Ukiwa na shemejio/mdogo wako kicheche

Ukiwa na shemejio/mdogo wako kicheche

Samawia

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2017
Posts
592
Reaction score
466
Wewe ni dereva wa masafa marefu, wakati mwingine miezi miwili huonekani nyumbani, mkeo naye mjasiriamali muda mwingi anakuwa kutafuta riziki, ma house girl nao ndio hivyo mara leo yupo mara kesho kaondoka, mkeo ana mdogo wake wa kike baada ya kuona usumbufu wa ma wa mabinti wa kazi anaamua kuja kukaa kwa dada yake ili awe anamsaidia kazi.

Baada ya miezi kama minne mkeo anagundua mdogo wake anatoka na majirani wawili (waume za watu), baadaye tena anakuja kuambiwa mdogowe ana wanaume wengine kadhaa. Mkeo anaamua kukushirikisha mumewe kuhusu mienendo michafu ya shemeji yako, shemeji yako 1,2,3,7,9 30.

Mume unaanza kuwaza namwamini sana mke wangu. Je, kwa tabia hii ya mdogo wake haiwezi kumletea vishawishi naye akaanza tabia chafu? Sijui nimwambie dada yake amtimue au nimtimue mwenyewe? Mkeo naye anawaza, wake za hawa michepuko wa mdogo wangu tunaheshimiana sana je wakijua itakuwaje si watajua mimi na mdogo wangu letu moja. Je, nitaheshimiana nao kama zamani? Je, nimwambie mdogo wangu aachane na hayo mambo au nisimwambie ila nimrudishe tu nyumbani?

Vaa uhusika wa mume au mke, utafanyaje?
 
Unapaswa kushika maisha yako na ya shemeji/ mdogo mtu atajijua siku akikamatwa..unamwambia kweni umemshika? tabia ya mdogo mtu pia siyo tabia ya mkubwa mtu
 
We muache aendelee kulichuma janga siku likimpata la kumpata atajua cha kufanya manake mtu mzima huyo
 
Kwa ushahidi upi?kama unaushahi hata wa sms mnachukua simu, then screenshot kisha mpe mkono wa kweheri kwenye K na M hakunaga makatazo.
 
Dada yake ndo ni wa kukaa nae chini we hayakusu fanya life yako asiposikia likimkuta la kumkuta we hata hasara huna
 
Mimi kama mwanaume ninawaza.

"Huyu binti ana ukali gani wa kuwatuliza wame za watu na wengine huko nje? Acha nifanye uchunguzi wa practical"
 
Nilishasema siwezi kuvurugiwa nyumba yangu na mtu wa kuja ambaye kuna siku ataondoka lakini nyie mtaishi hapo mpaka umauti,tabia ambazo siwezi kuzivumilia kwa ndugu zangu na wanangu ni umalaya na wizi.
Nimemaliza mkuu,nawasilisha.
 
Mabinti wa kazi hawakai? Shemeji yako anatembea na mabwana za watu?[emoji144][emoji144][emoji144] Nisiwaze vibaya Ila mkeo kuna Tabia anayo kwaiyo labda mdogo wake alimwambia aiache kwaiyo anatafuta namna ya kumtimua usikurupuke kufanya maamuzi ya kumfukuza embu mpeleke kwao kwanza mengi utayajua
 
Nilishasema siwezi kuvurugiwa nyumba yangu na mtu wa kuja ambaye kuna siku ataondoka lakini nyie mtaishi hapo mpaka umauti,tabia ambazo siwezi kuzivumilia kwa ndugu zangu na wanangu ni umalaya na wizi.
Nimemaliza mkuu,nawasilisha.
Nimekuelewa mkuu
 
Back
Top Bottom