UKAWA yaua BAWACHA na BAVICHA

Mkuu, huoni kuwa harakati za BAVICHA na BAWACHA za sasa zimefifia? Au mpaka uvalishwe miwaninya mbao ndo uone?
Hivi vikififia tatizo lako kubwa ni nini, kama umeshindwa kuijenga na kuishauri UVCCM inayochungulia kaburi utayaweza ya Bavicha.
 
niliiona ile thread na nilichangia sana.. ptrobas anachapa sana kazi tatizo cdm wanapenda mtu apambwe sana na media kila gazeti wakishika waone jamaa kaandikwa. mshikajia anachapa sana kazi
Anachapia wapi huko baharini au mtoni hatumuoni huku duniani yuko wapi?
 
Hivi vikififia tatizo lako kubwa ni nini, kama umeshindwa kuijenga na kuishauri UVCCM inayochungulia kaburi utayaweza ya Bavicha.
Jibu hoja acha kuanzisha hoja juu ya hoja bavicha imekufa au haijafa?
 
Mkuu, huoni kuwa harakati za BAVICHA na BAWACHA za sasa zimefifia? Au mpaka uvalishwe miwaninya mbao ndo uone?
mkuu inawezekana kwa macho yako na mtazamo wako ukaona zimefifia, huenda wamebadili mbinu katika kupambana na chama dola.any way ukiona shabiki wa simba anawaambia yanga wameshuka kiwango tofauti na zamani, inabidi wajiangalie mara mbilimbili. Ni nadra sana adui wako kukurekebisha pale unavyofanya vibaya.
 
Hivi vikififia tatizo lako kubwa ni nini, kama umeshindwa kuijenga na kuishauri UVCCM inayochungulia kaburi utayaweza ya Bavicha.
Utamu wa siasa ni pale kunapokuwa na kambi mbili zenye uwezo unaokaribiana. Kufa kwa chadema kutasababisha watu wengi wakose ajira hasa misukule ya Kinondoni
 
Mkuu, kwa kawaida harakati za mabaraza zinakuwa za wazi. Hizo mbinu za kificho wanafanya Red Brigade
 
Utamu wa siasa ni pale kunapokuwa na kambi mbili zenye uwezo unaokaribiana. Kufa kwa chadema kutasababisha watu wengi wakose ajira hasa misukule ya Kinondoni
haa haa kwani kazi ya kuwapa vijana ajira si ni kazi ya serikali iliyopo madarakani? Nimeamini ccm imepoteza dira kama chama tawala.
 

Hakuna kitu kibaya kama mtu ukifanya kazi ama shughuli nyingine alafu usipate mrejesho nyuma/feedback....UKAWA wamefanya kazi nzito inayowanyima usingizi ccm.!

Kwamba, post yako ni sehem ya feedback na inatafsirika waziwazi unakusudia kusema nini....Just simple....."MMEKAMATIKA VIBAYA MNOO, MMEKABWA KOO"!
 
UKAWA ni wasakatonge ~by Zitto.
teh teh, msiwaamini wanasiasa -by Zitto.

muungano wa vyama vya siasa vitasaidia kuitoa ccm madarakani…Zitto
 
Moto upi wa bawacha labda kunywa pombe wala siyo kitu kingine kunamoto gani wameonesha?
Nimekwambia muulize mama Escrow atakwambia.

PIGA KURA YA HAPANA KWA KATIBA PENDEKEZWA
 
naona umemisi kuandika post, subiri bmk lianze uendelee kuripoti. maana ule moto wa ukawa kwenye serikali za mitaa umewashtua sana.

Ndugu,
Kwa CCM kupata zaidi ya 80% ya viti vilivyopigiwa kura nchini, kweli itakuwa imeshtuliwa sana.
 
Uko sawa mkuu halafu hao bawacha na bavicha wenyewe hakuna mtu au kiongozi mwenye akili ya kiuongozi hata mmoja wengi wao ni wahuni tu.
Wewe tumia akili unapo evaluate vichwa vya watu. Akili ya Halima inamzidi Sofia Simba mara elfu moja. Au unaona Sofia Simba alipowakataza wanawake wawanyime waume zao tendo la ndoa kwa kuikataa ccm alikuwa anatekeleza sera ya UWT au alikuwa anajidhihirisha alivyo mwendawazimu?

Patroba ana akili nyingi kumzidi hata Mwenyekiti wako wa Chama.

Shika adabu yako!
 
Mkuu, huoni kuwa harakati za BAVICHA na BAWACHA za sasa zimefifia? Au mpaka uvalishwe miwaninya mbao ndo uone?
Harakati za Bavicha zimefifiaje? Mbona tunakamua kama kawa? Au kwa vile hutuoni TIBISII?
 

Kama kufa kwa BAWACHA na BAVICHA na kushamiri kwa UKAWA kutapelekea CCM kuondoka Madarakani.Natamani vife hata leo.
 
Ndugu,
Kwa CCM kupata zaidi ya 80% ya viti vilivyopigiwa kura nchini, kweli itakuwa imeshtuliwa sana.
Unafurahia kura ushindi wa mapingamizi,
ushindi wa kutangaza aliyeshindwa mshindi,
ushindi wa kiapisha aliyeshindwa na kumwambia mshindi aende mahakamani.

PIGA KURA YA HAPANA KWA KATIBA PENDEKEZWA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…