Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
JINAMIZI la ufisadi limeendelea kuzitesa taasisi za umma na za viongozi wastaafu, ambapo hivi sasa mradi wa ujenzi wa jengo la kumbukumbu la aliyekuwa Waziri Mkuu mstaafu hayati Rashid Mfaume Kawawa Simba wa Vita, inadaiwa zimetafunwa sh milioni 800 pamoja na vifaa. Fedha na vifaa hivyo vilitokana na harambee iliyoendeshwa mwaka 2008 iliyokuwa na lengo la kukusanya kiasi cha sh bilioni moja ili kujenga jengo la ghorofa tatu katika Kijiji cha Madale, Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Tanzania Daima Jumapili limedokezwa kuwa jengo hilo lilitarajiwa kuwa na ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM), ofisi za kituo cha kutunzia kumbukumbu za uelimishaji jamii kuhusu ugonjwa wa ukimwi, afya ya kina mama na watoto na kumbi za mikutano. Kwa mujibu wa watu walio karibu na familia ya Kawawa, wamebainisha kuwa iliundwa kamati maalumu kwa ajili ya kuratibu michango hiyo lakini mpaka sasa viongozi wa kamati hiyo wamekuwa wakirushiana mpira kuhusu ubadhirifu wa michango iliyokusanywa.
Diwani wa Kata ya Madale, John Moro, ndiye alikuwa mwenyekiti wa kamati hiyo na anatuhumiwa kuhusika na kashfa hiyo iliyoibuliwa na baadhi ya wananchi waliokuwa wakishangazwa na kusuasua kwa ujenzi husika. Baadhi ya wananchi waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili, kwa sharti la kutotaka majina yao yaandikwe, walisema awali wahusika walikwenda kwenye kiwanja kilichotolewa kwa shughuli hiyo na kuchimba mashimo na kuweka saruji pamoja na nondo, ikiwa ni ishara ya ujenzi wa ghorofa. Walidokeza kuwa eneo hilo kwa hivi sasa limegeuka pori kwa kuwa hakuna mwenye kulihudumia tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma. Tanzania Daima Jumapili liliwasiliana na Diwani wa Kata ya Madale, John Moro, kumtaka kujibu tuhuma za kutafuna kiasi cha sh milioni 800 pamoja na vifaa vya ujenzi vilivyopatikana kwenye harambee na baada ya harambee.
Moro alikiri kuhusika na uchangishaji wa fedha katika ujenzi huo lakini alikana kutafuna mamilioni ya fedha na vifaa vya ujenzi wa jengo hilo kama baadhi ya watu wanavyomtuhumu. Alibainisha kuwa sababu kubwa ya kukwama kwa ujenzi huo ni mvutano unaoendelea hivi sasa baina ya kamati yake na familia ya Kawawa inayotaka ujenzi huo ufanyike nyumbani kwake na si kwenye eneo lililotengwa. Msimamo wa familia ndio umetukwamisha, hatuwezi kuhamisha plan iliyokuwapo na kwenda kujenga nyumbani kwa marehemu kitega uchumi kama hiki, ni lazima tuangalie eneo sahihi, si vinginevyo, alisema. Diwani huyo pia alikana kuhusika na uuzaji wa vifaa vya ujenzi yakiwamo matofali 8,000, ambapo alisema aliyekuwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa ndiye aliyehusika na uuzwaji huo. Unajua matofali yalikuwepo lakini aliyekuwa mwenyekiti wangu wa serikali ya mtaa ndiye aliyeuza, mimi sikuwapo wakati biashara husika inafanyika, alisema Moro.
Tanzania Daima Jumapili lilifanikiwa kuzungumza na mwenyekiti huyo aliyetajwa kuhusika na uuzaji wa vifaa hivyo ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Mbelwa, ambaye alisema hahusiki na kashfa hiyo. Mbelwa alimtupia mpira Diwani Moro, kwa madai ndiye anayehusika kuuza tofali, nondo, mifuko ya sarufi pamoja na kutafuna fedha zilizochangwa na wananchi. Alisema Moro aliuza vifaa kwa mkandarasi mmoja aliyekuwa akijenga zahanati iliyopo maeneo ya Madale na fedha zilizopatikana hajazitolea maelezo zilipopelekwa. Alibainisha kuwa tangu ujenzi huo uasisiwe na hayati Kawawa kwa lengo la kuhifadhi kumbukumbu, wengi walifurahia jambo hilo na walitoa michango yao kwa hali na mali. Kimsingi kitendo cha uuzwaji wa vifaa vya ujenzi na matumizi yasiyojulikana ya fedha zilizochangwa kimetukera wengi wetu, ndugu yetu Moro ameuza vifaa hivyo, asikane tuhuma hizi, alisema Mbelwa.
Tanzania Daima Jumapili liliwasiliana na familia ya hayati Kawawa, ambapo mmoja wa watoto wake ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema familia yao inatengwa katika maamuzi yakiwamo ya fedha ambazo zilikuwa zimechangwa na vifaa ambavyo wahisani mbalimbali walitoa. Alisema kutengwa huko kulianza baada ya kuonyesha kutoridhishwa na utunzaji wa kumbukumbu wa kile kinachotolewa na wachangiaji wa mradi huo. Mwenyekiti wa kamati ile ana mambo ya ajabu ajabu sana, kabla ya mzee kufariki dunia alikuwa anaonyesha utu wa kutushirikisha lakini sasa kila akiulizwa juu ya ujenzi, hana majibu yanayoeleweka, zaidi ya kusema utaisha tu, alisema mtoto huyo.
Baadhi ya wananchi waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili walibainisha kuwa hivi sasa wanashindwa kuhoji zilipo fedha na vifaa husika kwa sababu ya kuchoshwa na majibu ya diwani huyo pamoja na vitisho vyake. Walibainisha kuwa waliamua kufikisha kilio chao TAKUKURU ili ifanyie uchunguzi sakata hilo, lakini hadi hivi sasa bado hawajaona uwajibishwaji wa wahusika. Tanzania Daima Jumapili lilifika ofisi za TAKUKURU na kuonana na ofisa aliyekataa kuandikwa jina lake kwa madai kuwa si msemaji wa taasisi hiyo, licha ya kukiri kuiona barua ya malalamiko ya wananchi hao. Ofisa huyo alisema anayeshughulikia suala hilo kwa sasa yuko katika likizo ya uzazi na hajui ni nani aliyekabidhiwa jukumu la kuchunguza sakata hilo.
Tanzania Daima
Tanzania Daima Jumapili limedokezwa kuwa jengo hilo lilitarajiwa kuwa na ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM), ofisi za kituo cha kutunzia kumbukumbu za uelimishaji jamii kuhusu ugonjwa wa ukimwi, afya ya kina mama na watoto na kumbi za mikutano. Kwa mujibu wa watu walio karibu na familia ya Kawawa, wamebainisha kuwa iliundwa kamati maalumu kwa ajili ya kuratibu michango hiyo lakini mpaka sasa viongozi wa kamati hiyo wamekuwa wakirushiana mpira kuhusu ubadhirifu wa michango iliyokusanywa.
Diwani wa Kata ya Madale, John Moro, ndiye alikuwa mwenyekiti wa kamati hiyo na anatuhumiwa kuhusika na kashfa hiyo iliyoibuliwa na baadhi ya wananchi waliokuwa wakishangazwa na kusuasua kwa ujenzi husika. Baadhi ya wananchi waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili, kwa sharti la kutotaka majina yao yaandikwe, walisema awali wahusika walikwenda kwenye kiwanja kilichotolewa kwa shughuli hiyo na kuchimba mashimo na kuweka saruji pamoja na nondo, ikiwa ni ishara ya ujenzi wa ghorofa. Walidokeza kuwa eneo hilo kwa hivi sasa limegeuka pori kwa kuwa hakuna mwenye kulihudumia tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma. Tanzania Daima Jumapili liliwasiliana na Diwani wa Kata ya Madale, John Moro, kumtaka kujibu tuhuma za kutafuna kiasi cha sh milioni 800 pamoja na vifaa vya ujenzi vilivyopatikana kwenye harambee na baada ya harambee.
Moro alikiri kuhusika na uchangishaji wa fedha katika ujenzi huo lakini alikana kutafuna mamilioni ya fedha na vifaa vya ujenzi wa jengo hilo kama baadhi ya watu wanavyomtuhumu. Alibainisha kuwa sababu kubwa ya kukwama kwa ujenzi huo ni mvutano unaoendelea hivi sasa baina ya kamati yake na familia ya Kawawa inayotaka ujenzi huo ufanyike nyumbani kwake na si kwenye eneo lililotengwa. Msimamo wa familia ndio umetukwamisha, hatuwezi kuhamisha plan iliyokuwapo na kwenda kujenga nyumbani kwa marehemu kitega uchumi kama hiki, ni lazima tuangalie eneo sahihi, si vinginevyo, alisema. Diwani huyo pia alikana kuhusika na uuzaji wa vifaa vya ujenzi yakiwamo matofali 8,000, ambapo alisema aliyekuwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa ndiye aliyehusika na uuzwaji huo. Unajua matofali yalikuwepo lakini aliyekuwa mwenyekiti wangu wa serikali ya mtaa ndiye aliyeuza, mimi sikuwapo wakati biashara husika inafanyika, alisema Moro.
Tanzania Daima Jumapili lilifanikiwa kuzungumza na mwenyekiti huyo aliyetajwa kuhusika na uuzaji wa vifaa hivyo ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Mbelwa, ambaye alisema hahusiki na kashfa hiyo. Mbelwa alimtupia mpira Diwani Moro, kwa madai ndiye anayehusika kuuza tofali, nondo, mifuko ya sarufi pamoja na kutafuna fedha zilizochangwa na wananchi. Alisema Moro aliuza vifaa kwa mkandarasi mmoja aliyekuwa akijenga zahanati iliyopo maeneo ya Madale na fedha zilizopatikana hajazitolea maelezo zilipopelekwa. Alibainisha kuwa tangu ujenzi huo uasisiwe na hayati Kawawa kwa lengo la kuhifadhi kumbukumbu, wengi walifurahia jambo hilo na walitoa michango yao kwa hali na mali. Kimsingi kitendo cha uuzwaji wa vifaa vya ujenzi na matumizi yasiyojulikana ya fedha zilizochangwa kimetukera wengi wetu, ndugu yetu Moro ameuza vifaa hivyo, asikane tuhuma hizi, alisema Mbelwa.
Tanzania Daima Jumapili liliwasiliana na familia ya hayati Kawawa, ambapo mmoja wa watoto wake ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema familia yao inatengwa katika maamuzi yakiwamo ya fedha ambazo zilikuwa zimechangwa na vifaa ambavyo wahisani mbalimbali walitoa. Alisema kutengwa huko kulianza baada ya kuonyesha kutoridhishwa na utunzaji wa kumbukumbu wa kile kinachotolewa na wachangiaji wa mradi huo. Mwenyekiti wa kamati ile ana mambo ya ajabu ajabu sana, kabla ya mzee kufariki dunia alikuwa anaonyesha utu wa kutushirikisha lakini sasa kila akiulizwa juu ya ujenzi, hana majibu yanayoeleweka, zaidi ya kusema utaisha tu, alisema mtoto huyo.
Baadhi ya wananchi waliozungumza na Tanzania Daima Jumapili walibainisha kuwa hivi sasa wanashindwa kuhoji zilipo fedha na vifaa husika kwa sababu ya kuchoshwa na majibu ya diwani huyo pamoja na vitisho vyake. Walibainisha kuwa waliamua kufikisha kilio chao TAKUKURU ili ifanyie uchunguzi sakata hilo, lakini hadi hivi sasa bado hawajaona uwajibishwaji wa wahusika. Tanzania Daima Jumapili lilifika ofisi za TAKUKURU na kuonana na ofisa aliyekataa kuandikwa jina lake kwa madai kuwa si msemaji wa taasisi hiyo, licha ya kukiri kuiona barua ya malalamiko ya wananchi hao. Ofisa huyo alisema anayeshughulikia suala hilo kwa sasa yuko katika likizo ya uzazi na hajui ni nani aliyekabidhiwa jukumu la kuchunguza sakata hilo.
Tanzania Daima