UKAWA wajipime, bila demokrasia wajiandae na maumivu makali

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Udhaifu mkubwa wa wana UKAWA ni kutowashirikisha wanachama wao na kutanguliza njia za mkato ambazo ndizo huzua migogoro isiyo na ukomo.

1) TEUZI ZOTE ZITOKANE NA MAONI YA WANACHAMA.

Mgogoro mkubwa uliojitokeza uchaguzi uliopita nafasi ya URAIS na kwa kiasi kidogo ubunge na udiwani ni kutowauliza wanachama wanataka nini. UKAWA walijipima bila ushahidi wowote wenye mashiko ni chama kipi kinakubalika bila ya kupiga kura za maoni za maeneo husika.

Matokeo yake Dr. Slaa na Prof. Lipumba na wafuasi wao hawakumuunga mkono Lowassa katika nafasi ya URAISI. Jibu lilikuwa ni kura ya maoni nchi nzima na ambaye angeshinda kura hizo za maoni za nafasi ya Urais angeliungwa mkono kwani hakuna utata.

Pia nafasi za ubunge na udiwani kama nafasi ya Urais walipaswa kupitishwa kwenye tanuru la UKAWA la kura ya maoni na atakayeibuka kidedea kuwakilisha UKAWA kupitia chama chake.

Vurugu nyingi zilizojitokeza katika kambi ya UKAWA na migogoro mingi ambayo iliacha makovu leo ingelikuwa haipo.

USHAURI.

UKAWA wajifunze juu ya umuhimu wa demokrasia kama silaha muhimu ya uteuzi. Hata hizi nafasi za EALA zimekumbwa na malalamiko kwa sababu ni maamuzi ya wachache tu.
 
Udhaifu mkubwa wa wana UKAWA ni kutowashirikisha wanachama wao na kutanguliza njia za mkato ambazo ndizo huzua migogoro isiyo na ukomo.

1) TEUZI ZOTE ZITOKANE NA MAONI YA WANACHAMA.

Mgogoro mkubwa uliojitokeza uchaguzi uliopita nafasi ya URAIS na kwa kiasi kidogo ubunge na udiwani ni kutowauliza wanachama wanataka nini. UKAWA walijipima bila ushahidi wowote wenye mashiko ni chama kipi kinakubalika bila ya kupiga kura za maoni za maeneo husika.

Matokeo yake Dr. Slaa na Prof. Lipumba na wafuasi wao hawakumuunga mkono Lowassa katika nafasi ya URAISI. Jibu lilikuwa ni kura ya maoni nchi nzima na ambaye angeshinda kura hizo za maoni za nafasi ya Urais angeliungwa mkono kwani hakuna utata.

Pia nafasi za ubunge na udiwani kama nafasi ya Urais walipaswa kupitishwa kwenye tanuru la UKAWA la kura ya maoni na atakayeibuka kidedea kuwakilisha UKAWA kupitia chama chake.

Vurugu nyingi zilizojitokeza katika kambi ya UKAWA na migogoro mingi ambayo iliacha makovu leo ingelikuwa haipo.

USHAURI.

UKAWA wajifunze juu ya umuhimu wa demokrasia kama silaha muhimu ya uteuzi. Hata hizi nafasi za EALA zimekumbwa na malalamiko kwa sababu ni maamuzi ya wachache tu.


Tundu Lisu ni mzigo chadema, huyu ndiye anayekwenda kuizika chadema, wengi wanamlaumu Mbowe lkn Tundu ndiye anayeimaliza chadema, hata ujio wa Lowasa yeye ndiye aliyeratibu, Tundu anawadharau wana chadema na anaamini kabisa anaweza kufanya chochote, kuwaambia chochote na kesho akaja kukitetea na kwamba watamuamini na ndicho kinachotokea, ukiangalia hili swala la Ubunge wa AM ni ujeuri tu kwamba watanifanya nini kwa maana kanuni ziko wazi kwa kila mtu kuzisoma lkn bado wamezipuuzia, sasa huu siyo mwisho bali ni muendelezo tu wa Tundu Lisu kuibomoa chadema!
 
Tundu Lisu ni mzigo chadema, huyu ndiye anayekwenda kuizika chadema, wengi wanamlaumu Mbowe lkn Tundu ndiye anayeimaliza chadema, hata ujio wa Lowasa yeye ndiye aliyeratibu, Tundu anawadharau wana chadema na anaamini kabisa anaweza kufanya chochote, kuwaambia chochote na kesho akaja kukitetea na kwamba watanuamini na ndicho kinachotokea!
Yaelekea Tundu Lissu anawanyima usingizi eeh? Akipata kikohozi nyie ndio mtakuwa hamlali maana kila akikohoa mnashtuka
 
_Kweli Wanaccm ni janga, yaani akina Fancy na Happiness ni bora kuliko Wenje na Masha kwenye masuala ya kimataifa hususani Jumuiya ya Afrika Mashariki?_
_Tutegemee bajeti mbobu kuliko ya mwaka jana_
 
Udhaifu mkubwa wa wana UKAWA ni kutowashirikisha wanachama wao na kutanguliza njia za mkato ambazo ndizo huzua migogoro isiyo na ukomo.

1) TEUZI ZOTE ZITOKANE NA MAONI YA WANACHAMA.

Mgogoro mkubwa uliojitokeza uchaguzi uliopita nafasi ya URAIS na kwa kiasi kidogo ubunge na udiwani ni kutowauliza wanachama wanataka nini. UKAWA walijipima bila ushahidi wowote wenye mashiko ni chama kipi kinakubalika bila ya kupiga kura za maoni za maeneo husika.

Matokeo yake Dr. Slaa na Prof. Lipumba na wafuasi wao hawakumuunga mkono Lowassa katika nafasi ya URAISI. Jibu lilikuwa ni kura ya maoni nchi nzima na ambaye angeshinda kura hizo za maoni za nafasi ya Urais angeliungwa mkono kwani hakuna utata.

Pia nafasi za ubunge na udiwani kama nafasi ya Urais walipaswa kupitishwa kwenye tanuru la UKAWA la kura ya maoni na atakayeibuka kidedea kuwakilisha UKAWA kupitia chama chake.

Vurugu nyingi zilizojitokeza katika kambi ya UKAWA na migogoro mingi ambayo iliacha makovu leo ingelikuwa haipo.

USHAURI.

UKAWA wajifunze juu ya umuhimu wa demokrasia kama silaha muhimu ya uteuzi. Hata hizi nafasi za EALA zimekumbwa na malalamiko kwa sababu ni maamuzi ya wachache tu.
Mkuu mimi naona Chadema bado hakijawa strong enough kutoa vyeo hovyo kama wafanyavyo CCM mpaka vinuka mkojo wanapewa ubunge.
Hii ni vita kati ya CCM na Chadema. Watu makini na strong ni tishio kwenye serikali ya CCM. Lazima chadema iimarike ndio itaweza kuangusha mbuyu. Ujio wa lowassa chadema haukuwa wa Bahati mbaya na nadhani muziki uliuona. Chama kipo kimkakati zaidi mkuu tuvumilie mbona vyeo vipo .
 
Tundu Lisu ni mzigo chadema, huyu ndiye anayekwenda kuizika chadema, wengi wanamlaumu Mbowe lkn Tundu ndiye anayeimaliza chadema, hata ujio wa Lowasa yeye ndiye aliyeratibu, Tundu anawadharau wana chadema na anaamini kabisa anaweza kufanya chochote, kuwaambia chochote na kesho akaja kukitetea na kwamba watamuamini na ndicho kinachotokea, ukiangalia hili swala la Ubunge wa AM ni ujeuri tu kwamba watanifanya nini kwa maana kanuni ziko wazi kwa kila mtu kuzisoma lkn bado wamezipuuzia, sasa huu siyo mwisho bali ni muendelezo tu wa Tundu Lisu kuibomoa chadema!
Usimlaumu sana Tundu Lisu bali kuanzia Mwenyekiti wao na kamati kuu, mm nimekuwa nikijiuliza kila siku hawa upinzan ambao hujisifia kujua sheria vzr tena wakiwa na wanasheria mahiri ni kwa nn wao badala ya kuwa mfan ili cc wapenda mabadiliko tuwaunge mkono lakini matokeo yake wao ndio wa kwanza kuisigina demokrasia. Viongozi wao mbali×2 huteuliwa bila kura ama hupitishwa jina moja na wagombea wengine kukatwa majina bila sababu ili tu wale waliyemteua apitishwe bila kupingwa..kama wataendelea na utaratibu wao wa kuwekana kwa kubebana bila kuzingatia uchaguzi na haki sawa kwa wanachama wote bac ndoto zao za kudhan wataing'oa ccm wasahau

Wanatumia kigezo cha eti wananchi wana hali ngumu wameichoka serikali hivyo watatwaa madaraka 2020 but I'm sure hata iwe 2040 kama hawataacha kusigina democrasia na kuyaishi wanayoyahubiri itabaki ndoto kwao.

Kiuhalisia wananchi wengi hawapendezwi na utendaji kazi wa serikali hususan ktk issue nzima ya uchumi ila ni nano atakuwa mbadala?, hapo ndipo wanapoona hakuna mbadala ni bora iendelee ccm maana nanaohubiri wanataka democracy wao wenyewe hawaitekelezi kwa vitendo, wanaohubiri wanauchukia ufisadi akifukuzwa fisadi wao humchukua na kumsafisha , wanaolalamika hatua hazichukuliwi dhidi ya wabadhilifu ni wao ila hatua zikichukuliwa wanarudi kuwatetea eti wanaonewa HII NI AIBU. hata kama asiyeenda shule hawezi kuwaamini watu wana calibre hii.
 
_Kweli Wanaccm ni janga, yaani akina Fancy na Happiness ni bora kuliko Wenje na Masha kwenye masuala ya kimataifa hususani Jumuiya ya Afrika Mashariki?_
_Tutegemee bajeti mbobu kuliko ya mwaka jana_
Hakuna aliesema hao hawafai, ila hamkuwapa wapiga kura uwanja mpana zaidi kuchagua...CUF walikuwa na nafasi moja lakini walipeleka wagombea wanne.

Nyie nafasi Mbili halafu mnapeleka mbili hizo hizo.....Kwa hiyo mnawachagulia CCM watu wa kuwapigia kura.

Halafu nafasi ya jinsia, hata Magufuli mwenyewe hakutaka kabisa kubalansi nafasi za wabunge kwenye viti maalum lakini katiba ilimbana ikabidi atengue baadhi wateule ili kukidhi matakwa ya katiba.

Hata CCM kupeleka wanawake sio kama wamependa sana ila kanuni imewabana..... Chadema lazima Mwanamke mmoja ateuliwa ili kuchangia 1/ 3 ya wabunge wote tisa....

La sivyo hamtoboi...!
 
Mkuu mimi naona Chadema bado hakijawa strong enough kutoa vyeo hovyo kama wafanyavyo CCM mpaka vinuka mkojo wanapewa ubunge.
Hii ni vita kati ya CCM na Chadema. Watu makini na strong ni tishio kwenye serikali ya CCM. Lazima chadema iimarike ndio itaweza kuangusha mbuyu. Ujio wa lowassa chadema haukuwa wa Bahati mbaya na nadhani muziki uliuona. Chama kipo kimkakati zaidi mkuu tuvumilie mbona vyeo vipo .
Kwa hiyo ndani ya Chadema Wenye sifa ni Masha na Wenje tu wengine wote vinuka mkojo.?

Au nimekunukuu vibaya Mkuu.!
 
Tatizo watu mnakariri wanachofanya ccm na wapinzani wafanye...chadema wamesema fomu ziltolewa wakachukua watu 17 kura zinapigwa wakapata wawili na ndio nafasi zao mbili..mlitaka wapeleke majina mengi ili ccm wawachagulie?
 
Tundu Lisu ni mzigo chadema, huyu ndiye anayekwenda kuizika chadema, wengi wanamlaumu Mbowe lkn Tundu ndiye anayeimaliza chadema, hata ujio wa Lowasa yeye ndiye aliyeratibu, Tundu anawadharau wana chadema na anaamini kabisa anaweza kufanya chochote, kuwaambia chochote na kesho akaja kukitetea na kwamba watamuamini na ndicho kinachotokea, ukiangalia hili swala la Ubunge wa AM ni ujeuri tu kwamba watanifanya nini kwa maana kanuni ziko wazi kwa kila mtu kuzisoma lkn bado wamezipuuzia, sasa huu siyo mwisho bali ni muendelezo tu wa Tundu Lisu kuibomoa chadema!
Unapenda sana kumtaja tundu lisu wewe..ulimuomba akakunyima? Mana kuuuuchwaaa..ukiwa faragha na mmeo vp unamtajaga pia?
 
Tundu Lisu ni mzigo chadema, huyu ndiye anayekwenda kuizika chadema, wengi wanamlaumu Mbowe lkn Tundu ndiye anayeimaliza chadema, hata ujio wa Lowasa yeye ndiye aliyeratibu, Tundu anawadharau wana chadema na anaamini kabisa anaweza kufanya chochote, kuwaambia chochote na kesho akaja kukitetea na kwamba watamuamini na ndicho kinachotokea, ukiangalia hili swala la Ubunge wa AM ni ujeuri tu kwamba watanifanya nini kwa maana kanuni ziko wazi kwa kila mtu kuzisoma lkn bado wamezipuuzia, sasa huu siyo mwisho bali ni muendelezo tu wa Tundu Lisu kuibomoa chadema!
Udikteta utawamaliza chama ni cha wanachama siyo kikundi cha watu
 
Back
Top Bottom