Masokotz
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,832
- 6,467
Hili ni swali ambalo najua kuna ambao wanajiuliza pia.
Kwa jinsi hali ilivyo na namna jambo hili linavyoshughuikiwa hapa nchini wengi watakuwa wanajiuliza swali hili kwa hofu kubwa na mashaka.
Sababu za mashaka ni ukweli kwamba wengi wameshaona kwamba kupata CORONA ni sawa na KIFO na kwa jinsi ambavyo imethibitika pasi na shaka kwamba mfumo wetu wa afya ni mbovu basi wengi wana hofu kubwa kwa kutokujua cha kufanya.
Le nataka tujadili kwa kina nini cha kufanya iwapo unahisi kwamba una maradhi haya.
NB.KUWA MAKINI SIO KILA HOMA NI CORONA-Vipimo viko DAR ES SALAAM TU kwa hivyo inahitaji uvumilivukuthibitisha iwapo una korona ila ili ujisaidi basi kila unapokuwa na homa basi fikiri kwamba ni korona na uchukue hatua ya kuzuia maambukizi ya ziada
Kwa jinsi hali ilivyo na namna jambo hili linavyoshughuikiwa hapa nchini wengi watakuwa wanajiuliza swali hili kwa hofu kubwa na mashaka.
Sababu za mashaka ni ukweli kwamba wengi wameshaona kwamba kupata CORONA ni sawa na KIFO na kwa jinsi ambavyo imethibitika pasi na shaka kwamba mfumo wetu wa afya ni mbovu basi wengi wana hofu kubwa kwa kutokujua cha kufanya.
Le nataka tujadili kwa kina nini cha kufanya iwapo unahisi kwamba una maradhi haya.
- Hatua ya kwanza ni kuwajulisha watu wako wa karibu juu ya wasi wasi wako na kwamba ungependa sasa Ujitenge nao na kuwa peke yako na huku ukiwasihi na wao wajitenge na watu wengine na kujitenga baina yao-SOCIAL distancing
- Hatua ya pili ni kuzitazama dalili ulizo nazo.Kulingana na dalili ulizo nazo unaweza kuamua aina ya tiba.Kumbuka katika kipindi hiki kinga yako ya mwili lazima iwe imara hivyo basi kula vyakula vyenye kuongeza kinga mwili huku ukkitumia muda mwingi kupumzika na iwpo una dalili kama vile homa,mafua,kikohozi basi tumia dawa za kutibu dalii hizo kama vile -Anti cough syrup,Anti allergy,pain killers kama panadol n.k.
- Hatu ya tatu ni iwapo unaona dalili zinakuwa kali basi toa taarifa kwa kituo cha dharura ya Korona waje kukuchukua.Iwapo hawatakuja endelea kukaa hapo na usijaribu kujichanganya na watu ili kufika hospitali kwani utasambaza maambukizi.
NB.KUWA MAKINI SIO KILA HOMA NI CORONA-Vipimo viko DAR ES SALAAM TU kwa hivyo inahitaji uvumilivukuthibitisha iwapo una korona ila ili ujisaidi basi kila unapokuwa na homa basi fikiri kwamba ni korona na uchukue hatua ya kuzuia maambukizi ya ziada