Ukweli kuhusu aliens

waterproof

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2020
Posts
388
Reaction score
352
Kuna minong'ono na maneno ya wazi kwamba kuna viumbe wa ajabu wamekimbilia katika dunia na kusababisha hofu na wasiwasi wa maisha ya binadamu wa kawaida, kwa mujibu wa mwanasayansi wa fizikia na nyuklia raia wa Canada Bwana Stanton Friedman aliwahi kunukuliwa akisema, "dunia imekua ikitembelewa sana na viumbe wa ajabu maarufu kama Aliens kwa lengo la kuangalia mienendo kadhaa ya kitekinolojia na maisha ya kawaida na muda sio mrefu wataweka makazi kabisa duniani, Hakuna doa la mashaka kwamba viumbe wa ajabu wenye akili nyingi sana wanafanya safari zao kuja duniani".

Bwana Friedman mwenye umri wa miaka 82 alikua akichunguza ajali ya chombo cha anga za juu hususani ajali ya mwaka 1947 iliohusu chombo cha anga kilichopata ajali mbaya katika anga za juu na kueleza kilipotezwa na kitu kisicho cha kawaida kabisa kilichokua na viumbe wa ajabu,

Aidha, aliwahi tena kunukuliwa akisema kuwa, faili lenye taarifa za siri sana za CIA juu ya uwepo wa viumbe hao ni moja ya ushahidi wa uwepo wa viumbe hao, nafikiri viumbe hao maarufu Aliens wanataka kulinda anga lao ambalo limekua likitembelewa sana na vyombo na binaadamu kutoka duniani.

Naye aliekua Waziri wa Ulinzi wa Canada Paul Hellyer aliwahi kunukuliwa akisema kuwa "dunia imekua ikitembelewa na viumbe hao kwa miongo kadhaa sasa, mwaka 1961 kulikua na vyombo vya anga vya ajabu 50 vilivyojulikana kama UFO na visivyo vya kawaida kabisa vikiruka kutoka kusini ya dunia vikielekea Urusi na Ulaya."

PIA,

Mtafiti wa masuala ya Aliens, Stewat Swardlow, na wengine wengi wamewahi kushuhudia kwa nyakati tofauti nyaraka za siri kutoka kwenye serikali tofauti tofauti kubwa duniani kama vile Marekani,China,Urusi,Japan,Ujerumani na nyingine zikionesha ukweli wa uwepo wa viumbe hawa.


Zifuatazo ni 4 kuu na kubwa za Aliens wanaopatikana kwenye mkanda wa Kuiper Belt...

1;Insectoid Aliens
2;Grey Aliens
3;Humanoid Aliens
4;Reptoid Aliens

Aina hizi ndizo ambazo serikali nyingi za dunia zimekubaliana na uwepo wake,lakini kwa siri kwa sababu ndiyo aina ya Aliens ambayo imewahi kuonekana hapa duniani. Lakini tujue kwamba,kama nilivyosema hapo juu ni kwamba wataalamu hawa wanasema kwamba kwenye mkanda wa Kuiper kuna mamia ya aina za Aliens lakini wanasema kwamba Aliens aina ya Insectoid ndiyo super power huko...

Insectoid, wanadaiwa kuwa na uwezo mkubwa sana wa kufikiri na kuweza kuiongoza au kuirubuni akili ya kiumbe mwingine afikiri kama atakavyo yeye na hii ndiyo imefanya wakawa na nguvu sana eneo hilo ambalo limezua mjadala na vurugu sana baina ya wataalam wengi.Kwa maana hiyo Insectoid ndiyo aina bora zaidi ya Aliens inayopatikana eneo hilo.

Hawa viumbe ni hatari sana kwa maisha ya binadamu na karibia kila kundi la Aliens lina ajenda yake kuhusiana na binadamu na dunia hii. Kama nilivyosema kuwa kuna aina nyingi ya Aliens,hapa nitaeleza makundi machache ya Aliens na ajenda zao dhidi ya dunia na sisi wakazi wake....

#Mantids_Aliens.

Hawa wao wanadai kuwa dunia hii ni yao na waliishi hapa kwa miaka mingi kisha wakaondoka kwenda kutafuta maisha maeneo mengine na sasa wanahitaji kurudi.

#Lionestic_being_Aliens.

Hawa wanafanana sana na binadamu lakini pia wanafanana na Simba. Nimekosa picha ya kuonesha namna wanavyoonekana lakini inastaajabisha sana.Hawa lengo lao ni kuondoa mtindo wa kisiasa ulioko hapa duniani.Hawa wao watasubiri hadi tumeshamalizana sana na ndipo watakuja na kuondoa kabisa mtindo huu wa siasa ulioko hapa duniani....

#Humanoid_Aliens.

Hawa ni miongoni mwa Aliens wengi na wenye uwezo mkubwa sana na wa hatari. Inadaiwa kwamba miongoni mwa aina za hawa humanoid Aliens ipo aina ambayo inafanana kabisa na binadamu na unaweza kukaa naye kwenye kiti na usijue kama siyo binadamu. Hawa wanaamini kuwa dunia hii iko chini ya mamlaka yao na ni eneo lao. Wanataka kuisafisha dunia yote na kuhakikisha hakuna binadamu anabakia hapa. Wanaamini wana haki ya kufanya yote na chochote watakacho na ajenda yao kubwa ni kuwaondoa binadamu.
 
Agenda zao hao Aliens binadamu/mwandishi amezijuaje?
 
๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ nimecheka hao wanaotaka kurudi Yani waondoke halafu hawakuacha familia then wanataka kurudi! Hawa dawa yao ni turampu tu!

Nje na masihara nakuwa napata kigugumizi juu ya hili swala la hawa alien!. Sijui Kama kweli wapo au tunachezewa kanyabazongo tu na wakuu wa dunia hi!.
Hili jambo ni pana sana ktk jicho yakinifu,yamesemwa mengi juu ya Hawa viumbe na kiukweli nikiiangalia ulimwengu naona kabisa unahubiri juu ya kuwepo maisha mengine zaidi ya hapa duniani!.
Lkn bado hakuna uhakika wa dhati wenye kuthibitisha uwepo wa hawa viumbe,kitendo cha kuona mi UFO bado haitoshi maana bado mtu unakuwa huna hakika ya kwamba hizo uitazo UFO ni man made or aliens..? Mambo ni kizungumkuti! Still nipo nuetral! Nitaamini hili siku nikimuona huyo alien na kuwajua kiundani zaidi.
 
Uwepo wa alien Ni kama hoax news

Habari za kufikirika kwa nini nasema hivyo ?

Ingawa zaidi ya exoplanets 4,000 zimethibitishwa kwenye galaxy yetu," Ambayo inaitwa"milk way" karibu theluthi yao katika kiwango cha ukubwa wa Dunia, utafiti bado uko katika hatua yake ya mapema kupata ushahidi wa maisha kwenye sayari hizo and yet mpka sasa baadhi zilizofanywiwa uchunguzi azijaonyesha uwepo wa maisha hivyo no alien


Kwa kuwa Galaxy ya Milky Way sasa inasukuma miaka bilioni 14, utaftaji bado unaendelea.

Pia

Mnamo Novemba 2013 astronomer
waliripoti, kutokana na vipimo na data za kifaa cha Kepler, kwamba kunaweza kuwa na sayari zenye ukubwa wa Dunia bilioni 40 katika maeneo ya makao ya nyota kama Jua na vijeba vyekundu katika Milky Way,.

Sayari 11 bilioni ambazo zinaweza kuzunguka kama nyota za Jua.

Mnamo mwaka wa 2021 wanasayansi walichapisha makadirio ya viwango vya kuwepo kwa sayari zenye ukanda wa miamba karibu na nyota kama Jua

Uhakiki wa 2015 ulihitimisha kuwa sayari exeplanets Kepler-62f, Kepler-186f na Kepler-442 zilikuwa na uwezekano wa kuwa na viumbe

Hizi ziko umbali wa miaka 1,200, 490 na 1,120 kutoka kwenye dunia so mtoa mada hapa unaona zko mbali sana hata uchunguzi unakuwa mgumu kufanyika.

Kati ya hizi, Kepler-186f iko karibu zaidi kwa ukubwa duniani, ikiwa na ukubwa wa mara 1.2 ya Dunia, na iko kuelekea ukingo wa nje wa eneo linaloweza kukaa karibu na nyota yake nyekundu .

So kama hakuna life in another part of Galaxy that means no alien
 
๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ Mkuu hao alien waliondelea ndo wanataka kuizimisha hiyo Rover kwa rungu..๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ halafu hako kengine kamekaa pozi kana kwamba kanataka kukata gogo..๐Ÿ˜…
 
Resident Alien Series ipo S1 imefika episode ya 7
 
Aisee hatari sana hao wanaodai hii dunia ni yao watakua ndo annunaki wa enzi zile wanataka kurudi tena!
 
Tunataka kuchezewa akili tu na wanaojifanya wajuzi wa Dunia.Na hakuna cha Alien wala nini;hayo ni majini ambayo yatamwagwa na Shetani na mawakala wake wa kibinadamu ili kumkasirisha Mungu zaidi na kuchochea Mwisho wa Dunia (Kiama).

Satanic agents hao.
 
Hivi hawa Aliens huwa wanaonekana huko Ulaya na Amerika tu

Sijawahi kusikia ati Aliens wameonekana Igunga au labda wanatudharau?
 
Alien ataweza ku fight na Alen na aka win au ni matambo tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ