Vyama vinavyounda umoja wa Katiba Ukawa vimeshindwa kukubaliana mgawanyo wa vyeo na badala yake kuamua kwenda Jangwani kwanza kwenye mkutano wa hadhara kisha ndiyo warejee kwenye meza ya mazungumzo.
Kikao kilichohusisha Viongozi wa vyama vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi kimeshindwa kufikia makubaliano baada ya baadhi ya Viongozi wa vyama hivyo kutokubaliana na mgawanyo wa nafasi za kugombea katika maeneo kadhaa.
maeneo yaliyoonesha mvutano katika kikao hicho ni pamoja na JIMBO la Ubungo ambalo hivi sasa linashikiliwa na John John Mnyika wa Chadema. JIMBO hili pia linawaniwa na Julius Mtatiro wa CUF, Jimbo la Vunjo ambalo limeibua mvutano Kati ya James Mbatia wa NCCR na John Mrema wa Chadema pamoja na Jimbo la Kawe ambalo Mbatia anataka mtu wake ndo agombee badala ya Halima Mdee wa sasa.
mvutano Huo ambao umedhihirisha kuwepo kwa Hatari ya umoja Huo kudumu, umesitiswa baada ya wenyeviti wa vyama vinavyounda umoja Huo kukaa kwa faragha na kuamua kuahirisha kikao hicho mpaka baadae wiki ijayo ili kupisha maandalizi ya mkutano wa Jangwan wa leo hii.
Kikao kilichohusisha Viongozi wa vyama vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi kimeshindwa kufikia makubaliano baada ya baadhi ya Viongozi wa vyama hivyo kutokubaliana na mgawanyo wa nafasi za kugombea katika maeneo kadhaa.
maeneo yaliyoonesha mvutano katika kikao hicho ni pamoja na JIMBO la Ubungo ambalo hivi sasa linashikiliwa na John John Mnyika wa Chadema. JIMBO hili pia linawaniwa na Julius Mtatiro wa CUF, Jimbo la Vunjo ambalo limeibua mvutano Kati ya James Mbatia wa NCCR na John Mrema wa Chadema pamoja na Jimbo la Kawe ambalo Mbatia anataka mtu wake ndo agombee badala ya Halima Mdee wa sasa.
mvutano Huo ambao umedhihirisha kuwepo kwa Hatari ya umoja Huo kudumu, umesitiswa baada ya wenyeviti wa vyama vinavyounda umoja Huo kukaa kwa faragha na kuamua kuahirisha kikao hicho mpaka baadae wiki ijayo ili kupisha maandalizi ya mkutano wa Jangwan wa leo hii.