UKAWA waiteka CC ya CCM

UKAWA waiteka CC ya CCM

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Jana,mjini Dodoma,kilifanyika kikao cha Kamati Kuu ya CCM (CC ya CCM) chini ya Uenyekiti wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ndiye Mwenyekiti wa Taifa wa CCM. Mkutano huo,kwa mujibu wa mtoa taarifa aliyekuwepo ndani ya kikao hicho,ulipokea Taarifa Rasmi ya Ziara zilizofanywa na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdurahman Kinana na timu yake katika mikoa mbalimbali hapa nchini.

Pia,kikao hicho kilipokea Mapendekezo ya Kamati Maalum ya Wataalamu waliopewa kazi ya kushauri cha kufanya katika hali ya sasa ya kisiasa nchini hasa katika suala la Katiba mpya. Taarifa zote mbili zliwasilishwa kikaoni na Katibu Mkuu wa CCM. Hatahivyo,kulikuwa na mambo mbalimbali mengineyo kama utendaji wa UVCCM,Umoja wa Wazazi,Umoja wa Wanawake na Idara mbalimbali za kichama na masula ya kifedha.

Katika kikao hicho kilichoisha usiku 'mnene',Umoja wa Ktiba ya Wananchi almaarufu kama UKAWA uliteka kikao hicho. " Ajenda zote zilimezwa na kujadili kuhusu UKAWA na jinsi ya kufanya mambo ya Katiba mpya yaliyokwama yasonge mbele|" alisema mmoja wa Wajumbe wa CC anayetokea Tanzania Bara. "Majadiliano yalikuwa moto sana.Mwisho wa yote, CC imetoa maagizo kwa Sekretarieti namna ya kukwamua suala la Katiba" aliongeza Mjumbe huyo bila ya kutaja maagizo yaliyotolewa.

Kuna kila dalili,CCM kuachana na msimamo wake wa Serikali mbili ili kusonga mbele kama Taifa katika kuimarisha Muungano kwa kuwa na Serikali tatu.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

 
Labda sio ccm unayoijua mzee tupatupa!
 
CCM hiyo hiyo inajua kima cha chini ni shs 270,000 na bado inaamua kulipa kundi fulani posho ya 300k. Kawaida ya mawazo ya ccm ni upside down.
 
...Kuna kila dalili,CCM kuachana na msimamo wake wa Serikali mbili ili kusonga mbele kama Taifa katika kuimarisha Muungano kwa kuwa na Serikali tatu.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam


CCM wamekwisha sema kuachana na msimamo wa serikali mbili ni ndoto, wako tayari waingie msituni...kuisambaratisha nchi.
 
"Kuna kila dalili,CCM kuachana na msimamo wake wa Serikali mbili ili kusonga mbele kama Taifa katika kuimarisha Muungano kwa kuwa na Serikali tatu. "
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Kwa CCM tunayoijua hilo litakuwa jambo la mwisho kufanya kabla hawajafa; kwa bahati mbaya kwa CCM issue sio maslahi ya taifa bali their own political and socio economic survival; hata kidogo sio kwa composition ya uongozi wa CCM ulioko madarakani kwa sasa; No sir thank you.
 
kwa ccm haitawezekana kupindua mawazo yao labda @nape domo kaya asiwe kiongozi wa hiko chama
 
Huu utakuwa muujiza shetan kuwa na mawazo ya kutenda mema ccm kukubal maon ya wananchi.
 
Jana,mjini Dodoma,kilifanyika kikao cha Kamati Kuu ya CCM (CC ya CCM) chini ya Uenyekiti wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ndiye Mwenyekiti wa Taifa wa CCM. Mkutano huo,kwa mujibu wa mtoa taarifa aliyekuwepo ndani ya kikao hicho,ulipokea Taarifa Rasmi ya Ziara zilizofanywa na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdurahman Kinana na timu yake katika mikoa mbalimbali hapa nchini.

Pia,kikao hicho kilipokea Mapendekezo ya Kamati Maalum ya Wataalamu waliopewa kazi ya kushauri cha kufanya katika hali ya sasa ya kisiasa nchini hasa katika suala la Katiba mpya. Taarifa zote mbili zliwasilishwa kikaoni na Katibu Mkuu wa CCM. Hatahivyo,kulikuwa na mambo mbalimbali mengineyo kama utendaji wa UVCCM,Umoja wa Wazazi,Umoja wa Wanawake na Idara mbalimbali za kichama na masula ya kifedha.

Katika kikao hicho kilichoisha usiku 'mnene',Umoja wa Ktiba ya Wananchi almaarufu kama UKAWA uliteka kikao hicho. " Ajenda zote zilimezwa na kujadili kuhusu UKAWA na jinsi ya kufanya mambo ya Katiba mpya yaliyokwama yasonge mbele|" alisema mmoja wa Wajumbe wa CC anayetokea Tanzania Bara. "Majadiliano yalikuwa moto sana.Mwisho wa yote, CC imetoa maagizo kwa Sekretarieti namna ya kukwamua suala la Katiba" aliongeza Mjumbe huyo bila ya kutaja maagizo yaliyotolewa.

Kuna kila dalili,CCM kuachana na msimamo wake wa Serikali mbili ili kusonga mbele kama Taifa katika kuimarisha Muungano kwa kuwa na Serikali tatu.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam


Tusubiri tuone. Lakini kwa ninavyojua mimi (out of uzoefu wa siasa za CCM) kinachofuatia ni kukimbilia kubadilisha sheria ya katiba hasa vipengele vya kura kupitisha katiba kutoka theluthi mbili TZ bara na TZ visiwani kuwa madudu mengine wanayotaka wao.

Kaeni muangalie kwenye bunge hili la bajeti!
 
Wenye nchi ndio wanajua uchungu wa nchi hii na hasa Watanganyika. Taratibu wataeleweka na kuendelea na maisha yao kwenye nchi yao adhimu. Hakuna cha kupoteza kwenye Muungano huu. Maoni ya wananchi kama yalivyokusanywa na Jaji Warioba ndio litakuwa suluhisho la mwisho hakika kazi hiyo adhimu haiwezi kwisha kienyeji hata kidogo
 
Ccm chama cha kicha machambaz hawa ni majambazi na wahun wa hii nchi kwanza lichama hili halina usajili wa kudumu,
Mtu yeyote alioko ccm hana akil na wote majambaz kwl
 
ccm haijawahi kubadili msimamo hata uwe wa hovyo kiasi gani, watakuwa tayari katiba isiandikwe lakini si kubadili msimamo
 
Yetu macho tu.

CCM ni janga kwetu na maaendeleo ya vizazi vyetu walalahoi lakini kwa mafisadi ni neema.


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!!!!
 
Tusubiri tuone. Lakini kwa ninavyojua mimi (out of uzoefu wa siasa za CCM) kinachofuatia ni kukimbilia kubadilisha sheria ya katiba hasa vipengele vya kura kupitisha katiba kutoka theluthi mbili TZ bara na TZ visiwani kuwa madudu mengine wanayotaka wao.

Kaeni muangalie kwenye bunge hili la bajeti!

Mhe kwa utaratibu duniani kote kwa maamuzi makubwa mfano uundwaji wa katiba inatakiwa 2/3 na nchi zingine kama marekani wamefikia 3/4, wakisema simple majority itakuwa ni muendelezo wa maajabu tanzania!!ila kwa ccm siwezi kuwashangaa walishafika ukomo wa kufikiri.
 
Kwa vyovyote vile ccm imekwama, hata walete mfumo gani, Tanzania ya sasa siyo ya 64 saivi ni mapambano tu huko wanakoelekea watajutia tu hali ya chama chao itakuwa mbaya sn
 
Sioni wenye busara hiyo ndani ya ccm!, matusi yote yale kwa tume ni jitihada za kuipindua rasimu. Hawatarudi nyuma wenye hekima na busara ndo wanaotukanwa!
 
Kwa ccm maslahi ya taifa baadae, kwao ni chama kwanza! Katiba mpya haiwezi kupatikana kwa sababu ccm imeteka mchakato mzima!
 
Back
Top Bottom