Satoh Hirosh
JF-Expert Member
- Mar 30, 2021
- 5,950
- 23,263
Nimekuja mkoani kumtembelea bradha. Kuna mzigo aliniagiza nimletee. Hapa kwa bro kuna mtoto wao wa kiume ana umri kama miaka minne au tano hivi. Asee, hiki kitoto ni kitundu sijapata ona. Mbaya zaidi, babaake na mama yake wanamlea kama yai, full kudeka-deka hovyo.
Sasa ni heri wangekuwa wanamlea hovyo, akawa anawasumbua wenyewe ingekuwa hakuna shida, ila akiwa na wenzake ni kakorofi, kanawapiga wenzake. Nimejilipua zangu fulana kutoka kwa vunja bei. Ameshaitanua shingo kwa kunivuta-vuta. Imekuwa kama nanyonyesha sasa. Mara aninyang'anye simu, mara aniparamie usoni kama mbwa, alafu ana vikucha vikali.
Basi naishia kujichekesha chekesha tu mbele ya mama yake. Maisha ya ugenini yana unafiki sana. Wazazi wake wala hawastuki, wanaona poa tu mtoto wao anavyo act kama kingedere. Mamaake ananiambia 'shemeji kama junia anakusumbua mchape.' Namchapaje mtoto wa watu ugenini? Kwa nini asimkataze kusumbua wageni na kukachapa kakiendelea kuleta ubishi.
Sasa mamaake akaenda dukani akaniacha na junia tunavutana-vutana. Happy ndiyo nikambadikilia, nikamwonyesha sura ya ukauzu na kumtoa shingoni maana ilikuwa kama ananidai kwa jinsi alivyokuwa ananikaba. Nikakashika mikono na kukaminya tu vidole vyake kama naminya karanga, huku namwambi acha utundu kwa wageni mtoto. Kakaanza kulia kanaelekea dukani kwa mamaake.
Maisha ya ugenini magumu sana. Nilipanga kukaa siku mbili, ila moja tu inatosha kwa kweli. Wazazi wengine hivi mnaleaje watoto kipuuzi kama hivi? Katoto ni ka-attention seeker. Mpo katika maongezi sebuleni, kenyewe kanapita-pita na kuvuta watu nguo, ili mradi tu kaonekane kapo live. Mkikapotezea, kataangusha hata glass!
Sasa ni heri wangekuwa wanamlea hovyo, akawa anawasumbua wenyewe ingekuwa hakuna shida, ila akiwa na wenzake ni kakorofi, kanawapiga wenzake. Nimejilipua zangu fulana kutoka kwa vunja bei. Ameshaitanua shingo kwa kunivuta-vuta. Imekuwa kama nanyonyesha sasa. Mara aninyang'anye simu, mara aniparamie usoni kama mbwa, alafu ana vikucha vikali.
Basi naishia kujichekesha chekesha tu mbele ya mama yake. Maisha ya ugenini yana unafiki sana. Wazazi wake wala hawastuki, wanaona poa tu mtoto wao anavyo act kama kingedere. Mamaake ananiambia 'shemeji kama junia anakusumbua mchape.' Namchapaje mtoto wa watu ugenini? Kwa nini asimkataze kusumbua wageni na kukachapa kakiendelea kuleta ubishi.
Sasa mamaake akaenda dukani akaniacha na junia tunavutana-vutana. Happy ndiyo nikambadikilia, nikamwonyesha sura ya ukauzu na kumtoa shingoni maana ilikuwa kama ananidai kwa jinsi alivyokuwa ananikaba. Nikakashika mikono na kukaminya tu vidole vyake kama naminya karanga, huku namwambi acha utundu kwa wageni mtoto. Kakaanza kulia kanaelekea dukani kwa mamaake.
Maisha ya ugenini magumu sana. Nilipanga kukaa siku mbili, ila moja tu inatosha kwa kweli. Wazazi wengine hivi mnaleaje watoto kipuuzi kama hivi? Katoto ni ka-attention seeker. Mpo katika maongezi sebuleni, kenyewe kanapita-pita na kuvuta watu nguo, ili mradi tu kaonekane kapo live. Mkikapotezea, kataangusha hata glass!