Manjagata
JF-Expert Member
- Mar 7, 2012
- 16,549
- 18,673
Wakuu habari za Alasiri?
Kumeibuka wimbi la raia kutimka Magambani na kuja UKAWA, hapa namaanisha viongozi na wanachama wa kawaida. Sasa hivi ni kila kona ya nchi ninasikia mara waliokuwa madiwani wa ccm wahamia CHADEMA, mara wahamia CUF, mara wahamia NCCR. Kidogo unasikia mwenyekiti wa ccm mkoa fulani ahamia CHADEMA au abwaga manyanga, sasa najiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu lakini swali kubwa kabisa linalonisumbua "TUMEJIPANGAJE?". Haitakuja kutokea kwamba vyama vyetu vikawa ccm B?
Hawa jamaa tutawadhibiti vipi ili wafuate misingi ya vyama vyetu vinavyounda UKAWA? Je, hayatatokea kama ya Mbingu wa Mutharika kule Malawi kwamba baada ya kukorofishana na chama chake akatimka na watu wake na kwenda kuanzisha chama kingine (ingawa hapa kwetu sina uhakika kama sheria zinaruhusu hili).
Hayatatulazimisha kuvaa manguo ya kijani haya? Nawaomba viongozi wetu wa UKAWA wawe makini na hili isije ikawa akina Makongoro, Kimbisa, Mgana n.k. wamekimbilia kwetu ili tuwapitishe kugombea ubunge halafu wakifika bungeni waanze kutusumbua kama Shibuda na Lety!
Mwisho viongozi wetu wamwagize rais wetu mtarajiwa aanze sasa kuvaa gwanda ili tumtambue kwa mavazi!! Kwa mfano kesho anapoenda kuchukua fomu anatakiwa atinge ndani ya Gwanda ili magamba yapukutike!!
Kumeibuka wimbi la raia kutimka Magambani na kuja UKAWA, hapa namaanisha viongozi na wanachama wa kawaida. Sasa hivi ni kila kona ya nchi ninasikia mara waliokuwa madiwani wa ccm wahamia CHADEMA, mara wahamia CUF, mara wahamia NCCR. Kidogo unasikia mwenyekiti wa ccm mkoa fulani ahamia CHADEMA au abwaga manyanga, sasa najiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu lakini swali kubwa kabisa linalonisumbua "TUMEJIPANGAJE?". Haitakuja kutokea kwamba vyama vyetu vikawa ccm B?
Hawa jamaa tutawadhibiti vipi ili wafuate misingi ya vyama vyetu vinavyounda UKAWA? Je, hayatatokea kama ya Mbingu wa Mutharika kule Malawi kwamba baada ya kukorofishana na chama chake akatimka na watu wake na kwenda kuanzisha chama kingine (ingawa hapa kwetu sina uhakika kama sheria zinaruhusu hili).
Hayatatulazimisha kuvaa manguo ya kijani haya? Nawaomba viongozi wetu wa UKAWA wawe makini na hili isije ikawa akina Makongoro, Kimbisa, Mgana n.k. wamekimbilia kwetu ili tuwapitishe kugombea ubunge halafu wakifika bungeni waanze kutusumbua kama Shibuda na Lety!
Mwisho viongozi wetu wamwagize rais wetu mtarajiwa aanze sasa kuvaa gwanda ili tumtambue kwa mavazi!! Kwa mfano kesho anapoenda kuchukua fomu anatakiwa atinge ndani ya Gwanda ili magamba yapukutike!!