mabuti ya kijeshi uyaone mafupi mepesi// yaani kama vile 'simple' toka nduki toka 'race'// kama risasi ya bunduki au jeti/ no kunyuti no kuketi/ wape nafasi wakushuti kama Malcolm X//
usikubali kubaki uwe pimbi upewe kesi//
ikibidi jitose ndani ya dimbwi la kinyesi//
sio suala la uoga kuogopa ukunguru..\\
ila bora kulogwa kuliko kukosa uhuru\\ wapi sheikh Mponda wapi Jenerali Komba/
sirikali sera kali cheza mbali na wajomba/
kimbia,
mitihani imevuja nyie hamjasikia?//
ya nini kusoma huku elimu inanunuliwa//
kimbia,
nchi imeshauzwa hii hamna kusikilizia//
TANESCO,Madini hadi Air Tanzania//
watoto wa uswazi hawana matumaini/
ndoto za ujambazi sababu ya umasikini/
matapeli wenye shahada kila hatua tatu//
makahaba wa miaka kumi na tatu//
maskani kama msitu vicheche na machatu//
usipite pekupeku bila kuvaa viatu//