UKAWA tafuteni njia nyingine ya kutokea, hii ya Zanzibar mnatudanganya

TataMadiba

JF-Expert Member
Feb 7, 2014
9,866
5,742
Habari za Jumatano wapendwa,

Baada ya UKAWA kuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John Pombe Magufuli ni kisiki cha mpingo, wameamua kuifanya hali ya kisisa Zanzibar kuwa habari ya mjini. Bahati mbaya kabisa wanaifanya kuwa habari ya mjini kwa hoja mfu kabisa.

Eti Rais aingilie kati mgogoro wa Zanzibar kwa sababu vurugu zikitokea yeye ndiye atakayepelekea majeshi kutuliza vurugu hizo. Wanakwenda mbali na kusema hali hiyo ikitokea Rais hatakwepa kusimama mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya ICC kama ilivyokuwa kwa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta(anayeyasema haya ni anayejiita Mwanasheria mahiri).

Hizi ni hoja mfu tu tena za kutapatata.Labda Lissu hajui sababu ya Uhuru Kenyatta kusimama kwenye Mahakama ya ICC. UHURU Kenyatta alisimama ICC siyo kama rais wa Kenya bali kama mmoja wa watu ambao alihamasisha wafuasi wa chama chake kufanya vurugu mwaka 2007, na hakuwa rais wa Kenya wakati huo.Hili swala la Rais Magufuli kupeleka jeshi Zanzibar endo kutakuwa na fyokofyoko, nilishalianzishia uzi humu JF.

JPM ni Amri jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania(Tanzania bara na Zanzibar). Anawajibika kikatiba kuhakikisha watu wake wanaishi kwa amani wao na mali zao. Kwa maaana ya Polisi, JWTZ na vyombo vingine vya ulinzi havina mahusiano yoyote na masuala ya siasa, vitaingia Bungeni, Mahakamani, Ikulu, ndani ya Ofisi ya chama siasa, kanisani, msikitini na mahali popote pale ambapo amani itaonekana kutoweka.

Ghasia zinapotokea Makanisani, misikitini na vyombo hivi kuingilia kati, mbona Lissu na wanasheria mahiri wenzake hawahoji hatua hizo? Majeshi ya Marekani yako Syria, Kongo DRC, Somalia, Elitria, Iraq n.k. Rais Obama wa Marekani alishaonesha juhudi zozote za kuingilia migogoro ya nchi hizo kabla ya kupeleka majeshi? Si hawa Marekani ndiyo baba wa Mahakama ya ICC?

TAFAKURI:
1. UKAWA kutumia hali ya kisiasa Zanzibar kama njia iliyobaki ya wao kupmbana na kasi ya JPM katika kumdhoofisha hakutawaondolea imani Watanzania kwa rais wao. Magufuli atabaki kuwa rais wa Watanzania Wanyonge ambao ndiyo wengi bila kujali itikadi ya vyama vya, dini zao, rangi zao na mahali wanapotokea. JPM kaletwa na Mungu kuwakomboa Watanzania. Tutazidi kumuombea kama ambavyo amekuwa akituomba Watanzania tumuombee ili watu aina ya Lissu washindwe na Walegee.

2. CHADEMA na MAALI SEIF wanaelekea kuwa wanufaika na hali hii ya Zanzibar bila kujali athari wanazozipata Wazanzibari Wenyewe. Bila kuwepo na mgogoro huu CHADEMA ni kama wamefilisika kisiasa kutokana na ukweli kwamba kile ambacho Watanzania walifikiri wangekipata kutoka kwa Wapinzani kabla ya kuingiliwa na Mafisadi sasa wanaelekea kukipata kwa JPM.

Maalim Seif Wazanzibari walishamchoka na wakatamani kuona sura mpya katika siasa za Upinzani ndani ya siasa za Zanzibar, anaamua kutumia mgogoro huu kuzaliwa upya katika siasa za Zanzibar na pia kuendelea kuvuna mlungula kutoka Makundi mbalimbali kwa kisingizio chs kumpa ushirikiano. Ingependeza kama Maali Seif angetangaza kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais Zanzibar ili kuuoneshea Upinzani wa Zanzibar dhamira yake ya kweli kwenye mgogoro huo.
 
Mleta mada acha ushabiki wa kisiasa kwenye maswala yanayohusu usalama as Raia. ..
Ikitokea vurugu Zanzibar wataathirika kina mama ,watoto,wazee na hata wanaume na vijana bila kujali vyama vyao....
Na wengine hata hawana vyama
 
Eti " JPM kaletwa na Mungu kuwakomboa Watanzania"?
Mumeanza kurudia maneno hata tena? Mungu mnayemtaja hapa ni yuleyule aliyekuwa na chaguo lake JK wakati ule?
Kama ni huyohuyo bora nikae kimya nisikilize waungwana wanasemaje.
 
A. Eti Rais aingilie kati mgogoro wa Zanzibar kwa sababu vurugu zikitokea yeye ndiye atakayepelekea majeshi kutuliza vurugu hizo.

UKAWA wapotoshaji sana.Raisi hapeleki majeshi Zanzibar hata siku moja.Majeshi yako kule yamewekwa na katiba ya nchi ambayo inatamka kuwa majeshi ni ya muungano.Majeshi yako kule siku zote.Hata saa hizi yapo hayasubiri kupelekwa wakati wa vurugu tu.JWTZ wako kule,POLISI WAKO KULE,magari ya washa washa yako kule,mabomu yako kule.Na wote hawahitaji ruksa ya raisi kupiga virungu au bomu au risasi jambazi liwe la CUF au CCM lililoko kule liwe linafanya ujambazi wakati wa kupiga kura,kuhesabu kura au wakati wa kutangaza matokeo.

Hili la kusema Raisi anapeleka majeshi ni uzushi wa UKAWA.Yako pande zote za muungano wakati wote na yanaweza enda sehemu yoyote ya muungano kwa mazoezi nk kadiri yapendavyo.Yaweza toka dodoma yakaenda kagera au yakatoka morogoro kwenda mwanza au yakatoka Dar kwenda Zanzibar au yakatoka Zanzibar kwenda arusha.Kutoka sehemu moja kwenda nyingine hawahitaji kibali wala kupelekwa na raisi.Ni shughuli zao za kawaida za kila siku.
 
Eti " JPM kaletwa na Mungu kuwakomboa Watanzania"?
Mumeanza kurudia maneno hata tena? Mungu mnayemtaja hapa ni yuleyule aliyekuwa na chaguo lake JK wakati ule?
Kama ni huyohuyo bora nikae kimya nisikilize waungwana wanasemaje.
Utapanic sana
ukweli ndio huo mpo hoi
hakuna ajenda tena tofauti na Zanzibar
Ninyi mlie mpaka mpasuke Magufuli ndio chaguo la kweli.
Mmekuwa wadogo kama pilitoni
Nshu ya Zanzibar itakapo kwisha
sioni hoja mtakayo izungumza
MKUMBUKE
PALIPO NA MALAIKA SHETANI HAKOSI
 
UKAWA wapotoshaji sana.Raisi hapeleki majeshi Zanzibar hata siku moja.Majeshi yako kule yamewekwa na katiba ya nchi ambayo inatamka kuwa majeshi ni ya muungano.Majeshi yako kule siku zote.Hata saa hizi yapo hayasubiri kupelekwa wakati wa vurugu tu.JWTZ wako kule,POLISI WAKO KULE,magari ya washa washa yako kule,mabomu yako kule.Na wote hawahitaji ruksa ya raisi kupiga virungu au bomu au risasi jambazi liwe la CUF au CCM lililoko kule liwe linafanya ujambazi wakati wa kupiga kura,kuhesabu kura au wakati wa kutangaza matokeo.

Hili la kusema Raisi anapeleka majeshi ni uzushi wa UKAWA.Yako pande zote za muungano wakati wote na yanaweza enda sehemu yoyote ya muungano kwa mazoezi nk kadiri yapendavyo.Yaweza toka dodoma yakaenda kagera au yakatoka morogoro kwenda mwanza au yakatoka Dar kwenda Zanzibar au yakatoka Zanzibar kwenda arusha.Kutoka sehemu moja kwenda nyingine hawahitaji kibali wala kupelekwa na raisi.Ni shughuli zao za kawaida za kila siku.
Hawasumbui tena hawa
wanatapatapa watajutia kununuliwa na Jizi milele
Unapo ishi kwa kuunda unda maneno ili upate kick mwisho wake ni aibu
 
Huwa mtu akiniambia maneno 5,moja likawa la uongo nikajua basi naelewa dhamira yake nzima ni kupotosha ukweli kwa sababu anayoijua yeye!

Huyu mleta mada amesema uongo,kwamba kabla ya Obama kupeleka majeshi kwenye nchi alizotaja,hakuwahi kuingilia migogoro ya nchi hizo na ilipofika wakati wakapeleka majeshi!Hili sio kweli,Marekani na umoja wa mataifa wamekuwa na utaratibu wa kuziwekea nchi vikwazo vya kiuchumi kabla ya kupeleka majeshi!Hii hali ya kuwekewa vikwazo ni hatua ya awali,ni kama Tanzania ilivyonyimwa misaada ya mcc!Iwapo mambo hayatakuwa shwari na violence ikatokea na ikaleta maafa ndio hapo tutaona hatua nyingine!

Kwa hayo machache nasema mleta mada ni muongo na uzi wake ni wa kupuuzwa!
 
Mleta mada acha ushabiki wa kisiasa kwenye maswala yanayohusu usalama as Raia. ..
Ikitokea vurugu Zanzibar wataathirika kina mama ,watoto,wazee na hata wanaume na vijana bila kujali vyama vyao....
Na wengine hata hawana vyama
Haya maneno unatakiwa uwambie akina Lissu na Lowassa ambao kila kukicha wimbo wao ni machafuko na Magaidi Zanzibar, wao ndo wanampango huo.
 
Huwa mtu akiniambia maneno 5,moja likawa la uongo nikajua basi naelewa dhamira yake nzima ni kupotosha ukweli kwa sababu anayoijua yeye!

Huyu mleta mada amesema uongo,kwamba kabla ya Obama kupeleka majeshi kwenye nchi alizotaja,hakuwahi kuingilia migogoro ya nchi hizo na ilipofika wakati wakapeleka majeshi!Hili sio kweli,Marekani na umoja wa mataifa wamekuwa na utaratibu wa kuziwekea nchi vikwazo vya kiuchumi kabla ya kupeleka majeshi!Hii hali ya kuwekewa vikwazo ni hatua ya awali,ni kama Tanzania ilivyonyimwa misaada ya mcc!Iwapo mambo hayatakuwa shwari na violence ikatokea na ikaleta maafa ndio hapo tutaona hatua nyingine!

Kwa hayo machache nasema mleta mada ni muongo na uzi wake ni wa kupuuzwa!
Wewe mbumbumbu kwelikweli eleza vikwazo vilivyowekwa na marekani kwa nchi hizo. Na kama vipo ni kwa maslahi ya Marekani. Wewe ndo unataka kuwapotosha wajinga wenzako
 
Habari za Jumatano wapendwa,

Baada ya UKAWA kuona Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John Pombe Magufuli ni kisiki cha mpingo, wameamua kuifanya hali ya kisisa Zanzibar kuwa habari ya mjini. Bahati mbaya kabisa wanaifanya kuwa habari ya mjini kwa hoja mfu kabisa.

Eti Rais aingilie kati mgogoro wa Zanzibar kwa sababu vurugu zikitokea yeye ndiye atakayepelekea majeshi kutuliza vurugu hizo. Wanakwenda mbali na kusema hali hiyo ikitokea Rais hatakwepa kusimama mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya ICC kama ilivyokuwa kwa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta(anayeyasema haya ni anayejiita Mwanasheria mahiri).

Hizi ni hoja mfu tu tena za kutapatata.Labda Lissu hajui sababu ya Uhuru Kenyatta kusimama kwenye Mahakama ya ICC. UHURU Kenyatta alisimama ICC siyo kama rais wa Kenya bali kama mmoja wa watu ambao alihamasisha wafuasi wa chama chake kufanya vurugu mwaka 2007, na hakuwa rais wa Kenya wakati huo.Hili swala la Rais Magufuli kupeleka jeshi Zanzibar endo kutakuwa na fyokofyoko, nilishalianzishia uzi humu JF.

JPM ni Amri jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania(Tanzania bara na Zanzibar). Anawajibika kikatiba kuhakikisha watu wake wanaishi kwa amani wao na mali zao. Kwa maaana ya Polisi, JWTZ na vyombo vingine vya ulinzi havina mahusiano yoyote na masuala ya siasa, vitaingia Bungeni, Mahakamani, Ikulu, ndani ya Ofisi ya chama siasa, kanisani, msikitini na mahali popote pale ambapo amani itaonekana kutoweka.

Ghasia zinapotokea Makanisani, misikitini na vyombo hivi kuingilia kati, mbona Lissu na wanasheria mahiri wenzake hawahoji hatua hizo? Majeshi ya Marekani yako Syria, Kongo DRC, Somalia, Elitria, Iraq n.k. Rais Obama wa Marekani alishaonesha juhudi zozote za kuingilia migogoro ya nchi hizo kabla ya kupeleka majeshi? Si hawa Marekani ndiyo baba wa Mahakama ya ICC?

TAFAKURI:
1. UKAWA kutumia hali ya kisiasa Zanzibar kama njia iliyobaki ya wao kupmbana na kasi ya JPM katika kumdhoofisha hakutawaondolea imani Watanzania kwa rais wao. Magufuli atabaki kuwa rais wa Watanzania Wanyonge ambao ndiyo wengi bila kujali itikadi ya vyama vya, dini zao, rangi zao na mahali wanapotokea. JPM kaletwa na Mungu kuwakomboa Watanzania. Tutazidi kumuombea kama ambavyo amekuwa akituomba Watanzania tumuombee ili watu aina ya Lissu washindwe na Walegee.

2. CHADEMA na MAALI SEIF wanaelekea kuwa wanufaika na hali hii ya Zanzibar bila kujali athari wanazozipata Wazanzibari Wenyewe. Bila kuwepo na mgogoro huu CHADEMA ni kama wamefilisika kisiasa kutokana na ukweli kwamba kile ambacho Watanzania walifikiri wangekipata kutoka kwa Wapinzani kabla ya kuingiliwa na Mafisadi sasa wanaelekea kukipata kwa JPM.

Maalim Seif Wazanzibari walishamchoka na wakatamani kuona sura mpya katika siasa za Upinzani ndani ya siasa za Zanzibar, anaamua kutumia mgogoro huu kuzaliwa upya katika siasa za Zanzibar na pia kuendelea kuvuna mlungula kutoka Makundi mbalimbali kwa kisingizio chs kumpa ushirikiano. Ingependeza kama Maali Seif angetangaza kujiuzulu nafasi ya Makamu wa Rais Zanzibar ili kuuoneshea Upinzani wa Zanzibar dhamira yake ya kweli kwenye mgogoro huo.
naona lissu na kidomodomo chake ndio atapelekwa icc kwa uchochezi. seif sasa mtu mzima na anaumwa. kina lissu et al wanamwita dar kila siku kumjaza upepo aanzishe vagi zanzibar wao na lowassa wao wanakula kuku dar.
 
Wewe mbumbumbu kwelikweli eleza vikwazo vilivyowekwa na marekani kwa nchi hizo. Na kama vipo ni kwa maslahi ya Marekani. Wewe ndo unataka kuwapotosha wajinga wenzako

Kuna watu hawajui wanafikiri vikwazo vikiwekwa huwa ni kwa maslahi ya nchi husika sio kweli.Mfano IRANI na Iraq iliwekewa vikwazo lengo likiwa makampuni ya kimarekani ya mafuta na gesi yaliyoko Kuwait yawe na ukiritimba wa biashara ya mafuta sababu nchi hizo mbili zilikuwa ndio tishio la kibiashara kwao.Wakaanza ohh!!

Wakitaka kuwekea vikwazo Tanzania kwanza wanajiwazia wao matokeo yatakuweje.Mfano wakiwekea vikwazo Tanzania ndege zao ndio zinaleta watalii kwa maelfu zitakula hasara.Pili Mahoteli makubwa kitalii yaliyoko Zanzibar na Arusha ni ya watu wao yatakula hasara kubwa.Makampuni yao makubwa ya utalii kule kwao yatakula hasara kubwa.

Ndio maana Marekani haithubutu hata siku moja kuiwekea vikwazo China pamoja na kuwa china hakuna demokrasia na nchi ni ya chama kimoja.Wanajua wakithubutu wao na makampuni yao yaliyoko china ndio watakula hasara

Wakipima wakaona itakula kwao hawaweki vikwazo.Haweweki vikwazo kwa kuwa wamevutiwa na sharubu za Seif SHARRIF Hamad
 
RAIS Wa WATANZANIA Wanyonge, JE, ZANZIBAR Hakuna Hao WATANZANIA Wanyonge!!?? MBONA Ninyi Mnatuboa Na VIUZI VYENU Vya KISHOGA!!!! YAANI Huyo MAGUFULI Mnataka Tumuone Kama MUNGU Vile, Kila Kitu Ambacho Anakifanya Hakosei!!! ACHENI UPUMBAVU Wenu, Kwani Miaka Yote Hiyo Ya Uhuru TANZANIA Si Inaongozwa Na CCM, Ilikuwa Ikiongozwa Na Upinzani!!!!!!??? SUALA La Zanzibar Halina Pakulikwepea, Ninyi Zungumzeni Yote Mliyopanga Na Mnayopayuka Tu, Mwisho Wa Siku Tutakuja Kuyaona MATOKEO Yake!! SASA Hivi Si Mnatetea MIPANGO Mkakati Yenu Mliyopanga Ili KUWADANGANYA WATANZANIA Kuwa ZANZIBAR Ina UONGOZI Wa Haki Na HALALI!!!!
 
RAIS Wa WATANZANIA Wanyonge, JE, ZANZIBAR Hakuna Hao WATANZANIA Wanyonge!!?? MBONA Ninyi Mnatuboa Na VIUZI VYENU Vya KISHOGA!!!! YAANI Huyo MAGUFULI Mnataka Tumuone Kama MUNGU Vile, Kila Kitu Ambacho Anakifanya Hakosei!!! ACHENI UPUMBAVU Wenu, Kwani Miaka Yote Hiyo Ya Uhuru TANZANIA Si Inaongozwa Na CCM, Ilikuwa Ikiongozwa Na Upinzani!!!!!!??? SUALA La Zanzibar Halina Pakulikwepea, Ninyi Zungumzeni Yote Mliyopanga Na Mnayopayuka Tu, Mwisho Wa Siku Tutakuja Kuyaona MATOKEO Yake!! SASA Hivi Si Mnatetea MIPANGO Mkakati Yenu Mliyopanga Ili KUWADANGANYA WATANZANIA Kuwa ZANZIBAR Ina UONGOZI Wa Haki Na HALALI!!!!
Swali la kizushi tu pamoja na mapovu yako unayoyatoa: huu mgogoro wa sasa zanzibar unatofauti gani na ule wa 1997? CHADEMA na LISSU hawakuwepo? Si Lissu huyuhuyu aliyesimama Bugeni na kusema CUF ni chama cha Zanzibar na kwamba hawazihitaji kura za Zanzibar kwa sababu kura zao hazilingani hata na za jimbo moja la Dar es Salaam? Leo huo uzalendo wa kuipenda Zanzibar Lissu na Chadema wanautoa wapi?
 
MOTOCHINI na wenzako sitaki hata kuwa quote ila mbona swali language hamjibu?
Mnaposema JPM kaletwa na Mungu kuwakomboa Watanzania, jee ni Mungu yuleyule mliyesema JK ni chaguo lake?
Wewe uliza viswali vyako vya kitoto
lengo lako upewe majibu ya kitoto
na unapo uliza jiulize kwanza mwenyewe swali kama hilo likigeuzwa upande wako unayo majibu!!?

Kifupi
Jk alikuwa mpango wa mungu kuzuia Shetani Lowassa asitupeleke motoni Watanzania

Magufuli pia nimpango wa mungu
kutuletea wakati muafaka
maana Nchi ilitaka kugeuka Janga la Nyumbu
Kila kiongozi ana lakwake
Jk kafanya yake mema
JPM Naye anafanya yake
 
Wewe uliza viswali vyako vya kitoto
lengo lako upewe majibu ya kitoto
na unapo uliza jiulize kwanza mwenyewe swali kama hilo likigeuzwa upande wako unayo majibu!!?

Kifupi
Jk alikuwa mpango wa mungu kuzuia Shetani Lowassa asitupeleke motoni Watanzania

Magufuli pia nimpango wa mungu
kutuletea wakati muafaka
maana Nchi ilitaka kugeuka Janga la Nyumbu
Kila kiongozi ana lakwake
Jk kafanya yake mema
JPM Naye anafanya yake
Umemaliza kazi mkuu.
 
Back
Top Bottom