Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 2,439
- 6,692
Wakuu,
Kama swali linavyojieleza hapo juu
Yaani kwa mfano mimi naitwa XYZ muda wa kujiandikisha alafu miezi michache baadae nikabadilisha jina langu kuwa XYS je ina maana nimepoteza haki yangu ya kupiga kura kwa kuwa jina langu limebadilika?
Sasa ukweli ulivyo ni kwamba sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2024 inaeleza “Mtu aliyeandikishwa kuwa Mpiga Kura ambaye jina lake limebadilika kutokana na ndoa au kwa sababu nyingine yoyote baada ya kuandikishwa, iwapo hajapoteza sifa za kupiga kura chini ya kifungu cha 14, atastahili kupiga kura kwa jina ambalo ameandikishwa.”
Hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2024, inayotumika upande wa Tanzania Bara na Zanzibar kwa Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano, na kwa uchaguzi wa Madiwani kwa Tanzania Bara.
Kama swali linavyojieleza hapo juu
Yaani kwa mfano mimi naitwa XYZ muda wa kujiandikisha alafu miezi michache baadae nikabadilisha jina langu kuwa XYS je ina maana nimepoteza haki yangu ya kupiga kura kwa kuwa jina langu limebadilika?
Sasa ukweli ulivyo ni kwamba sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2024 inaeleza “Mtu aliyeandikishwa kuwa Mpiga Kura ambaye jina lake limebadilika kutokana na ndoa au kwa sababu nyingine yoyote baada ya kuandikishwa, iwapo hajapoteza sifa za kupiga kura chini ya kifungu cha 14, atastahili kupiga kura kwa jina ambalo ameandikishwa.”
Hiyo ni kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya Mwaka 2024, inayotumika upande wa Tanzania Bara na Zanzibar kwa Uchaguzi wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano, na kwa uchaguzi wa Madiwani kwa Tanzania Bara.