Ujumbe kwa Waziri wa Elimu na Serikali

Ujumbe kwa Waziri wa Elimu na Serikali

buffaro89

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2016
Posts
592
Reaction score
378
Hongera sana mama, kwa kukalia kiti na mamlaka ya kuamua au kukataa kitu furani ukiwa wewe kama wewe lakini siku zote binadamu hata ungekuwa na elimu kubwa kiasi gani, aimaanishi ndio unaweza ukatoa maamuzi sahihi ya kuiongoza nchi.

Pia kumbuka unao ongoza ni watu na hao watu, wanamatatizo na changamoto zao katika maishayao kwa ujumla.

Kwanini unaweka vikwazo, vingi vingi miongoni mwa watu wanaotaka kujiendeleza kielimu. Huoni tanzania ni nchi pekee inayo kumbatia elimu ya kukalilishwa na inayozalisha wahitimu wanao tegemea kuajiliwa na sio kujiajiri.
maamuzi haya ya elimu, je yamefanyiwa utafiti?

Data sahihi ni pamoja na kuwashirikisha wananchi, hii nchi sio ya watu wachache jamani muwe mnafanya research ni kwanini watu wanafeli,changamoto zipi zinazo wapelekea watu hawa washindwe kufanikiwa! kuferi shure mara nyingine sio kwa sababu mtu hana akiri darasani usisahau nchi yetu ni masikini kuna watu shida zao zinawaathili katika masomo yao, lakini kauli mnazo zitoa kama viongozi. mnawaita ma failers.

Unapandisha GPA ili iweje? boresheni mitaala ya ufundishaji na curriculum za kila level.

Level za elimu ni international recognized, certificate, baada ya hapo ni diploma na baada ya hapo ni degree na kuendelea. sasa hatuelewi vikwazo vinatokana na nini mtu ashindwe kuunganisha anapo toka diploma na kuenda degree.

Mtakuja kugundua kwamba hapo kinacho tafutwa ni status na cheti, lakini baada ya hapo muhitimu huyo hana kingine cha kufanya zaidi ya kutegemea kuajiriwa!

Serikali iumize kichwa kutengeneza wasomi watakao zarisha katika sekta zote na sio ku deal na vitu ambavyo sio kipa umbele sana na impact yake haizarishi chochote.

Mkumbukeni Marehemu Joseph Mungai, jinsi alivyo fanya katika kutoa maamuzi binafsi ya kubadilisha mitahara ya elimu. Alifuta masomo ya biashara,alifuta michezo,aliunganisha masomo ya physics na chemistry kuwa somo moja! lakini mwisho wa siku impact zake zilikuwa ni mbaya kupita kawaida.

Sasa hivi tena makosa yanaludi tena kwa mfumo mwingine unao kuja kama uboreshaji kumbe ni uharibifu. Elimu hizi tumekopi ng'ambo na mitahara ni hivyo hivyo, vitabu ni hivyo hivyo.

Leo hii tanzania tujifanye kama tunaijua sana elimu kuliko hata walio anzisha.
hata meri hatuwezi kutengeneza,electronics hatuwezi kutengeneza,magari na vyombo vyote vyamoto na visivyo vyamoto, tumeshindwa kutengeneza, hata kiwanda cha kusindika nyanya tuu! tumeshindwa,kilimo tumeshindwa, iyo elimu inasaidia kufanya nini sasa kama sio kutafuta status na hazi ya umiliki wa kisomo.tunakumbatia elimu kwa viwango vya juu lakini ni elimu useless.

Uchumi wetu utategemea sana kilimo,lakini mikakati ya kilimo mbona hakuna, masomo ya kilimo mbona hayapewi kipa umbele,secta ya utalihi inakosa afya pia.
tukisema technologia sio kweli, elimu inayo tolewa haina ubora!

Ni hayo tuu! wananchi tuna umia sana pale tunapo ona nchi inaongozwa kama familia za majumbani kwetu.
 
Tatzo kila MTU anakurupuka, waweke mbinu mpya za kuboresha elimu nasio sababu kila siku za ajabu ajabu, waanze upya sio kupoteza MUDA kufukia ya nyuma, kwanza na yy alikua hayaon haya ktk uongoz uliopita? Wamekalia kukosoa wakat walioharb ni wao! Uongoz hovyoo huu!
 
Tatzo kila MTU anakurupuka, waweke mbinu mpya za kuboresha elimu nasio sababu kila siku za ajabu ajabu, waanze upya sio kupoteza MUDA kufukia ya nyuma, kwanza na yy alikua hayaon haya ktk uongoz uliopita? Wamekalia kukosoa wakat walioharb ni wao! Uongoz hovyoo huu!
Kweli mkuuu Upo sahii,,,,
 
Jaman mnajua sheria ya elimu ni ngumu sana ukizingatia huo mswada wake unaangalia nini hasa kwa wachambuzi wa elimu ni kwamba tunapeleka taifa kuwa maskini zaidi kwani kutakuwa na tabaka kubwa sana sana sana na uhalifu utaongezeka na kama endapo anataka kupitisha ikawa sheria basi A level schools ziongezwe ili kupunguza hili wimbi la wanafunzi wanaokosa shule na kuingia kwenye fani nyingine tofauti alafu kikubwa kinachokwamisha ni mitaala yetu bado haijasimama inayumba kila siku lakini pia amefanya tafiti gani zilizopelekea akatoa tamko hilo na je ni nchi gani wamearchieve hicho kitu?
 
Anakazania watu kusoma A level kwa sababu zipi za msingi? mtu aliyemaliza certificate na aliyemaliza unaweza kuwashinda katika soka la ajira? Kwa nn watu wasisomee taaruma zaidi kuliko kusomea kujibu mtihani wa necta na baada ya kurudi nyumbani bila kuwa na ujuzi wowote kichwani? Serikali lazima ijifunze kufanya tafiti na kutoa miongozo yenye tija kwa taifa kuliko kukumbatia mambo tulitolisishwa na vizazi vilivyopita lkn hayana tija kwa maisha ya sasa.
 
Nilitegemea mtu akimaliza six apige diploma kwanza mwaka mmoja ndiyo aende degree tungezalisha wasomi pure kabisa.
 
Back
Top Bottom