tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,994
- 25,387
Ipo haja ya UKAWA kuanzisha vyombo vyake vya habari vitakavyosaidia kunadi na kutangaza sera zao ili kuendana na kasi ya CCM wenye vyombo lukuki vinavyowasaidia kunadi sera zao kama vile TBC1, TBC Radio, TBC FM na Radio Uhuru. Lakini pia wana magazeti lukuki yanayosaidia kuwanadi kama vile Habari Leo, Jambo Leo, Uhuru, Mzalendo, Daily News, Majira na vipeperushi vingi tu.
Kwa utitiri huu wa vyombo vya habari vinavyonadi sera za CCM huku vikijitahidi kuficha habari mbaya za chama hicho na serikali yake, ipo haja ya UKAWA nao kuanzisha vyombo vya habari vitakavyosaidia kunadi sera na habari zao. Unajua chama kikisemwa sana...kila siku watu wakilala wakiamka wanaamkia habari ztinazohusu chama kimoja tu, itajenga taswira mbaya miongoni mwa wananchi kwamba ndicho chama chenye sera nzuri.
Ni sawa na kuwa na bidhaa nzuri inayofichwa halafu kukawa na bidhaa mbovu na feki inayotangazwa kila siku...watu watanunua bidhaa hiyo hiyo mbovu kwa kuwa hawana habari juu ya bidhaa bora wasiyojua kama ipo sokoni.
:israel:
Kwa utitiri huu wa vyombo vya habari vinavyonadi sera za CCM huku vikijitahidi kuficha habari mbaya za chama hicho na serikali yake, ipo haja ya UKAWA nao kuanzisha vyombo vya habari vitakavyosaidia kunadi sera na habari zao. Unajua chama kikisemwa sana...kila siku watu wakilala wakiamka wanaamkia habari ztinazohusu chama kimoja tu, itajenga taswira mbaya miongoni mwa wananchi kwamba ndicho chama chenye sera nzuri.
Ni sawa na kuwa na bidhaa nzuri inayofichwa halafu kukawa na bidhaa mbovu na feki inayotangazwa kila siku...watu watanunua bidhaa hiyo hiyo mbovu kwa kuwa hawana habari juu ya bidhaa bora wasiyojua kama ipo sokoni.
:israel: