UKAWA Wanatumiwa Kuleta Machafuko

UKAWA Wanatumiwa Kuleta Machafuko

Mwenyekiti wa Tanzania Kwanza ambao ni umoja wa muungano wa vyama saba vya siasa ikiwamo CCM katika bunge maalum la katiba Ndugu.Agustino Matefu amesema leo kuwa UKAWA inatumiwa ili kuleta machafuko na kuvuruga amani ya nchi.

Mwenyekiti huyo ameeleza hayo katika mohojiano kama mgeni katika kituo cha matangazo cha UHURU Fm.Matefu amesema kuwa nchi za uholanzi na Omani zimekuwa zikitumika kufadhili shughuli mbalimbali za UKAWA kwa kutoka pesa ambazo zimekuwa zukiingizwa katika akaunti binafsi za viongozi wa umoja huo.

Amesema kuwa Mbowe na Slaa mpaka sasa kupitia akaunti zao binafsi wameshapokea kiasi cha Sh.1,700,000(Awamu ya kwanza) huku awamu ya pili na tatu jumla ikiwa ni Dola 850,000/=kutoka Uholanzi.Wakati kwa upande wa CUF Prof.Ibrahim Lipumba kupitia akaunti yake binafsi amepokea kiasi cha dola 400,000/=kutoka Oman.

Ndugu Matefu ameeleza kuwa viongozi wa UKAWA wanatumika kama kijiko kwa manufaa ya watu wengine nje ya nchi kutaka kutuvuruga. Amesema kuwa Umoja huo hauna lengo zuri na nchi hii ndiyo maana pamoja na vikao vyote vyama usuluhishi bado wameendelea kuwa wagumu hawataki kumsikiliza yeyote.

Awali kabla ya hapo Ndugu Matefu kupitia umoja huyo alishazungumza na waandishi wa habari kuwaagiza Viongozi wa UKAWA ndani ya siku Saba wewe wamerudi Bungeni vinginevyo atamwaga Siri nzito zilizojificha nyuma ya Muungani humo.


Tanzania Kwanza ukiwa ni muungano wa vyama saba vya siasa katika Bunge la Katiba unajitambulisha kuwa ni umoja unaotetea maslahi ya nchi,kujali utaifa na kuangalia kwanza masuala muhimu ya kitaifa bila kujali tofauti zao kichama,kisera,kimtazamo na kiitikadi.

WAJINGA ndiyo waliwao, wabunge wa UKAWA wanapata huo mgao au ni viongozi peke yao ndiyo wanalamba?
 
Huu ni ujinga kabisa hakuna nchi ambayo inaweza kutetea hii rasimu ya Warioba kwani kwa jinsi ilivyo itawanyima fursa ya kuendelea kutuibia kwa hiyo Chama ambacho kinaweza kufadhiriwa na kinafadhiriwa ili kuvuruga mchakato huu ni CCM kwani wanapingana na maoni ya wananchi ambayo kiuhalisia ni kikwazo kwa wezi wa rasilimali zetu.

Umeshaambiwa UKAWA wanafadhiliwa na Uholanzi na oman, haya na wewe pika uzushi wako, CCM wanafadhiliwa na nani?
 
CCM hawakudhani kuna siku CUF na CDM wanaweza kukaa meza moja na kuungana!! kweli hii ndiyo dawa ya hawa wababaishaji wa Lumumba - Tumewashika.

UKAWA mpango mzima!! UKAWA habari ya mujini.
 
Wakamatwe kama uzi huu ni waukweli na mtoa uzi naye anaswe alete vielelezo
 
Huyo Agustino Matefu kama amesema haya nje ya bunge kwa nini asishtakiwe mahakamani?
 
Kama wafadhili wanatoa fedha kutetea maoni ya wananchi kuna ubaya gani? Huyo anayepinga maoni ya wananchi ana ajenda gani zaidi ya kuhakikisha rasilimali za nchi zinatumiwa kwa maslahi ya wageni na CCM? Wafadhili please ongezeni misaada kwa watetezi wa maoni ya wananchi.
 
AO WATU WA NJE (oman & uholanzi) WANATUVURUGA VIPI ? Kwani MADAI YA UKAWA NI NINI? Na pili watu kupewa pesa ndo kiashiriano cha kwamba tunavurugwa mbona ata mimi HUPEWA PESA NA BABA KWA AJILI YA MATUMIZI YANGU BINAFSI LAKINI PIA KAKA/MJOMBA/RAFIKI HUNIPA PIA je io inadhihirisha kua huvuruga familia yetu?


EMU FIKIRI KWA UMAKINI AFU NDIO USEME TENA
 
hata shetani akisaidia kuyatoa mapepo (CCM) nitampongeza
 
Uholanzi na Oman waivuruge Tanzania ili wanufaike na nini?..mawazo yakipumbav kweli!
 
Jamani mnisaidie pengine mi macho yangu. Awamu ya kwanza wametoa sh 1,700,000......Uholanzi watoe mil moja na laki saba..........mbona kama vihela kiduchu sana.......huu uongo haukupangwa vizuri.
 
Mwenyekiti wa Tanzania Kwanza ambao ni umoja wa muungano wa vyama saba vya siasa ikiwamo CCM katika bunge maalum la katiba Ndugu.Agustino Matefu amesema leo kuwa UKAWA inatumiwa ili kuleta machafuko na kuvuruga amani ya nchi.

Mwenyekiti huyo ameeleza hayo katika mohojiano kama mgeni katika kituo cha matangazo cha UHURU Fm.Matefu amesema kuwa nchi za uholanzi na Omani zimekuwa zikitumika kufadhili shughuli mbalimbali za UKAWA kwa kutoka pesa ambazo zimekuwa zukiingizwa katika akaunti binafsi za viongozi wa umoja huo.

Amesema kuwa Mbowe na Slaa mpaka sasa kupitia akaunti zao binafsi wameshapokea kiasi cha Sh.1,700,000(Awamu ya kwanza) huku awamu ya pili na tatu jumla ikiwa ni Dola 850,000/=kutoka Uholanzi.Wakati kwa upande wa CUF Prof.Ibrahim Lipumba kupitia akaunti yake binafsi amepokea kiasi cha dola 400,000/=kutoka Oman.

Ndugu Matefu ameeleza kuwa viongozi wa UKAWA wanatumika kama kijiko kwa manufaa ya watu wengine nje ya nchi kutaka kutuvuruga. Amesema kuwa Umoja huo hauna lengo zuri na nchi hii ndiyo maana pamoja na vikao vyote vyama usuluhishi bado wameendelea kuwa wagumu hawataki kumsikiliza yeyote.

Awali kabla ya hapo Ndugu Matefu kupitia umoja huyo alishazungumza na waandishi wa habari kuwaagiza Viongozi wa UKAWA ndani ya siku Saba wewe wamerudi Bungeni vinginevyo atamwaga Siri nzito zilizojificha nyuma ya Muungani humo.


Tanzania Kwanza ukiwa ni muungano wa vyama saba vya siasa katika Bunge la Katiba unajitambulisha kuwa ni umoja unaotetea maslahi ya nchi,kujali utaifa na kuangalia kwanza masuala muhimu ya kitaifa bila kujali tofauti zao kichama,kisera,kimtazamo na kiitikadi.
Ungetuwekea ushahidi wa hizo transaction tungeamini lakini maneno matupu ni BURE, kuingiziwa Millioni moja na laki saba ndizo zisaidie kuvuruga Katiba!!!Lete Data kamili unaweza ukatushawishi. Harafu serikali iko wapi? Polisi wako wapi? Usalama wa Taifa wako wapi? DHAIFU!!!
 
kadanganye wa kwenu

Akadanganye wa kwao wapi kwani hata wanamtambua?.Kama nilivyosema bado hawa wazee wanadhani wanaweza kufikiri kwa niaba ya vijana ambao ni asilimia 65 ya wananchi wa taifa hili.Wanajidanganya wanaoelewa taratibu za benki kuu kuruhusu fedha za nje kuingizwa nchini tena kwenye akaunti ya mtu ni wao tu.Aelezwe siku hizi kuna mitandao na teknologia ya kisasa kila kitu kiko wazi kwa yeyote kujua sio wakati wao wa typewritter,simu za kuzungusha na landrover za kuwasha kwa hendeli. Hii ndio taarifa kwa umma baada ya siku saba kumalizika? Tunachotaka ni katiba itakayokubalika na wengi na si taarifa za nani kapokea nini. Kwani umoja wao ulipewa na madaraka ya vyombo kama usalalma wa taifa na benki kuu?Kwa hiyo tutegemee raisi atakapokutana na wapinzani atahoji na hilo la kupokea fedha? Yeye Matafu atakuwepo ikulu atoe ufafanuzi wa hilo?
 
Mwenyekiti wa Tanzania Kwanza ambao ni umoja wa muungano wa vyama saba vya siasa ikiwamo CCM katika bunge maalum la katiba Ndugu.Agustino Matefu amesema leo kuwa UKAWA inatumiwa ili kuleta machafuko na kuvuruga amani ya nchi.

Mwenyekiti huyo ameeleza hayo katika mohojiano kama mgeni katika kituo cha matangazo cha UHURU Fm.Matefu amesema kuwa nchi za uholanzi na Omani zimekuwa zikitumika kufadhili shughuli mbalimbali za UKAWA kwa kutoka pesa ambazo zimekuwa zukiingizwa katika akaunti binafsi za viongozi wa umoja huo.

Amesema kuwa Mbowe na Slaa mpaka sasa kupitia akaunti zao binafsi wameshapokea kiasi cha Sh.1,700,000(Awamu ya kwanza) huku awamu ya pili na tatu jumla ikiwa ni Dola 850,000/=kutoka Uholanzi.Wakati kwa upande wa CUF Prof.Ibrahim Lipumba kupitia akaunti yake binafsi amepokea kiasi cha dola 400,000/=kutoka Oman.

Ndugu Matefu ameeleza kuwa viongozi wa UKAWA wanatumika kama kijiko kwa manufaa ya watu wengine nje ya nchi kutaka kutuvuruga. Amesema kuwa Umoja huo hauna lengo zuri na nchi hii ndiyo maana pamoja na vikao vyote vyama usuluhishi bado wameendelea kuwa wagumu hawataki kumsikiliza yeyote.

Awali kabla ya hapo Ndugu Matefu kupitia umoja huyo alishazungumza na waandishi wa habari kuwaagiza Viongozi wa UKAWA ndani ya siku Saba wewe wamerudi Bungeni vinginevyo atamwaga Siri nzito zilizojificha nyuma ya Muungani humo.


Tanzania Kwanza ukiwa ni muungano wa vyama saba vya siasa katika Bunge la Katiba unajitambulisha kuwa ni umoja unaotetea maslahi ya nchi,kujali utaifa na kuangalia kwanza masuala muhimu ya kitaifa bila kujali tofauti zao kichama,kisera,kimtazamo na kiitikadi.

Huu ni uongo. Kwamba huyo anaefadhili ndo aliwaambia CCM wajadili Rasimu3 iliyosukwa kusikoeleweka. Muundo wq S2 haumo ndani ya Rasimu2 kama wangeamua kuukataa kwanza kwa kura za siri za kila mmoja
 
Mwambieni haya awaambie watu wenye IQ ndogo kama yake, hii habari siyo size yetu sisi wenye kujitambua, sisi tuna-deal na mambo makubwa na genuine kwa Taifa, sasa huu udhaifu wa serikali yanu na vyombo vya dola mnatueleza sisi tufanye nini?
 
Haya ndiyo matatizo ya kuishi Tanzania huku akili zako na fikra zako zikiwa zimeolewa na wazungu.Kwamba watanzania hawawezi kuwachangia UKAWA mpaka wachangiwe na wazungu?Kwamba watanzania hawawezi wakafanikiwa mpaka wasaidiwe na nchi za nje?Kwamba hakuna jambo jema linalo weza kufanywa na wananchi bila kusaidiwa na wazungu?Kwamba watanzania hawawezi kutumia haki yao ya kuandamana kwa ajili ya kupinga maovu yanayo fanywa na serekali iliyoko madarakani mpaka watumiwe na wazungu?.Kwamba watanzania wenyewe wamejiwekea haki ya kuandamana lakini hawawezi kuandamana mpaka watumiwe na wazungu?.Hii ina onyesha ni jinsi gani ambavyo viongozi wengi wa CCM walivyojaa uongo wa kuwadanganya wananchi kuwa hakuna jambo jema linalo weza kufanywa na wanao tofautiana nao kimtazamo pasipo kutumiwa na wazungu.Ndiyo maana nchi imekuwa na deni kubwa kwa sababu CCM walipo kuwa wanatekereza sera yao ya uwekezaji walijikuta wamewekeza na akili zao kwa wazungu,Wakati wanabinafsisha mashirika ya serekali kwa wazungu wakajikuta wamebinafsisha na akili zao kwa wazungu.Sasa kila kitu ni mzungu,mzungu,Haki ya kuandamana mzungu,UKAWA mzungu,Kuendesha nchi haiwezekani mpaka ukakope kwa mzungu.Hii ndiyo CCM ya wenyewe.
 
Back
Top Bottom