisha kiwanda chambolea kisijengwekwa sababuwao wanapata mabilioni kwa kuagiza mbolea toka nje ya nchi na kuiuzia serikali,huu nimfano tu wa watu wachache wanavyoiyumbisha nchi kwa maslai yao binafsi,
Pia kulikuwa na kampuni binafsi ya umoja light kusambaza umeme katika mikoa ya mtwara,lindi na Ruvuma lakini serekali ilipinga kwakuwa kampuni ya rostam azizi ndiyo wanatenda ya kusambaza mafuta katika magenereta ya kuzalishia umeme katika sehemu zinazotumia mitambo ya mafuta katika mikoa hiyo