VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Katika Mtaa wa Kandambili,kulikuwa na wapishi na wauzaji mbalimbali wa vitafunwa. Yaliuzwa maandazi,chapati,kalimati,bagia na vitumbua. Muuzaji mmoja aliitwa Fatuma. Yeye alikuwa anauza vitumbua.
Kutokana na upinzani wa kibiashara pale Kandambili,vitumbua vya Fatuma vilipigwa zengwe. Yakapikwa na kusambazwa majungu. Kuwa haviandaliwi katika mazingira ya usafi;havina sukari;haviivi vizuri na kadhalika. Hakíka,havikuuzika na vilidoda. Si unajua tena majungu na propaganda vilivyo na nguvu!
Akaja Bibiafya. Akakagua wapishi wote. Ni Fatuma tu akaonekana kuwa amekidhi vígezo vya usafi. Waliobaki wote wakapigwa marufuku. Vikabaki vitumbua vya Fatuma tu. WanaKandambili wakamiminika kununua na kusifia. Vitumbua vya Fatuma vikawa tegemezi na mkombozi.
Ndivyo zilivyo hoja za UKAWA juu ya Tume Huru ya Uchaguzi,Kura ya Maoni,Sheria mbalimbali,Katiba Pendekezwa na kadhalika. Tunamsubiri Bibiafya. Hoja za UKAWA ni vitumbua vya Fatuma kabisa.
Happy Good Friday!
Mzee Tupatupa
Kutokana na upinzani wa kibiashara pale Kandambili,vitumbua vya Fatuma vilipigwa zengwe. Yakapikwa na kusambazwa majungu. Kuwa haviandaliwi katika mazingira ya usafi;havina sukari;haviivi vizuri na kadhalika. Hakíka,havikuuzika na vilidoda. Si unajua tena majungu na propaganda vilivyo na nguvu!
Akaja Bibiafya. Akakagua wapishi wote. Ni Fatuma tu akaonekana kuwa amekidhi vígezo vya usafi. Waliobaki wote wakapigwa marufuku. Vikabaki vitumbua vya Fatuma tu. WanaKandambili wakamiminika kununua na kusifia. Vitumbua vya Fatuma vikawa tegemezi na mkombozi.
Ndivyo zilivyo hoja za UKAWA juu ya Tume Huru ya Uchaguzi,Kura ya Maoni,Sheria mbalimbali,Katiba Pendekezwa na kadhalika. Tunamsubiri Bibiafya. Hoja za UKAWA ni vitumbua vya Fatuma kabisa.
Happy Good Friday!
Mzee Tupatupa