VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Jana,mjini Dodoma,kilifanyika kikao cha Kamati Kuu ya CCM (CC ya CCM) chini ya Uenyekiti wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ndiye Mwenyekiti wa Taifa wa CCM. Mkutano huo,kwa mujibu wa mtoa taarifa aliyekuwepo ndani ya kikao hicho,ulipokea Taarifa Rasmi ya Ziara zilizofanywa na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdurahman Kinana na timu yake katika mikoa mbalimbali hapa nchini.
Pia,kikao hicho kilipokea Mapendekezo ya Kamati Maalum ya Wataalamu waliopewa kazi ya kushauri cha kufanya katika hali ya sasa ya kisiasa nchini hasa katika suala la Katiba mpya. Taarifa zote mbili zliwasilishwa kikaoni na Katibu Mkuu wa CCM. Hatahivyo,kulikuwa na mambo mbalimbali mengineyo kama utendaji wa UVCCM,Umoja wa Wazazi,Umoja wa Wanawake na Idara mbalimbali za kichama na masula ya kifedha.
Katika kikao hicho kilichoisha usiku 'mnene',Umoja wa Ktiba ya Wananchi almaarufu kama UKAWA uliteka kikao hicho. " Ajenda zote zilimezwa na kujadili kuhusu UKAWA na jinsi ya kufanya mambo ya Katiba mpya yaliyokwama yasonge mbele|" alisema mmoja wa Wajumbe wa CC anayetokea Tanzania Bara. "Majadiliano yalikuwa moto sana.Mwisho wa yote, CC imetoa maagizo kwa Sekretarieti namna ya kukwamua suala la Katiba" aliongeza Mjumbe huyo bila ya kutaja maagizo yaliyotolewa.
Kuna kila dalili,CCM kuachana na msimamo wake wa Serikali mbili ili kusonga mbele kama Taifa katika kuimarisha Muungano kwa kuwa na Serikali tatu.
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Pia,kikao hicho kilipokea Mapendekezo ya Kamati Maalum ya Wataalamu waliopewa kazi ya kushauri cha kufanya katika hali ya sasa ya kisiasa nchini hasa katika suala la Katiba mpya. Taarifa zote mbili zliwasilishwa kikaoni na Katibu Mkuu wa CCM. Hatahivyo,kulikuwa na mambo mbalimbali mengineyo kama utendaji wa UVCCM,Umoja wa Wazazi,Umoja wa Wanawake na Idara mbalimbali za kichama na masula ya kifedha.
Katika kikao hicho kilichoisha usiku 'mnene',Umoja wa Ktiba ya Wananchi almaarufu kama UKAWA uliteka kikao hicho. " Ajenda zote zilimezwa na kujadili kuhusu UKAWA na jinsi ya kufanya mambo ya Katiba mpya yaliyokwama yasonge mbele|" alisema mmoja wa Wajumbe wa CC anayetokea Tanzania Bara. "Majadiliano yalikuwa moto sana.Mwisho wa yote, CC imetoa maagizo kwa Sekretarieti namna ya kukwamua suala la Katiba" aliongeza Mjumbe huyo bila ya kutaja maagizo yaliyotolewa.
Kuna kila dalili,CCM kuachana na msimamo wake wa Serikali mbili ili kusonga mbele kama Taifa katika kuimarisha Muungano kwa kuwa na Serikali tatu.
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam