Ukweli kuhusu dunia (earth)

Mfano wako wa gari nimeuelewa sana, hivi mkuu mfano ndo nipo kwenye gari kama ulivyosema, yaani gari inavyotembea na ndivyo na mimi ninavyotembea maana nipo ndani ya gari.

Swali, Je ni kipi kinafanya nisiihisi speed ya dunia wakati nikiwa ndani ya mwendo mwingine wowote ule kama Gari, Train n.k speed ninaihisi?
 
kinachokufanya uihisi speed ya gari ni vitu vingi kwanza speed yenyew ya gari haipo costant, kuna wakati inaongezeka na kuna wakati inapungua so lazima utaihisi hiyo hali, pia gari inapita kwenye bara bara ambayo sio tulivu kwanza uwepo wa kona kona lazima wewe utazihisi, pia mashimo shimo barabarani yatakufanya uhisi kuwa upo kweny chumba kinachotembea.

Jiulize watu wanasafiri na ndege au meli wanawezaje kutembea ndani ya vyombo hivyo hali ya kuwa vipo kwenye mwendo? ni kwa kuwa vyombo hivyo vinakuwa vimetulia tofauti na magari....

sasa fikiria ukubwa hii dunia, wewe ni kajidude kadogo sana juu ya uso wa dunia yaan kadogo sana so huwez ukahis chochote kutokana na mwendo wa dunia, maana dunia ipo katika constant speed, na hakuna vizuiz vyoyote....
 
mtoa mada unamaanisha kuna sehemu ukifika utasema apa dunia imeishia?,na kama ipo flat na hakuna gravity kwanini maji ya bahari ayamwagiki uko mwisho ni sawa na kumwaga maji juu ya meza?
 
Natamani nikupe bia Kreti Nzima
 
Earth moves very fast. It spins (rotates) at a speed of about 1,000 miles (1600 kilometers) per hour and orbits around the Sun at a speed of about 67,000 miles (107,000 kilometers) per hour. We do not feel any of this motion because these speedsare constant.
 
Wewe hujaelewa vizuri unachokitetea.

Adui mkubwa wa Gravity ni Atmospher hasa Hewa inayosababisha au kusaidia ueleaji na ubebaji wa objects/organisms kutoka ardhini na kwenda hewani.
 
Good explanation...!

Mfano mzuri ni kumbikumbi, akishatoka manyoya hawezi kupaa tena angani na anaathiriwa sasa na force of gravity
 
hii mada nlishawai kuiona hapa jukwaani kdg mtoa mada alikuwa na baadhi ya hoja zenye Mashiko ila kwa huyu wa leo naona hoja zake ni dhaifu sana sa mfano anadai Antactica ndo ukingo wa dunia kwenye flat earth sa duara gani lenye ukingo sehem moja tu.. ama hyo Atanctica imezunguuka duara lote!... [HASHTAG]#shameonyou[/HASHTAG]
 

wewe jamaa ni Genius, heshima yako mkuu.
 
Ndio maana nilifeli physics
malumbano ya Physics, Mathematics na. Geography. sisi ngoja tuendelee kuangalia mtanange na kuhitimisha kama yule babu kwa mjukuu wake kuhusu ndege kuelea angani, 'Mwanangu hayo ni mambo ya kitaalam sana'
 
Kama dunia ni flat tuambie umbo lake likoje ni mviringo kama sarafu au ni mstatili au umbo gani?? Na kama ni mstatili au duara mfano wa sarafu tupia picha tuone ukingo wake.
 
Mi mwenyewe nashangaa eti dunia inazunguka !

Mbona mi kila siku niko pale pale sizunguki nikafika hata china ?
Mkuu upo nyuma sana tena sana,maana hujui hata jinsi inavyozunguuka,hebu cheki hii VIDEO unaweza kujua ni jinsi gani inavyozunguuuka.
 
Mkuu upo nyuma sana tena sana,maana hujui hata jinsi inavyozunguuka,hebu cheki hii VIDEO unaweza kujua ni jinsi gani inavyozunguuuka.

Mkuu hapa sijaambulia hata moja !
Bado nina maswali mwengi ambayo hayana majibu ....

Kama dunia inazunguka,inazunguka na sisi ?
Kama inazunguka na sisi kwa nini tunasafiri kwenda sehemu flan ?
 
Me hua najiuliza kama kweli dunia sio sphere, hao ambao wanatuaminisha wanataka wapate nini?? mleta mada nijibu swali, hii dunia ikiwa sphere hao wanasayansi wanaoshikilia hii point wanafaidika na nini kudanganya na kwanini iwe ni siri kubwa hivyo??
 
siezi nikatema facts 200 humu ndani... nyingine ni physics zaidi, ntngne mpaka video na nyngne mpaka picha ndo utaelewa zaidi... fuata hyo link uangalie just a short video alafu urudi hapa....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…