UKAWA, Vijana kama Joel Nanauka mgombea wa CHADEMA Mtwara Mjini ni potential sana

UKAWA, Vijana kama Joel Nanauka mgombea wa CHADEMA Mtwara Mjini ni potential sana

activisty

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
315
Reaction score
107
Habari zenu wakuu wanajf,natumai mnaendelea vizuri na shughuli zenu za kila siku.Nimeuleta huu uzi ili nitoe japo ushauri kwa vyama vinavyounda UKAWA.

Mnamo tarehe 25 june,siku 4 tu zilizopita nilibahatika ufika jimbo la Mtwara Mjini,hapo nilikutana na shamrashamra za watia nia wa ubunge CHADEMA wakirudisha fomu zao.

Katika pitapita Zangu za hapa na pale nililisikia sana jina la Joel Nanauka, nikavutiwa kulifuatilia.Huyu ni kijana ambaye ana nguvu kubwa,yenye ushawishi kisiasa.Mwaka 2010 alishiriki kura za maoni ndani ya CCM ambapo walimpiga chini sababu hakuwa na fedha,jambo hili inasemekana liliwakera watu wengi sana.

Nilifanikiwa kusoma CV yake kutoka kwenye moja kati ya vipeperushi vyake,nilifurahi kuona amewahi kuwa tanzania one na kazi alizozifanya ni mtu aliyepikwa kwelikweli.

Watu wa UKAWA mliopo Mtwara Mjini nina hakika hamtafanya makosa,huyu kijana akipeperusha bendera ya UKAWA mtapata kura za vyama vyote na za wananchi wote wasiokuwa wanachama wa vyama vya siasa ambao kwa hakika idadi yao ni kubwa zaidi.

Licha ya propaganda nilizozisikia juu yake bado kwa nguvu ile ya yeye kuongelewa na watu mbalimbali,bado nashawishika huyu kijana akisimama mtwara mjini atashinda kwa kishindo.

Nilijaribu kufuatilia kuhusu mgombea wa CUF pia anaitwa bwana MUFTAA huyu jamaa kwa taarifa nilizozipata hajiamini sababu tayari wanachama wa CUF wamegawanyika baada ya bwana MATATA ambaye wanachama wa CUF wengi waliokuwa wanamtaka kutopitishwa kama mgombea kupitia CUF.

Nawasihi sana watu wa UKAWA wapime nguvu ya mgombea ili kuhakikisha jimbo la mtwara mjini halirudi mikononi mwa CCM.

Wengne waliotajwa katika kurudisha fomu hizo ni mwenyekiti wa chadema wilaya ya mtwara mjin bwana IBRAHIM MANDOA ambaye anaonekana anayo nguvu ndani ya chama japo watu waliokuwa wanamuunga mkono baada ya kuja JOEL NANAUKA wamemuhama kwa kusema kuwa japo kakitumikia sana chama mtwara mjin lakini hatauzika kwa wananchi ukilinganisha na JOEL.

Nilijaribu kuongea na viongozi wawili wa CHADEMA jimboni Mtwara ambapo wote kwa pamoja walisema wameona ujio wa Joel kama neema ya CHADEMA kushinda kwa kishindo Mtwara Mjini.

Pia yupo bwana MOHAMED HANGA aliyewahi kuwa mkurugenzi wa bodi ya korosho,huyu nasikia alikuwa na ushawishi mwanzoni ila baada ya ujio wa Nanauka na yeye amefifia kabsa..na mwingine ni bwana Mulukozi ambaye na yeye aliwahi kugombea ubunge kupitia chama hicho 2005 ila kwa sasa hana nguvu tena.

Kwa upande wa ubunge viti maalumu yupo binti anaitwa Anne Deo,huyu kwa nilivyofuatilia ni kamanda wa muda mrefu wa chadema ni kati ya wale walioibua vuguvugu za chadema vyuo vikuu...kwa chadema kuwa na binti mdogo kama yule wa kupaza sauti kusini ni jambo la kheri sana.

Huyu jamaa anayeitwa NANAUKA sikubahatika kumuona face to face,ila natamani siku moja nionane naye,nasisitiza sana kama ukawa mnataka kushinda mtwara mjini na majimbo mengine,vijana aina ya joel ni muhimu sana.
 
Nini kimemfanya mpaka Joel akahama CCM na kuhamia Chadema ?
 
Yaani UKAWA wakileta wagombea wenye ushawishi...ccm kwishaaaa...kwa kuwa nina rafiki zangu kibao mtwara town ngoja nianze mfatilia bwana JOEL NANAUKA ntaleta mrejesho
 
ukawa wakituliza vichwa vyao vizuri watajaza wabunge wengi sana bungeni. wasikubali kugawanyika lengo liwe kuitoa ccm kwanza...
 
Nini kimemfanya mpaka Joel akahama CCM na kuhamia Chadema ?

Kwa maelezo niliyopewa,baada ya kijana kutotendewa haki kwenye kura za maoni ndani ya CCM,alianza kuiona dhuluma ndani ya chama hicho..kipindi cha vurugu za gesi akisimama kidete kuwatetea watu wa mtwara..hapa ndo alizid kujenga uadui mkubwa na CCM na hata kuhatarisha maisha yake.Nadhani ni jambo jema kwa yeye kuhamia chama makini kama chadema maana ata mwalimu nyerere alisema watanzania wakiyakosa mabadiliko ndani ya ccm watayatafuta nje ya ccm.
 
ukawa wakituliza vichwa vyao vizuri watajaza wabunge wengi sana bungeni. wasikubali kugawanyika lengo liwe kuitoa ccm kwanza...
Kabisa kabsa kiongozi,ni vyema waweke lengo kuu mbele,wakifanya hivyo watafanya maamuzi sahihi.sana
 
Yaani UKAWA wakileta wagombea wenye ushawishi...ccm kwishaaaa...kwa kuwa nina rafiki zangu kibao mtwara town ngoja nianze mfatilia bwana JOEL NANAUKA ntaleta mrejesho

Binafsi hiyu kijana nimemfahamu tokea akiwa kibaha sec...ni kijana aliye na hofu sana na Mungu.Ana uwezo mkubwa naamini ni rahisi kumuuza kwa wananchi...tukiwa kibaha alinitangulia darasa moja...he was bright kwa kweli.
 
Yaani UKAWA wakileta wagombea wenye ushawishi...ccm kwishaaaa...kwa kuwa nina rafiki zangu kibao mtwara town ngoja nianze mfatilia bwana JOEL NANAUKA ntaleta mrejesho

Joel na mjua kiasi hila ni intellegent sana jamaa amesoma shule ya msingi shangan primary pale alinitangulia alikua darasa moja bro wangu,kiufupi jamaa anakubalika mtwara pia n mtu wa maadili na msimamo.joel he deserve to represent mtwara go go go brother.
 
Nini kimemfanya mpaka Joel akahama CCM na kuhamia Chadema ?


Baada ya Joel Nanauka kuanza kufuatilia ishu za gesi na kutoa hotuba kali iliyowafungua macho wananchi na akieleza jinsi ambavyo mradi wa gesi ulivyokuwa unakiuka mipango iliyokuwa kabla ya nchi yetu wananchi walimwelewa na ndipo walipoanza kumsapoti kwa nguvu zote.Hapo ndipo CCM walipoanza kumsakama na kuanza kutishia maisha yake na wazazi wake.Kuanzia hapo alitangaza kuondoka CCM na baadaye ndipo alijiunga na chadema 2014.Ukweli ni kwamba engine ya vuguvugu la gesi Mtwara ilikuwa ni yeye.

Hotuba yake inapatikana hapa.

GAS SPEECH - SoundCloud - Listen to GAS SPEECH by Joel Nanauka 1 #np on #SoundCloud
https://soundcloud.com/joel-nanauka-1/gas-speech
 
Kijana Joel Nanauka ni.mzaliwa wa mtwara,alimaliza kidato cha sita kibaha sec..Amesoma masomo ya uongozi na biashara chuo kikuu cha dar es salaam na kuwa mbunge wa kitivo cha uongozi na biashara chuoni hapo.
Mwaka 2012 aliliwakilisha taifa katika mkutano wa viongozi vijana nchini china ambapo aliteuliwa kuwa kiongozi bora kwa vijana waliohudhuria ktk mkutano huo.
Ni mtaalamu wa diplomasia ya uchumi katika eneo la mahusiano ya nchi mbalimbali ktk kufanya biashara ya uwekezaji.

Amewah kupewa tuzo mbalimbali za mafanikio katika elimu zikiwemo tuzo kutoka wizara ya elimu,tume ya sayansi na teknolojia,stanbinc na coca cola.

Joel Nanauka amekuwa na mchango mkubwa katika jamii ya wana mtwara tangu akiwa mwanafunzi alijishughulisha kuchangia kidogo alichonacho kwa wanafunzi wasiojiweza na kuwalipia ada wanafunzi mia moja 100,Amehusika katika utoaji mada mbalimbali katika makongamano ya kitaifa na kimataifa yaliyoandaliwa na taasisi mbalimbali nchini Na nje ya nchi.

Alitoa ushauri mbalimbali wa kitaalamu wa fedha kwa vikundi mbalimbali na kuwaunganisha kwa fursa alizoweza kuzipata.Na wakati wa gesi alikuwa pamoja sana na watu wa mtwara kwa kutoa hotuba ya kizalendo ambayo ililenga kusimamia haki kwa wananchi wote.
 
Huyu joel nimesoma nae Kibaha. Sijui huyu mandoa ni yule ambae pia tumesoma pamoja kibaha. Muulize kuhusu ile campaign ya kugombea urais wa kibaha kati ya makene na yusuph. Joel alikuwa anavutiwa na siasa za upinzani za yusuph. Lakini makene alishinda kwa kishindo. Ila joel nilimsikia clouds kwenye uzi mmoja hapa jf juu ya elimu
 
Baada ya Joel Nanauka kuanza kufuatilia ishu za gesi na kutoa hotuba kali iliyowafungua macho wananchi na akieleza jinsi ambavyo mradi wa gesi ulivyokuwa unakiuka mipango iliyokuwa kabla ya nchi yetu wananchi walimwelewa na ndipo walipoanza kumsapoti kwa nguvu zote.Hapo ndipo CCM walipoanza kumsakama na kuanza kutishia maisha yake na wazazi wake.Kuanzia hapo alitangaza kuondoka CCM na baadaye ndipo alijiunga na chadema 2014.Ukweli ni kwamba engine ya vuguvugu la gesi Mtwara ilikuwa ni yeye.

Hotuba yake inapatikana hapa.

GAS SPEECH - SoundCloud - Listen to GAS SPEECH by Joel Nanauka 1 #np on #SoundCloud
https://soundcloud.com/joel-nanauka-1/gas-speech

Yuko vizuri nimemskiza but ngoja jamaa zangu wa mtwara wanipe full data
 
Huyu joel nimesoma nae Kibaha. Sijui huyu mandoa ni yule ambae pia tumesoma pamoja kibaha. Muulize kuhusu ile campaign ya kugombea urais wa kibaha kati ya makene na yusuph. Joel alikuwa anavutiwa na siasa za upinzani za yusuph. Lakini makene alishinda kwa kishindo. Ila joel nilimsikia clouds kwenye uzi mmoja hapa jf juu ya elimu

Mzee inatosha ,Mandoa unayemzungumzia sio huyo,sidhani kama anaweza jihusisha na mambo ya siasa
 
Namfahamu vizuri Joel Nanauka, ni kijana mwenye hofu ya Mungu, anao uwezo mkubwa sana kiakili(aliongoza kitaifa kwa ufaulu matokeo ya kidato cha nne mwaka 2002). Ana upeo mkubwa wa kupambanua mambo na kusimamia anachokiamini bila UNAFIKI, ni kijana ambae ni hazina kubwa kwa wana Mtwara na Taifa.
 
Namfahamu vizuri Joel Nanauka, ni kijana mwenye hofu ya Mungu, anao uwezo mkubwa sana kiakili(aliongoza kitaifa kwa ufaulu matokeo ya kidato cha nne mwaka 2002). Ana upeo mkubwa wa kupambanua mambo na kusimamia anachokiamini bila UNAFIKI, ni kijana ambae ni hazina kubwa kwa wana Mtwara na Taifa.

Jimbo la Mtwara wameachiwa CUF kwa hiyo Joel amwunge mkono ili Ukawa kwa ujumla wetu tuchukue nchi. Tuache tamaa. Umoja ni give and take.!
 
Jimbo la Mtwara wameachiwa CUF kwa hiyo Joel amwunge mkono ili Ukawa kwa ujumla wetu tuchukue nchi. Tuache tamaa. Umoja ni give and take.!

Hakuna aliegoma but vikao vya ukawa bado hajijakaa kupitisha mmoja ndio maana Kila chama kina watia nia wake....Acha kuchafua hali ya hewa...
 
Kwa maelezo niliyopewa,baada ya kijana kutotendewa haki kwenye kura za maoni ndani ya CCM,alianza kuiona dhuluma ndani ya chama hicho..kipindi cha vurugu za gesi akisimama kidete kuwatetea watu wa mtwara..hapa ndo alizid kujenga uadui mkubwa na CCM na hata kuhatarisha maisha yake.Nadhani ni jambo jema kwa yeye kuhamia chama makini kama chadema maana ata mwalimu nyerere alisema watanzania wakiyakosa mabadiliko ndani ya ccm watayatafuta nje ya ccm.

siasa tu hzo
 
Back
Top Bottom