Nawasalimi kwa jina la Mwenyezi Mungu.
WANA UKAWA - Wananchi lukuki wako nyuma yenu, pamoja na vitimbwi vingi vya CCM mnavyokutana navyo katika bunge maalumu.
Nachukua nafasi hii kuwakumbusha na kuwashauri yafuatayo:
1. Mko vitani kwa niaba ya wananchi, msitegemee adui kuwaletea mess-tin au beef, au mikate, adui atakutwanga singe, rungu hata risasi. CCM wavyofanya ndiyovita imeanza, kama mnasubiri filimbi mmekwisha.
Mapambano yanambinu kali kamavile kuvamia, ambush na adui akizidiwa atasema maridhiano. KATU CCM HAIWEZI TAKA MARIDHIANO ambapo ina maslahi, inauhakika wa ki-sheria au ki-hoja. Wakitaka Maridhiano kuweni makini sana na hapo, huenda unafiki ukawa ndio msingi mkuu wa maridhiano hayo na baadaye watawageuka. Si mliona maridhiano ya kuruhu Jaji Warioba aanze Kuwasilisha rasimu yalivyowatokea puani! Hivyo nduguzangu hapo ukumbini punguza ustaarabu, zidisha mapambano, vita imeishaanza, Tumemuona kamanda Tundulisu kesha ona adui kamtungua, la sivyo kanuni zingelala zimepinda leo.
2.Mfamaji haachi kutapatapa, Viroja vya CCM wanavyowafanyia nikwakuwa Rasimu ya katiba mpya imewagusa pabaya, ufalme wao uanatishiwa. Nawaomba msiwe na woga wowote wa jeshi kubwa la askari wa miguu wakati nyie mna manowari- (Rasimu ya Katiba) na ndege za kivita - (Nguvu ya hoja). Idadi ya silaha zenu ni ndogo lakini angamizi! Rasimu ya katiba inatambulika kisheri lakini hotuba ya kikwete haina nafasi ya kujadiliwa hata kwenye kamati kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko katiba. Raisi alichelewa kutoa maoni yake kwenye tume ya Jaji Warioba, au labda anafanya Backward Motion. Yeye Kama Kikwete ama kama Taasisi ya Ras alikuwa na nafasi ya kutosha kufanya marekebisho ya hayo aliyoyaita mapungufu ya rasimu ya katiba.
3. UKAWA Mnayodhamana ya kusimamia maboresho maoni ya wananchi yaliyo katiba rasimu ya katiba, hapa sasa, no retreat, no surender, ni mbele kwa mbele. Tengeneza mbinu za kutokubali kubuluzwa kama vile ilivyofanyika wakati Jaji Warioba alifanyiwa wakati ameitwa kuwasilisha rasimu mara ya kwanza. Mkiondoka mtawapotezea wananchi fursa muhimu ambayo huenda ikapatikana kwa gharama kubwa zaidi.
Msikubali kujadili kitu tofaoti na rasimu ya katiba kama inavyoelekezwa na sheria ya mabadiliko ya katiba kifungu 25 na msikubali kuondoka na msikubali kubuluzwa. Ujasiri, Nguvu ya hoja na Sala za Wananchi ndiyo silaha zenu.
Nawatakia kila rakheli komreds!
Mungu Ibariki Zanziba, Mungu Ibariki Tanganyika, Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Africa.
WANA UKAWA - Wananchi lukuki wako nyuma yenu, pamoja na vitimbwi vingi vya CCM mnavyokutana navyo katika bunge maalumu.
Nachukua nafasi hii kuwakumbusha na kuwashauri yafuatayo:
1. Mko vitani kwa niaba ya wananchi, msitegemee adui kuwaletea mess-tin au beef, au mikate, adui atakutwanga singe, rungu hata risasi. CCM wavyofanya ndiyovita imeanza, kama mnasubiri filimbi mmekwisha.
Mapambano yanambinu kali kamavile kuvamia, ambush na adui akizidiwa atasema maridhiano. KATU CCM HAIWEZI TAKA MARIDHIANO ambapo ina maslahi, inauhakika wa ki-sheria au ki-hoja. Wakitaka Maridhiano kuweni makini sana na hapo, huenda unafiki ukawa ndio msingi mkuu wa maridhiano hayo na baadaye watawageuka. Si mliona maridhiano ya kuruhu Jaji Warioba aanze Kuwasilisha rasimu yalivyowatokea puani! Hivyo nduguzangu hapo ukumbini punguza ustaarabu, zidisha mapambano, vita imeishaanza, Tumemuona kamanda Tundulisu kesha ona adui kamtungua, la sivyo kanuni zingelala zimepinda leo.
2.Mfamaji haachi kutapatapa, Viroja vya CCM wanavyowafanyia nikwakuwa Rasimu ya katiba mpya imewagusa pabaya, ufalme wao uanatishiwa. Nawaomba msiwe na woga wowote wa jeshi kubwa la askari wa miguu wakati nyie mna manowari- (Rasimu ya Katiba) na ndege za kivita - (Nguvu ya hoja). Idadi ya silaha zenu ni ndogo lakini angamizi! Rasimu ya katiba inatambulika kisheri lakini hotuba ya kikwete haina nafasi ya kujadiliwa hata kwenye kamati kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko katiba. Raisi alichelewa kutoa maoni yake kwenye tume ya Jaji Warioba, au labda anafanya Backward Motion. Yeye Kama Kikwete ama kama Taasisi ya Ras alikuwa na nafasi ya kutosha kufanya marekebisho ya hayo aliyoyaita mapungufu ya rasimu ya katiba.
3. UKAWA Mnayodhamana ya kusimamia maboresho maoni ya wananchi yaliyo katiba rasimu ya katiba, hapa sasa, no retreat, no surender, ni mbele kwa mbele. Tengeneza mbinu za kutokubali kubuluzwa kama vile ilivyofanyika wakati Jaji Warioba alifanyiwa wakati ameitwa kuwasilisha rasimu mara ya kwanza. Mkiondoka mtawapotezea wananchi fursa muhimu ambayo huenda ikapatikana kwa gharama kubwa zaidi.
Msikubali kujadili kitu tofaoti na rasimu ya katiba kama inavyoelekezwa na sheria ya mabadiliko ya katiba kifungu 25 na msikubali kuondoka na msikubali kubuluzwa. Ujasiri, Nguvu ya hoja na Sala za Wananchi ndiyo silaha zenu.
Nawatakia kila rakheli komreds!
Mungu Ibariki Zanziba, Mungu Ibariki Tanganyika, Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Africa.